Patriote
JF-Expert Member
- Jul 13, 2011
- 1,718
- 1,047
SUALA la maslahi ya wabunge jana liliibuka tena wakati wabunge walipokutana kupewa maelekezo kuhusu mkutano wa tano, huku wabunge wa CCM na wale wa upinzani wakionekana kuwa na kauli moja ya kudai maslahi zaidi. Hivi sasa wabunge wanalipwa mshahara wa Sh2.3 milioni kabla ya kukatwa kodi, kiwango ambacho wanadai hakilingani na kazi wanazofanya na kwamba, kiwango hicho kimepitwa na wakati kutokana na kupanda kwa gharama za maisha.
1.Hoja: Kiwango cha mshahara tunaolipwa sasa kiliwekwa muda mrefu na inawezekana wakati huo kilikuwa kikitosheleza, lakini kimebakia hapo kwa muda mrefu licha ya watumishi wengine viwango vyao kubadilika, sasa tunadhani ni wakati mwafaka jambo hili kufikiriwa, alisema mmoja wa wabunge aliyehudhuria kikao hicho.
Maoni yangu: Kama kiwango cha Tsh 2.3M kiliwekwa muda mrefu, je mmewafikiria mwananchi wa kima cha chini ambao toka nchi imepata uhuru hadi leo hajafikia mshahara wa Tsh 130,000/= kwa mwezi???Mnajua kuwa viwango vya nyongeza ya watumishi wa kima cha chini haizidigi Tsh 10,000 kwa ongezeko??Wabunge mna Posho zaid ya mara mbili ya mishahara yenu, mwananchi huyu KCC hana hata Posho moja yaani hata posho ya nauli ya kumfikisha kazini. Hivyo mshahara anaolipwa kwa ajili ya familia yake inabidi atenge nauli ya kwendea kazini. Mnaona ni sawa????Kwanini msimfikirie huyu KCC kuongezewa mshahara na kulipwa posho muhimu????
2. Hoja: Hapa nina mialiko 26 ya kwenda kuchangia ujenzi wa shule na shughuli nyingine za maendeleo kule Rombo, zote hizi zinanihitaji kama mbunge nitoe fedha, sasa jamani fedha hizi zinatoka wapi,? chanzo chetu kilimnukuu mbunge huyo akihoji na kuungwa mkono na wabunge wengi. Aidha alisema kuwa wabunge hukutana na kero ya wananchi kuomba fedha ili wakatatue matatizo yao mbalimbali nakwamba ni vigumu kukwepa jukumu hilo kutokana na hali ya maisha ilivyo sasa nchini.
Maoni yangu: Huyu ndo kaungea upupu kabisa na kawadhalilisha wananchi wake wa Rombo. Hivi kweli mbunge unaweza kujenga hoja ya kibabaishaji kama hii?? Wananchi wanahitaji wawezeshwe kuvua samaki sio uwape samaki na kujenga utegemezi kwako. Mambo ya kadi za mialiko yako ni personal issues. Huwezi wataka wananchi watoe kodi zao eti ili wewe uchangie watu wako kitchen party. huu ni upuuzi kabisa.
3. Hoja: Mbunge wa Mbulu (Chadema), Mustafa Akunaay, ambaye alimuunga mkono Selasini akisema malipo ya mbunge hayalingani na wajibu wake kwa umma.
Maoni yangu: Wabunge wengi wanatumia hiki kama kichaka, ni majukumu gani ya bunge mnayotekeleza bila kulipwa Posho nyinyi???Mbona mnalipwa posho hata mkitekeleza majukumu ya msingi ya ajira yenu-Double payment??Ukikaa kikao cha kamati unalipwa posho, Ukikaa kikao cha bunge unalipwa posho, ukitumwa kazi yoyote ya bunge unalipwa posho nono tu, kila kitu ninyi ni posho, ni posho, ni posho. Je mnataka nini zaidi kama sio ulafi na ubinafsi???
4 Hoja: Malipo yetu ni kidogo sana, hayatoshelezi kabisa lakini wananchi tunaowawakilisha hawatuelewi katika hili, maana wanadhani tuna fedha nyingi, sasa hapa kuna tatizo. Nadhani kuwapo utaratibu wa kuwaelimisha, wajue hata kazi nyingine tunazofanya siyo wajibu wetu ila tunajitolea na nyingine hizi zina gharama kubwa, alinukuliwa Lusinde.
Maoni yangu: kwani unalazimishwa ujitolee??kwa nini usiache???kama kazi si yako na umeamua kuifanya kwa hiari yako kwa kujitolea kwanini unapiga mayowe uongezewe posho kwa kufanya kazi isiyo yako???na anayepaswa kuifanya hiyo kazi yupo wapi hadi umfanyie wewe???je wewe huna kazi zako za kufanya hadi ufanyie wenzako???Je mimi nikimsaidia kazi mzazi wangu nyumbani, nije kuiomba serikali iniongezee mshahara na posho kwa vile nimemsaidia mzee wangu kazi nyumbani???Ujengaji hoja wa aina hii unatia shaka sana, hasa kama utatoka kwa mtu aliyekabidhiwa jukumu zito la kutunga sheria za nchi.
5. Hoja: Spika kwa mujibu wa taarifa hizo naye aliwalaumu baadhi ya wabunge ambao wamekuwa vinara wa kutangaza kuwa maslahi ya wabunge ni makubwa, ilhali wakifahamu fedha hizo ni kidogo hasa ikilinganishwa na wabunge wa nchi jirani.
Maoni yangu: Spika sio kila wanachofanya wenzetu wa nje basi na sisi lazima tuige. Anataka kusema wabunge wa mabunge ya nchi jirani wakitembea uchi basi na wa hapa kwetu nao sharti watembee uchi, bunge la kenya likikataa kupitisha bajeti yao basi na sisi hivyo hivyo. Spika anajifanya hajui kuwa uchumi wa nchi upo dhohofu lihali, Spika anaona productivity yetu na ya wenzetu zipo sawa. Mbona hamjalinganisha viwango vya chini vya mishahara na vya nchi jirani???
Hapa Spika umejitia aibu na kudhalilisha hicho kiti na wale waliokupa hicho kiti mana mnaonekana wote thinking yenu ni ya aina moja. Hivi kweli sababu ya kuongezwa posho na mishahara iwe tu kwa vile wa Kenya wanalipwa zaidi?Naimani mawazo ya namna hii wachunguzi wa mambo ndo wanaiita poor thinking.
WanaJF naomba mawazo yenu je kwa hoja hizi za wabunge wetu wanafaa kuongezewa Posho na Mishahara???Na kama wakijiongezea nini kifanyike ili wote tupandishiwe mishahara na tuanze kupewa posho za msingi km Posho za nauli, nyumba, likizo n.k. mana kama kushuka kwa thamani ya shilingi kumeshuka kwa wote, kama gharama za maisha zimepanda kwa wote na kama kuwajibika nadhani inawezekana wananchi wa chini tunawajibika kuliko wabunge. Naomba kuwasilisha.
Source Mwananchi 09/11/2011
1.Hoja: Kiwango cha mshahara tunaolipwa sasa kiliwekwa muda mrefu na inawezekana wakati huo kilikuwa kikitosheleza, lakini kimebakia hapo kwa muda mrefu licha ya watumishi wengine viwango vyao kubadilika, sasa tunadhani ni wakati mwafaka jambo hili kufikiriwa, alisema mmoja wa wabunge aliyehudhuria kikao hicho.
Maoni yangu: Kama kiwango cha Tsh 2.3M kiliwekwa muda mrefu, je mmewafikiria mwananchi wa kima cha chini ambao toka nchi imepata uhuru hadi leo hajafikia mshahara wa Tsh 130,000/= kwa mwezi???Mnajua kuwa viwango vya nyongeza ya watumishi wa kima cha chini haizidigi Tsh 10,000 kwa ongezeko??Wabunge mna Posho zaid ya mara mbili ya mishahara yenu, mwananchi huyu KCC hana hata Posho moja yaani hata posho ya nauli ya kumfikisha kazini. Hivyo mshahara anaolipwa kwa ajili ya familia yake inabidi atenge nauli ya kwendea kazini. Mnaona ni sawa????Kwanini msimfikirie huyu KCC kuongezewa mshahara na kulipwa posho muhimu????
2. Hoja: Hapa nina mialiko 26 ya kwenda kuchangia ujenzi wa shule na shughuli nyingine za maendeleo kule Rombo, zote hizi zinanihitaji kama mbunge nitoe fedha, sasa jamani fedha hizi zinatoka wapi,? chanzo chetu kilimnukuu mbunge huyo akihoji na kuungwa mkono na wabunge wengi. Aidha alisema kuwa wabunge hukutana na kero ya wananchi kuomba fedha ili wakatatue matatizo yao mbalimbali nakwamba ni vigumu kukwepa jukumu hilo kutokana na hali ya maisha ilivyo sasa nchini.
Maoni yangu: Huyu ndo kaungea upupu kabisa na kawadhalilisha wananchi wake wa Rombo. Hivi kweli mbunge unaweza kujenga hoja ya kibabaishaji kama hii?? Wananchi wanahitaji wawezeshwe kuvua samaki sio uwape samaki na kujenga utegemezi kwako. Mambo ya kadi za mialiko yako ni personal issues. Huwezi wataka wananchi watoe kodi zao eti ili wewe uchangie watu wako kitchen party. huu ni upuuzi kabisa.
3. Hoja: Mbunge wa Mbulu (Chadema), Mustafa Akunaay, ambaye alimuunga mkono Selasini akisema malipo ya mbunge hayalingani na wajibu wake kwa umma.
Maoni yangu: Wabunge wengi wanatumia hiki kama kichaka, ni majukumu gani ya bunge mnayotekeleza bila kulipwa Posho nyinyi???Mbona mnalipwa posho hata mkitekeleza majukumu ya msingi ya ajira yenu-Double payment??Ukikaa kikao cha kamati unalipwa posho, Ukikaa kikao cha bunge unalipwa posho, ukitumwa kazi yoyote ya bunge unalipwa posho nono tu, kila kitu ninyi ni posho, ni posho, ni posho. Je mnataka nini zaidi kama sio ulafi na ubinafsi???
4 Hoja: Malipo yetu ni kidogo sana, hayatoshelezi kabisa lakini wananchi tunaowawakilisha hawatuelewi katika hili, maana wanadhani tuna fedha nyingi, sasa hapa kuna tatizo. Nadhani kuwapo utaratibu wa kuwaelimisha, wajue hata kazi nyingine tunazofanya siyo wajibu wetu ila tunajitolea na nyingine hizi zina gharama kubwa, alinukuliwa Lusinde.
Maoni yangu: kwani unalazimishwa ujitolee??kwa nini usiache???kama kazi si yako na umeamua kuifanya kwa hiari yako kwa kujitolea kwanini unapiga mayowe uongezewe posho kwa kufanya kazi isiyo yako???na anayepaswa kuifanya hiyo kazi yupo wapi hadi umfanyie wewe???je wewe huna kazi zako za kufanya hadi ufanyie wenzako???Je mimi nikimsaidia kazi mzazi wangu nyumbani, nije kuiomba serikali iniongezee mshahara na posho kwa vile nimemsaidia mzee wangu kazi nyumbani???Ujengaji hoja wa aina hii unatia shaka sana, hasa kama utatoka kwa mtu aliyekabidhiwa jukumu zito la kutunga sheria za nchi.
5. Hoja: Spika kwa mujibu wa taarifa hizo naye aliwalaumu baadhi ya wabunge ambao wamekuwa vinara wa kutangaza kuwa maslahi ya wabunge ni makubwa, ilhali wakifahamu fedha hizo ni kidogo hasa ikilinganishwa na wabunge wa nchi jirani.
Maoni yangu: Spika sio kila wanachofanya wenzetu wa nje basi na sisi lazima tuige. Anataka kusema wabunge wa mabunge ya nchi jirani wakitembea uchi basi na wa hapa kwetu nao sharti watembee uchi, bunge la kenya likikataa kupitisha bajeti yao basi na sisi hivyo hivyo. Spika anajifanya hajui kuwa uchumi wa nchi upo dhohofu lihali, Spika anaona productivity yetu na ya wenzetu zipo sawa. Mbona hamjalinganisha viwango vya chini vya mishahara na vya nchi jirani???
Hapa Spika umejitia aibu na kudhalilisha hicho kiti na wale waliokupa hicho kiti mana mnaonekana wote thinking yenu ni ya aina moja. Hivi kweli sababu ya kuongezwa posho na mishahara iwe tu kwa vile wa Kenya wanalipwa zaidi?Naimani mawazo ya namna hii wachunguzi wa mambo ndo wanaiita poor thinking.
WanaJF naomba mawazo yenu je kwa hoja hizi za wabunge wetu wanafaa kuongezewa Posho na Mishahara???Na kama wakijiongezea nini kifanyike ili wote tupandishiwe mishahara na tuanze kupewa posho za msingi km Posho za nauli, nyumba, likizo n.k. mana kama kushuka kwa thamani ya shilingi kumeshuka kwa wote, kama gharama za maisha zimepanda kwa wote na kama kuwajibika nadhani inawezekana wananchi wa chini tunawajibika kuliko wabunge. Naomba kuwasilisha.
Source Mwananchi 09/11/2011