Dodoma: Bunge la Bajeti kuanza kesho na kumalizika tarehe 28 Juni 2019

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,890
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzani linatarajia kuanza mkutano wake wa kumi na tano siku ya kesho, Aprili 2 huku mkutano huo ukitarajiwa kumalizika tarehe 28 Juni mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa ya Bunge, mkutano huo utakuwa mahsusi kwa ajili ya kujadili utekelezwaji wa bajeti za wizara kwa mwaka wa fedha 2018/19 pamoja na mapato na matumizi ya serikali kwa mwaka wa fedha 2019/20.

Kwenye mkutano huo, wastani wa maswali 515 ya kawaida yanatarajiwa kuulizwa na kujibiwa na serikali huku wastani wa maswali 88 ya papo kwa papo yakitarajiwa kuulizwa kwa waziri mkuu siku za Alhamisi.

Sambamba na maswali hayo pia mkutano huo wa kumi na tano unatarajiwa kujadili hotuba ya hali ya uchumi wa taifa na bajeti ya serikali itakayowasilishwa na wizara ya fedha na mipango.

Miswada miwili ya sheria ya fedha za matumizi ya mwaka 2019 (The Appropriation Bill, 2019) na Muswada wa Sheria ya Fedha mwaka 2019 (The Finance Bill, 2019) pia inatarajiwa kujadiliwa na kupitishwa.
 
Baadhi ya Mawizara hata 40% ya bajeti hawakupata lakini pesa ya kununua wachumia tumbo haikosi. Nangoja kwa hamu kuu kuzisoma details za ripoti ya CAG Assad bila ya shaka kuna madudu ya kutisha sana.
Hivi hatuwezi kuidukua ile kabla haijachakachuliwa ?
 
Eti Binge linakutana kutekeleza bajeti wakati tunajua anayepanga pesa gani itoke hazina na ufanye kazi gani Ni jiwe!
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzani linatarajia kuanza mkutano wake wa kumi na tano siku ya kesho, Aprili 2 huku mkutano huo ukitarajiwa kumalizika tarehe 28 Juni mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa ya Bunge, mkutano huo utakuwa mahsusi kwa ajili ya kujadili utekelezwaji wa bajeti za wizara kwa mwaka wa fedha 2018/19 pamoja na mapato na matumizi ya serikali kwa mwaka wa fedha 2019/20.

Kwenye mkutano huo, wastani wa maswali 515 ya kawaida yanatarajiwa kuulizwa na kujibiwa na serikali huku wastani wa maswali 88 ya papo kwa papo yakitarajiwa kuulizwa kwa waziri mkuu siku za Alhamisi.

Sambamba na maswali hayo pia mkutano huo wa kumi na tano unatarajiwa kujadili hotuba ya hali ya uchumi wa taifa na bajeti ya serikali itakayowasilishwa na wizara ya fedha na mipango.

Miswada miwili ya sheria ya fedha za matumizi ya mwaka 2019 (The Appropriation Bill, 2019) na Muswada wa Sheria ya Fedha mwaka 2019 (The Finance Bill, 2019) pia inatarajiwa kujadiliwa na kupitishwa.

Dunia nzima imedharau mno bunge la kibongo
 
Bajeti ziheshimiwe, unakuta researcher kwenye sekta mfano, kilimo, mifugo, afya unakaa ofisini kama kwenye kijiwe cha kahawa. Huna hizo pesa za kufanyia utafiti, labda zote zinatumiwa na vigogo kulipana per diem na safari za dodoma. Let us get serious, tuache usanii...
 
Kwa hali ya nchi yetu ilipo fikia, watu wengi wanajua binge halina faida yoyote kama ilivyo uchaguzi. Sasa wanatafakari njia nyingine ya kujitawala. Haya yote yamelazimishwa na Serikali hasa ya awamu hii.
 
Back
Top Bottom