Donald Mtetemela vs Valentino Mokiwa

ansebaluu

Member
Aug 15, 2013
21
9
Hawa ni maaskofu wawili wa Anglikana, mmoja mstaafu na pia amewahi kuwa kiongozi wa Anglikana Tanzania. Huyu ni Askofu Donald Mtetemela na sasa ni mjumbe wa bunge maalumu la katiba. Askofu Valentino Mokiwa yeye ni askofu wa Anglikana jimbo la Dar. Sasa tofauti yao ni kubwa.

Mtetemela ambaye amewahi kushika nafasi kubwa kanisani, ameonyesha udhaifu hasa alipochangia bungeni kuhusu kauli ya Lipumba. Alionekana wazi kama ni mtu mwenye mapenzi na CCM, japo yeye anasema yupo neutral, si kweli.

CCM wamempuuza Warioba, Mtetemela hakuongea. Kuna matusi yalikuwa yanaporomoshwa bungeni, hakukemea. Mwenzake, Askofu Mokiwa, akiwa anazungumza kwenye ibada ya Pasaka, hakuwa mnafiki. Aliponda waziwazi wote walioikejeli na kuidharau tume ya katiba. Huyu ndiye kiongozi mathubuti nasubutu kusema.
 
Wote wana akili timamu na wana uhuru wa kuzungumza watakayo alimradi hawavunji sheria za nchi
 
Hawa ni Maaskofu wawili waanglikana mmoja mstaafu na pia amewahi kuwa kiongozi Wa waanglikana Tanzania huyu ni Askofu Donald mtetemela na sasa ni mjumbe Wa bunge maalumu la katiba. Askofu Valentino Mokiwa yeye ni Askofu Wa Anglikana Jimbo la Dar. Sasa tofauti yao ni kubwa Mtetemela ambaye amewahi kushika bafasi kubwa hivyo kanisani ameonyesha udhaifu hasa alipochangia bungeni kuhusu kauli ya Lipumba alionekana wazi kama ni mtu mwenye mapenzi na CCM japo yeye anasema yupo neutral si kweli. Ccm wamempuuza warioba Mtetemela hakuongea. Kuna matusi yalikua yanaporomoshwa bungeni hakukemea lo! Mwenzake Askofu Mokiwa akiwa anazungumza kwenye ibada ya pasaka hakuwa mnafiki aliponda waziwazi wote walioikejeli na kuidharau tume ya katiba. Huyu ndo kiongozi mathubuti nasubutu kusema.

(1) Viongozi wote wawili ni watumishi wa Mungu;
(2) Viongozi wote wawili wamestaafu ukuu wa Uaskofu wa Anglican Church of Tanzania ("ACT");
(3) Kwa bahati mbaya, Askofu Dr. V. Mokiwa alikaa katika ukuu wa Uaskofu wa ACT kwa kipindi kimoja tu, lakini bado ni Askofu Mkuu wa Dayosisi ya Dar es Salaam;
(4) Askofu Donald Mtetemela anayo haki ya kutoa maoni yake juu ya kile anachoona ni sahihi kwake;
(5) Vile vile, maoni ya Askofu Dr. Valentino Mokiwa ni kwasababu anayo haki ya kusema chochote anachoona kinafaa;

Kwahiyo, haitakuwa vema kujaribu kusema kuwa kuna mgawanyiko wa viongozi au misimamo ya viongozi ndani ya taasisi ya ACT.

Mwisho, sitaki kuamini kuwa Askofu D. Mtetemela anaweza kutekwa na CCM kwa tamaa ya fedha au ushawishi wa aina yoyote kwa manufaa ya muda mfupi, kwani ameliongoza kanisa Anglikana vizuri sana na yeye ni mtu wa kanuni.

Hata hivyo, pesa inayo nguvu nyingi sana na mtu yeyote yule anaweza kutekwa na fedha mahali popote na kwa wakati wowote.

Blessings.
 
Mtetemelwa hakuona sahihi kulaani kauli ya Lukuvi kuwa BLK likipitisha Serikali 3 Jeshi litashika nchi, Zanzibar wanataka serikali 3 ili waunde dola ya Kiislamu. Ni mnafiki huyu mzee! Warioba ni mzee kama alivyo Nyerere! CCM wamemdhalilisha ndani na nje ya Bunge lakini Mtetemelwa hakukemea. Askofu opportunistic
 
Hao wote wawili - kila mtu ana jukwaa lake, Askofu Mokiwa - lazima aseme vile kwa kuwa alikuwa jukwaa hilo (Mimbarani) ila kama naye angekuwa mjumbe wa Bunge hili nadhani ungestaajabu ya Musa....,
 
Wote wana akili timamu na wana uhuru wa kuzungumza watakayo alimradi hawavunji sheria za nchi
Pamoja na kuwa na uhuru wa kuzungumza, lakini unatakakiwa kutokuwa manafiki, D. Mtetemela ni msaka tonge amekula kiinua mgongo chakae kimeiisha anatafuta jinsi ya kuishi.
 
Hao wote wawili - kila mtu ana jukwaa lake, Askofu Mokiwa - lazima aseme vile kwa kuwa alikuwa jukwaa hilo (Mimbarani) ila kama naye angekuwa mjumbe wa Bunge hili nadhani ungestaajabu ya Musa....,
 
Leo Mtetemela yuko happy baada ya Mokiwa kupatiwa mrithi wake kwa mbinde...
 
Kwa hiyo
Hawa ni Maaskofu wawili waanglikana mmoja mstaafu na pia amewahi kuwa kiongozi Wa waanglikana Tanzania huyu ni Askofu Donald mtetemela na sasa ni mjumbe Wa bunge maalumu la katiba. Askofu Valentino Mokiwa yeye ni Askofu Wa Anglikana Jimbo la Dar. Sasa tofauti yao ni kubwa Mtetemela ambaye amewahi kushika bafasi kubwa hivyo kanisani ameonyesha udhaifu hasa alipochangia bungeni kuhusu kauli ya Lipumba alionekana wazi kama ni mtu mwenye mapenzi na CCM japo yeye anasema yupo neutral si kweli. Ccm wamempuuza warioba Mtetemela hakuongea. Kuna matusi yalikua yanaporomoshwa bungeni hakukemea lo! Mwenzake Askofu Mokiwa akiwa anazungumza kwenye ibada ya pasaka hakuwa mnafiki aliponda waziwazi wote walioikejeli na kuidharau tume ya katiba. Huyu ndo kiongozi mathubuti nasubutu kusema.

Kwa mawazo yako unaona kuiponda Katiba alivyofanya Askofu Mokiwa ndo ubora wa uongozi?
Ondoa mawazo hayo. Naamini wewe ni muumini wa upande fulani wa chama caha kisiasa.
 
maoni ya Askofu Dr. Valentino Mokiwa ni kwasababu anayo haki ya kusema chochote anachoona kinafaa au hakifai
 
Back
Top Bottom