Dkt. Slaa atua na kutoa maoni yake kupitia Radio One kuhusu hali ya siasa nchini

Dr W. Slaa kaingia TZ jana Jumanne 10/03 usiku. Leo amefanya interview kwenye kipindi cha "Kumepambazuka" cha Radio One.

Amezungumza mengi kama vile diplomasia ya uchumi nk ila kuhusu siasa hizi ni dondoo muhimu kwenye interview hiyo:

1. Alijiuzulu siasa za vyama (active party politics). Hajarudi CCM na hategemei kurudi CCM. Si lazima arudi CCM (awe mwanachama) ili alitumikie taifa lake.Yeye kule Sweden hamuwakilishi mwenyekiti wa CCM, anamuwakilisha Rais.

2. Slaa anasema kama wapinzani walishindwa kuiondoa CCM 2015 hawataweza kuiondoa tena. Chama tawala kimebeba na kutekeleza agenda iliyoipa umaarufu upinzani 2015. Anasema upinzani unajenga mawazo chama tawala kinatekeleza. Hakuna kosa kwa chama tawala kuiba mawazo. Vyama vya upinzani vinapewa ruzuku kuwa "Viwanda vya Mawazo" ambayo chama tawala kinayatumia sababu upinzani hawana mahali (platform) ya kutekeleza mawazo yao.

3. Slaa anasema hakuna waraka (decree) unaowazuia wapinzani kuendesha shughuli zao. Serikali haifanyi kazi kwa matamko. Anasema kilichotokea ni kwamba kuna matamko ya upinzani (Chadema) yalileta sura ya kuchafua utulivu (Civil Disobedience). Walisema wataandamana kila kona - mkoa hadi mkoa, kijiji hadi Kijiji, mtaa hadi mtaa. Anasema kwa tafsiri yake, sheria inayotumika kudhibiti shughuli za wapinzani ni ya kipolisi sababu ikifika mahali unakwamisha mambo hauwezi kuachwa.

Anatoa mfano ofisi yake ya ubalozi Sweden ilipokea taarifa ya "Maandamano ya Mange Kimambi." Mamlaka ya Serikali ya Sweden ilitaka maelezo ya kina (details) za waandamanaji ikiwemo majina yao. Mamlaka hiyo ilielekeza idadi yao, sehemu ya kusimama na masharti mengine kama kutotumia vipaza sauti, nk. Anasema hii ni kuonyesha hata kwenye nchi kama Sweden, masharti yapo ili kuepuka kusumbua wananchi. Kati ya wale 100 walioruhusiwa kuandamana ni 6 tu walijitokeza.

Slaa anasema aliwaasa Chadema wajirekebishe kuhusu hili ila wameshindwa. Anasema ukombozi haupatikani kwa "Red Brigade" kuwa barabarani.

Anawaasa wanaotaka kujua Chadema ilipoanza kukosea wasome kitabu chake cha "Nyuma ya Pazia"
Msaliti mkubwa huyo, ndiyo maana upadili ulimshinda!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dr Slaa ni mtu makini sana, ni muongo na mnafiki atakayesema Dr., hakuwa the biggest asset alipokuwa chadema.

Ubaya wa ndugu zetu huwa hawafanyi proper crisis analysis na kujirekebisha. Alichokisema hapa ni muhimu sana na kinaeleweka.

Sent using Jamii Forums mobile app

Mtu makini anayezungumza mapungufu ya upinzani tu, huku akifumbia macho ya ccm. Kimsingi anatumiwa akidhani ataweza kuvuta na kubadilisha mitazamo ya wapinzani.
 
Hoja namba moja Dr. Slaa; hawezi kumtofautisha Rais na Mwenyekiti wa CCM, huyo ni mtu mmoja japo ana vyeo tofauti, kusema unamfanyia kazi Rais na sio M/kiti wa CCM ni uongo kwasababu kwenye ufanyaji kazi wake atakuwa analinda interest za M/kiti wa CCM, ambae ndie bosi wa Dr. Slaa; mfano ni pale alipoulizwa maoni yake baada ya Lissu kupigwa risasi, akajibu ili kumfurahisha M/kiti wa CCM ambae ndie bosi wake; alijibu kwamba Lissu sio wa kwanza kupigwa risasi. Hili jibu kimsingi alilenga kumfurahisha M/kiti wa CCM.

Hoja mamba mbili nimeipenda; na hii kina Sabaya na wenzake waisome vizuri, zile kelele zao kwamba wapinzani waoneshe walichofanya leo zimepewa jibu na rafiki yao, kwamba wapinzani hawana mahali pa kutekeleza mawazo yao, hivyo kelele za kina Sabaya na wale "wananchi"' wa Hai hazina maana, wasimsumbue Mbowe.

Hoja namba tatu Slaa kaongea kisiasa; anayajua fika mazingira ya siasa Tanzania, hasa siasa za vyama pinzani, tamko la Rais, ambae ndie M/kiti wa CCM linachukuliwa kama sheria, linatekelezwa na vyombo vya dola. Juzi Bashiru katoka kujisifu kuhusu matumizi ya dola kui-favour CCM, sijui hakusikia hilo, tunamuona Bashiru akizunguka nchi nzima kufanya shughuli za siasa, wakati upinzani hata kufanya mikutano kwenye majimbo yao imekuwa tabu (Sugu), ni Mbatia pekee alieenda Mbeya hivi karibuni tena baada ya kutoka ikulu kwa mazungumzo na Rais.

Mwisho, Dr. Slaa anatoa mfano wa Sweden kwamba watu wakitaka kuandamana wanatakiwa kutoa details zao, atuambie hapa Tanzania wapi waandamanaji walitakiwa kupeleka details zao wakagoma kuzipeleka? Mazingira ya Sweden na hapa kwetu ni tofauti, hilo analijua, anajitoa akili makusudi.

Ile kauli ya "nitawachapa mpaka shangazi zao" aliwahi kuisikia au hakuisikia?
hope alikuwa busy ubalozini!.

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu kimsingi kwa sasa hivi maoni ya Dr. Slaa Ni ya nongwa dhidi ya cdm. Namfananisha kabisa na nongwa aliyo nayo Waitara dhidi ya cdm. Katika maongezi yake yote haonyeshi kama ni mtu huru bali anatoa maoni ya kuponya hisia zake, na kutaka kuwakandamiza wote anaoona walimuumiza moyo wake.
 
Mtu makini anayezungumza mapungufu ya upinzani tu, huku akifumbia macho ya ccm. Kimsingi anatumiwa akidhani ataweza kuvuta na kubadilisha mitazamo ya wapinzani.
Kwani vibaya kueleza mapungufu ya upinzani tu? Mbona kuna watu wanaeleza mapungufu ya ccm tu kana kwamba upinzani hakuna mapungufu. Ccm inajulikana ilivyo hivyo sasa huu upinzani ambao tunautegemea kuleta mabadiliko ndio wa kuonesha mapungufu ili kujiweka sawa kukabiliana na ccm.
 
Kwani vibaya kueleza mapungufu ya upinzani tu? Mbona kuna watu wanaeleza mapungufu ya ccm tu kana kwamba upinzani hakuna mapungufu. Ccm inajulikana ilivyo hivyo sasa huu upinzani ambao tunautegemea kuleta mabadiliko ndio wa kuonesha mapungufu ili kujiweka sawa kukabiliana na ccm.

Yeye kasimama kama mtu huru. Hao wanaoonyesha mapungufu tu ya ccm au upinzani tayari wanakuwa na upande na sio huru kama yeye.
 
CHADEMA hawatakuja tena kupata Secretary General aliye Smart Upstairs, Strategist, Daring na very Brave Politically kama huyu Dkt. Wilborad Slaa. Uwezo wake huu mkubwa ndiyo uliifanya CCM ikose Usingizi 24/7 na sishangai baada ya Yeye kuachana na CHADEMA ndipo nao ( CCM ) wakapumua huku wengine wakimshukuru Mwenyezi Mungu.

Kama ambavyo pengo la nyerere halizibiki ni vita tu kila uchwao
 
I really love Dr. Slaa..
Those days he made me feel proud of CDM.
Dr. aliteka moyo wangu sana hasa kwenye umahiri wake wa kujenga hoja.
All the best my role model.

Jamaa yuko vzr kwenye kujenga hoja na kuelezea misimamo yake. Si rahisi kwa balozi tena wa nchi kama Sweden kutamka hadharani kwamba yeye si mwana CCM na hana mpango wa kujiunga nacho !!!
 
Mkuu.. Inamaana sikuile ya maandamano alikuwa akiwalazimisha watu sita tuu waingie ndani ya ubalozi kuyajadili??????



Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hapo sielewi ilikuaje ila inanekana kwenye maandalizi kulikuwa na vuguvugu kubwa siku ya tukio mwitikio ulikua mdogo. Ila Slaa aliposema mamlaka za huko Sweden zilihitaji majina ya watakaoandamana hapo naona si practical !!!
 
Dr W. Slaa kaingia TZ jana Jumanne 10/03 usiku. Leo amefanya interview kwenye kipindi cha "Kumepambazuka" cha Radio One.

Amezungumza mengi kama vile diplomasia ya uchumi nk ila kuhusu siasa hizi ni dondoo muhimu kwenye interview hiyo:

1. Alijiuzulu siasa za vyama (active party politics). Hajarudi CCM na hategemei kurudi CCM. Si lazima arudi CCM (awe mwanachama) ili alitumikie taifa lake.Yeye kule Sweden hamuwakilishi mwenyekiti wa CCM, anamuwakilisha Rais.

2. Slaa anasema kama wapinzani walishindwa kuiondoa CCM 2015 hawataweza kuiondoa tena. Chama tawala kimebeba na kutekeleza agenda iliyoipa umaarufu upinzani 2015. Anasema upinzani unajenga mawazo chama tawala kinatekeleza. Hakuna kosa kwa chama tawala kuiba mawazo. Vyama vya upinzani vinapewa ruzuku kuwa "Viwanda vya Mawazo" ambayo chama tawala kinayatumia sababu upinzani hawana mahali (platform) ya kutekeleza mawazo yao.

3. Slaa anasema hakuna waraka (decree) unaowazuia wapinzani kuendesha shughuli zao. Serikali haifanyi kazi kwa matamko. Anasema kilichotokea ni kwamba kuna matamko ya upinzani (Chadema) yalileta sura ya kuchafua utulivu (Civil Disobedience). Walisema wataandamana kila kona - mkoa hadi mkoa, kijiji hadi Kijiji, mtaa hadi mtaa. Anasema kwa tafsiri yake, sheria inayotumika kudhibiti shughuli za wapinzani ni ya kipolisi sababu ikifika mahali unakwamisha mambo hauwezi kuachwa.

Anatoa mfano ofisi yake ya ubalozi Sweden ilipokea taarifa ya "Maandamano ya Mange Kimambi." Mamlaka ya Serikali ya Sweden ilitaka maelezo ya kina (details) za waandamanaji ikiwemo majina yao. Mamlaka hiyo ilielekeza idadi yao, sehemu ya kusimama na masharti mengine kama kutotumia vipaza sauti, nk. Anasema hii ni kuonyesha hata kwenye nchi kama Sweden, masharti yapo ili kuepuka kusumbua wananchi. Kati ya wale 100 walioruhusiwa kuandamana ni 6 tu walijitokeza.

Slaa anasema aliwaasa Chadema wajirekebishe kuhusu hili ila wameshindwa. Anasema ukombozi haupatikani kwa "Red Brigade" kuwa barabarani.

Anawaasa wanaotaka kujua Chadema ilipoanza kukosea wasome kitabu chake cha "Nyuma ya Pazia"
shit talkin about
 
Dr. Slaa alipoondoka Chadema naye alikuwa na deni na nyumba yake kule mbweni almanusura ipigwe mnada sema tu CCM waliingilia kati na kumlipia.
 
Back
Top Bottom