Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi kuendeleza programu ya "Tutunzane" ili kukomesha migogoro ya ardhi kati ya wafugaji na wakulima, endapo atachaguliwa kuwa Rais kwa awamu nyingine.
Akizungumza na wananchi wa Kilosa, mkoani Morogoro, katika kampeni zake, Dkt. Samia amesema kuwa programu hiyo imekuwa na matokeo chanya katika Wilaya ya Mvomero, mkoani Morogoro, ambapo sasa wakulima na wafugaji wanaishi pamoja kwa amani na upendo. Ameahidi kuipanua na kuitekeleza katika Wilaya ya Kilosa endapo atapewa ridhaa ya kuongoza kwa awamu ya pili.
Aidha, Dkt. Samia ameahidi kuboresha huduma za elimu na afya kwa kuongeza shule na vituo vya afya, pamoja na kufufua Bwawa la Idete wilayani humo ili liweze kutumika katika shughuli za kilimo na kutatua changamoto za maji.
Akizungumza na wananchi wa Kilosa, mkoani Morogoro, katika kampeni zake, Dkt. Samia amesema kuwa programu hiyo imekuwa na matokeo chanya katika Wilaya ya Mvomero, mkoani Morogoro, ambapo sasa wakulima na wafugaji wanaishi pamoja kwa amani na upendo. Ameahidi kuipanua na kuitekeleza katika Wilaya ya Kilosa endapo atapewa ridhaa ya kuongoza kwa awamu ya pili.
Aidha, Dkt. Samia ameahidi kuboresha huduma za elimu na afya kwa kuongeza shule na vituo vya afya, pamoja na kufufua Bwawa la Idete wilayani humo ili liweze kutumika katika shughuli za kilimo na kutatua changamoto za maji.