PreGE2025 Dokezo la Ushauri kwa Viongozi wa CCM

PreGE2025 Dokezo la Ushauri kwa Viongozi wa CCM

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Alloyce PR

JF-Expert Member
Joined
Nov 15, 2020
Posts
595
Reaction score
714
Kwa Ndugu, Stephen Wasira, na CPA Amos Makala.

Kwa heshima na taadhima, naomba kutoa ushauri huu wa bure kwa viongozi wawili muhimu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa Stephen Wasira (Makamu Mwenyekiti wa CCM) na CPA Amos Makala (Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM):

Katika mikutano yenu ya hadhara na majukwaa ya kisiasa, ni vyema kupunguza sana kuzungumzia masuala ya ndani ya CHADEMA, ikiwemo migogoro yao ya ndani, kesi zao mahakamani, au kauli mbiu yao ya kisiasa kama vile “Pasipo Mabadiliko Hakuna Uchaguzi.” Kwa kufanya hivyo, kuna hatari ya kuwaletea umaarufu na nguvu ya maudhui, nyie wenyewe pasipo kujua au pengine mkijua lakini mkadharau athari zake.

Ni wakati sasa kwa CCM kuelekeza nguvu zake katika kunadi sera na ujumbe wa chama cha CCM kwa wananchi. Kama kauli mbiu ya “KAZI NA UTU” ndiyo rasmi, basi ipeni nafasi ya mbele kwa kuielezea kwa kina na kueleza namna inavyogusa maisha ya Watanzania wa kawaida. Kama bado kuna kauli mbiu nyingine mbadala, basi isimamiwe na kuenezwa kikamilifu, mfano, “Oktoba Tuna Tiki” kama ilivyokuwa ikitajwa.

Mwisho kabisa,
Ni muhimu kwa vijana wa UVCCM kuwa hai na makini katika kujibu hoja zinazotolewa na vyama vya upinzani au wananchi mitandaoni na kwenye majukwaa ya kiraia. Tunahitaji vijana, hapa haina budi kuwapa vipaumbele vijana waliokomaa kisiasa na kitaaluma, wanaoweza kuandika na kutoa maudhui yenye majibu thabiti na yenye kueleweka kwa umma juu ya masuala yanayozungumzwa kwenye jamii.

Kwa maneno machache: mzingatie kuonesha nguvu ya CCM kupitia hoja zenu wenyewe badala ya kujenga majukwaa kwa wapinzani. Naomba kuwasilisha. -Alloyce, P.R.
 
UVCCM inajengwa kijeshi zaidi ili kuilinda CCM kama alivyofanya rais wa Malawi Hastings Banda kuwajenga Young Pioneers vijana wa MCP(Malawi Congress Party), hawa walijijenga kijeshi na kuwa na nguvu ya madaraka kuliko jeshi kiasi waliweza kudhibitiwa na jeshi kwa kushitukizwa, huu ndio muelekeo wa UVCCM.
 
UVCCM inajengwa kijeshi zaidi ili kuilinda CCM kama alivyofanya rais wa Malawi Hastings Banda kuwajenga Young Pioneers vijana wa MCP(Malawi Congress Party), hawa walijijenga kijeshi na kuwa na nguvu ya madaraka kuliko jeshi kiasi waliweza kudhibitiwa na jeshi kwa kushitukizwa, huu ndio muelekeo wa UVCCM.
Kama kuna ukweli katika hilo, inabidi wabadilike.
 
Katika mikutano yenu ya hadhara na majukwaa ya kisiasa, ni vyema kupunguza sana kuzungumzia masuala ya ndani ya CHADEMA, ikiwemo migogoro yao ya ndani, kesi zao mahakamani, au kauli mbiu yao ya kisiasa kama vile “Pasipo Mabadiliko Hakuna Uchaguzi.”
Huenda hawana jipya la kuwaambia wananchi tena Mkuu. Miaka 63 sio mchezo.
 
Kwa, Ndugu Stephen Wasira, na CPA Amos Makala.

Kwa heshima na taadhima, naomba kutoa ushauri huu wa bure kwa viongozi wawili muhimu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa Stephen Wasira (Makamu Mwenyekiti wa CCM) na CPA Amos Makala (Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM):

Katika mikutano yenu ya hadhara na majukwaa ya kisiasa, ni vyema kupunguza sana kuzungumzia masuala ya ndani ya CHADEMA, ikiwemo migogoro yao ya ndani, kesi zao mahakamani, au kauli mbiu yao ya kisiasa kama vile “Pasipo Mabadiliko Hakuna Uchaguzi.” Kwa kufanya hivyo, kuna hatari ya kuwaletea umaarufu na nguvu ya maudhui, nyie wenyewe pasipo kujua au pengine mkijua lakini mkadharau athari zake.

Ni wakati sasa kwa CCM kuelekeza nguvu zake katika kunadi sera na ujumbe wa chama cha CCM kwa wananchi. Kama kauli mbiu ya “KAZI NA UTU” ndiyo rasmi, basi ipeni nafasi ya mbele kwa kuielezea kwa kina na kueleza namna inavyogusa maisha ya Watanzania wa kawaida. Kama bado kuna kauli mbiu nyingine mbadala, basi isimamiwe na kuenezwa kikamilifu, mfano, “Oktoba Tuna Tiki” kama ilivyokuwa ikitajwa.

Mwisho kabisa,
Ni muhimu kwa vijana wa UVCCM kuwa hai na makini katika kujibu hoja zinazotolewa na vyama vya upinzani au wananchi mitandaoni na kwenye majukwaa ya kiraia. Tunahitaji vijana, hapa haina budi kuwapa vipaumbele vijana waliokomaa kisiasa na kitaaluma, wanaoweza kuandika na kutoa maudhui yenye majibu thabiti na yenye kueleweka kwa umma juu ya masuala yanayozungumzwa kwenye jamii.

Kwa maneno machache: mzingatie kuonesha nguvu ya CCM kupitia hoja zenu wenyewe badala ya kujenga majukwaa kwa wapinzani. Naomba kuwasilisha. -Alloyce, P.R.
Kijana mmoja wa CHADEMA nisawa na vijana buku wa uv CCM
 
Kazi na utu upi ilhali watu wanauwawa hadharani na hakemei?

Unaanzaje kusema ana utu mbele ya JAMII?

Mtkuwa mmechanganyikiwa huko Lumumba trust me!
Nchi Gani hawafi. Sema nyumbu muache kumalizana
 
UVCCM inajengwa kijeshi zaidi ili kuilinda CCM kama alivyofanya rais wa Malawi Hastings Banda kuwajenga Young Pioneers vijana wa MCP(Malawi Congress Party), hawa walijijenga kijeshi na kuwa na nguvu ya madaraka kuliko jeshi kiasi waliweza kudhibitiwa na jeshi kwa kushitukizwa, huu ndio muelekeo wa UVCCM.
Viongozi wote wa CCM hawana hoja za kuzungumzia zaidi ya Chadema, hivi sasa CCM haina wanasiasa wengi wamejiingiza CCM kiajira ya upigadebe.
 
Kwa Ndugu, Stephen Wasira, na CPA Amos Makala.

Kwa heshima na taadhima, naomba kutoa ushauri huu wa bure kwa viongozi wawili muhimu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa Stephen Wasira (Makamu Mwenyekiti wa CCM) na CPA Amos Makala (Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM):

Katika mikutano yenu ya hadhara na majukwaa ya kisiasa, ni vyema kupunguza sana kuzungumzia masuala ya ndani ya CHADEMA, ikiwemo migogoro yao ya ndani, kesi zao mahakamani, au kauli mbiu yao ya kisiasa kama vile “Pasipo Mabadiliko Hakuna Uchaguzi.” Kwa kufanya hivyo, kuna hatari ya kuwaletea umaarufu na nguvu ya maudhui, nyie wenyewe pasipo kujua au pengine mkijua lakini mkadharau athari zake.

Ni wakati sasa kwa CCM kuelekeza nguvu zake katika kunadi sera na ujumbe wa chama cha CCM kwa wananchi. Kama kauli mbiu ya “KAZI NA UTU” ndiyo rasmi, basi ipeni nafasi ya mbele kwa kuielezea kwa kina na kueleza namna inavyogusa maisha ya Watanzania wa kawaida. Kama bado kuna kauli mbiu nyingine mbadala, basi isimamiwe na kuenezwa kikamilifu, mfano, “Oktoba Tuna Tiki” kama ilivyokuwa ikitajwa.

Mwisho kabisa,
Ni muhimu kwa vijana wa UVCCM kuwa hai na makini katika kujibu hoja zinazotolewa na vyama vya upinzani au wananchi mitandaoni na kwenye majukwaa ya kiraia. Tunahitaji vijana, hapa haina budi kuwapa vipaumbele vijana waliokomaa kisiasa na kitaaluma, wanaoweza kuandika na kutoa maudhui yenye majibu thabiti na yenye kueleweka kwa umma juu ya masuala yanayozungumzwa kwenye jamii.

Kwa maneno machache: mzingatie kuonesha nguvu ya CCM kupitia hoja zenu wenyewe badala ya kujenga majukwaa kwa wapinzani. Naomba kuwasilisha. -Alloyce, P.R.
Haisaidii kitu.
CCM tayari imekwisha kuwa na kasoro kubwa sana ndani yake.
Hata wapake marashi kiasi gani, uvundo hauwezi kufichika.

WaTanzania wanaona maovu yote yanayo endelea, huku CCM hao hao, na viongozi hao uliowataja wakiimba wimbo wa AMANI!
Amani ipi, ambayo, watu kusema maneno tu dhidi ya viongozi au chama hukumu yake inakuwa kutekwa, kupotezwa, au kuuliwa!
Mkuu 'Aloloyce, P.R.', bila kutaka kukuchosha na maelezo ya maovu mengi yaliyofanywa na hicho chama; napenda nikukumbushe tu mawili ya mwisho hapa.
CCM kama chama cha siasa, kimebaki kama dubwasha tu sasa hivi, ambalo limechukuliwa na kundi (GENGE) la watu wanaopigana kufa na kupona kumsalimisha Samia Suluhu Hassan abaki madarakani kwa njia zozote na gharama yoyote. Hizo sera na mambo unayozungumzia wewe hapo juu GENGE hilo, na Samia mwenyewe, wamekwisha hitimisha kuwa haziwezi kutimiza lengo hilo.
Hata huko huko ndani ya dubwasha hilo la CCM, hukuona jinsi walivyo mpigisha chenga Samia katika uteuzi wa mgombea wa urais?
Kama unaelewa hivyo, kwa nini sasa uje hapa na kutaka kuaminisha watu kwamba CCM wanaweza tena kushinda uchaguzi bila ya kufanya yaleyale ya wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa?
Kwa akili yako wewe bado unaamini kwamba pakiwepo na uchaguzi HURU na wa HAKI, CCM watashinda na hizo sera unazowashauri wazitumie?

Sasa fahamu kwamba, jambo moja lililobaki kwa waTanzania ni hili la NO REFORM, NO ELECTION. Hiyo ndiyo taarifa unayotakiwa kuwaeleza wenzio huko kwenye dubwasha lenu lililotekwa na kundi la wahuni kwa manufaa yao na siyo manufaa ya nchi.
 
Kwa Ndugu, Stephen Wasira, na CPA Amos Makala.

Kwa heshima na taadhima, naomba kutoa ushauri huu wa bure kwa viongozi wawili muhimu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa Stephen Wasira (Makamu Mwenyekiti wa CCM) na CPA Amos Makala (Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM):

Katika mikutano yenu ya hadhara na majukwaa ya kisiasa, ni vyema kupunguza sana kuzungumzia masuala ya ndani ya CHADEMA, ikiwemo migogoro yao ya ndani, kesi zao mahakamani, au kauli mbiu yao ya kisiasa kama vile “Pasipo Mabadiliko Hakuna Uchaguzi.” Kwa kufanya hivyo, kuna hatari ya kuwaletea umaarufu na nguvu ya maudhui, nyie wenyewe pasipo kujua au pengine mkijua lakini mkadharau athari zake.

Ni wakati sasa kwa CCM kuelekeza nguvu zake katika kunadi sera na ujumbe wa chama cha CCM kwa wananchi. Kama kauli mbiu ya “KAZI NA UTU” ndiyo rasmi, basi ipeni nafasi ya mbele kwa kuielezea kwa kina na kueleza namna inavyogusa maisha ya Watanzania wa kawaida. Kama bado kuna kauli mbiu nyingine mbadala, basi isimamiwe na kuenezwa kikamilifu, mfano, “Oktoba Tuna Tiki” kama ilivyokuwa ikitajwa.

Mwisho kabisa,
Ni muhimu kwa vijana wa UVCCM kuwa hai na makini katika kujibu hoja zinazotolewa na vyama vya upinzani au wananchi mitandaoni na kwenye majukwaa ya kiraia. Tunahitaji vijana, hapa haina budi kuwapa vipaumbele vijana waliokomaa kisiasa na kitaaluma, wanaoweza kuandika na kutoa maudhui yenye majibu thabiti na yenye kueleweka kwa umma juu ya masuala yanayozungumzwa kwenye jamii.

Kwa maneno machache: mzingatie kuonesha nguvu ya CCM kupitia hoja zenu wenyewe badala ya kujenga majukwaa kwa wapinzani. Naomba kuwasilisha. -Alloyce, P.R.
Makala na Wassira nje ya Chadema wana' lipi la kuwa ambia Watanganyika
 
Back
Top Bottom