Dkt. Philip Mpango: Tumkumbuke Mungu pale tunapoteswa isivyo haki

Dkt. Philip Mpango: Tumkumbuke Mungu pale tunapoteswa isivyo haki

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
IMG_4619.jpeg
"Napenda niwahakikishie watanzania na wapenda amani na usalama kuwa tayari serikali kupitia Wizara ya Mambo ya ndani imeviagiza vyombo vya dola kuwatafuta, kuwakamata na kuwachukulia hatua kali za kisheria waliohusika na tukio hili na wale wote watakaothibitika kujihusisha na matukio kama haya hapa nchini ambayo hayakubaliki kabisa mahali popote.

Nawaomba sana Mahashamu Maaskofu na wote walioumizwa na tukio hili baya (kushambuliwa kwa Padri Charles Kitima, Katibu Mkuu Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania) kujikabidhi kwa Mungu pale tunapoumizwa na udhalimu kama tunavyosoma katika Waraka wa kwanza wa Petro, sura ya pili aya ya kumi na tisa ambayo inasema "maana huu ndiyo wema hasa, mtu akivumilia huzuni kwa kumkumbuka Mungu pale ateswapo isipo haki"

Aidha nawasihi sana watanzania wote tuendelee kupendana na kusimama pamoja kulaani matendo haya mabaya yasiyoakisi Tanzania yetu inayosifika kama kisiwa cha Amani."-Makamu wa Rais Dkt. Philip Isdor Mpango akizungumza kwenye Sherehe za uzinduzi wa Jimbo Jipya la Katoliki Bagamoyo leo Mei 04, 2025.
 
Wote wale waliohusika na tukio hilo wasakwe, wakamatwe na wafikishwe mahakamani
 
Hayo maneno aliyotamka yalitakiwa yaambatane na uamuzi wa kukaa kando kwenye hicho cheo alicho nacho ili aendane na maneno aliyotamka..! Huyu ni mtu ambae anadhani anaweza kumfurahisha Mungu kwa maneno na kuonyesha unyenyekevu wa kinafiki huku yeye ni sehemu ya udhalimu! Mbona tukio la Mzee kibao hatukumsikia..Fr. Kitima ana thamani zaidi mbele za Mungu kuliko Mzee Kibao? km huu sio unafiki ni nini..
 
Hayo maneno aliyotamka yalitakiwa yaambatane na uamuzi wa kukaa kando kwenye hicho cheo alicho nacho ili aendane na maneno aliyotamka..! Huyu ni mtu ambae anadhani anaweza kumfurahisha Mungu kwa maneno na kuonyesha unyenyekevu wa kinafiki huku yeye ni sehemu ya udhalimu! Mbona tukio la Mzee kibao hatukumsikia..Fr. Kitima ana thamani zaidi mbele za Mungu kuliko Mzee Kibao? km huu sio unafiki ni nini..
Ficha ujingawako kidogo, amesema "matukio" Sasa kama huna akili ndio unaweza kuweka justification zako kulingana na uelewa wako.

Mzee ameongelea matukio kwa ujumlawake, kama hujamuelewa stop crying, uliza ueleweshwe.
 
View attachment 3324455"Napenda niwahakikishie watanzania na wapenda amani na usalama kuwa tayari serikali kupitia Wizara ya Mambo ya ndani imeviagiza vyombo vya dola kuwatafuta, kuwakamata na kuwachukulia hatua kali za kisheria waliohusika na tukio hili na wale wote watakaothibitika kujihusisha na matukio kama haya hapa nchini ambayo hayakubaliki kabisa mahali popote.

Nawaomba sana Mahashamu Maaskofu na wote walioumizwa na tukio hili baya (kushambuliwa kwa Padri Charles Kitima, Katibu Mkuu Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania) kujikabidhi kwa Mungu pale tunapoumizwa na udhalimu kama tunavyosoma katika Waraka wa kwanza wa Petro, sura ya pili aya ya kumi na tisa ambayo inasema "maana huu ndiyo wema hasa, mtu akivumilia huzuni kwa kumkumbuka Mungu pale ateswapo isipo haki"

Aidha nawasihi sana watanzania wote tuendelee kupendana na kusimama pamoja kulaani matendo haya mabaya yasiyoakisi Tanzania yetu inayosifika kama kisiwa cha Amani."-Makamu wa Rais Dkt. Philip Isdor Mpango akizungumza kwenye Sherehe za uzinduzi wa Jimbo Jipya la Katoliki Bagamoyo leo Mei 04, 2025.
Nasikitika sana, lakini Makamu wa Rais ni kama analaza akili za watu. Ulaghai wa lugha kama hizi hizi ndio umetufikisha hapa tulipo sasa. CCM, taratibu, ndani kwa ndani ndio wametumika na kulegezwa kwa lugha za aina hii, angalia sasa tulipofikia na ulaghai huo..

"... kumkumbuka Mungu pale ateswapo ..." bila ya kuwa na akili ya kujikinga na mateso, hata Mungu hawezi kukubaliana na hilo.

Simlaumu Philipo kwa ujumbe; lakini ujumbe hauna maana katika nyakati za namna hii. Hebu atueleze huyo Bosi wake kasema nini? Haoni ulaghai unakoanzia?
 
Mpango anajua fika hakuna HAKI katika serikali inayoongozwa na ccm.......kwa amani siyo rahisi
 
View attachment 3324455"Napenda niwahakikishie watanzania na wapenda amani na usalama kuwa tayari serikali kupitia Wizara ya Mambo ya ndani imeviagiza vyombo vya dola kuwatafuta, kuwakamata na kuwachukulia hatua kali za kisheria waliohusika na tukio hili na wale wote watakaothibitika kujihusisha na matukio kama haya hapa nchini ambayo hayakubaliki kabisa mahali popote.

Nawaomba sana Mahashamu Maaskofu na wote walioumizwa na tukio hili baya (kushambuliwa kwa Padri Charles Kitima, Katibu Mkuu Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania) kujikabidhi kwa Mungu pale tunapoumizwa na udhalimu kama tunavyosoma katika Waraka wa kwanza wa Petro, sura ya pili aya ya kumi na tisa ambayo inasema "maana huu ndiyo wema hasa, mtu akivumilia huzuni kwa kumkumbuka Mungu pale ateswapo isipo haki"

Aidha nawasihi sana watanzania wote tuendelee kupendana na kusimama pamoja kulaani matendo haya mabaya yasiyoakisi Tanzania yetu inayosifika kama kisiwa cha Amani."-Makamu wa Rais Dkt. Philip Isdor Mpango akizungumza kwenye Sherehe za uzinduzi wa Jimbo Jipya la Katoliki Bagamoyo leo Mei 04, 2025.
Huyu si aliomba kujiuzuru, imekuwaje tena
 
Boss wake alishasema ni drama, yeye ni nani anapingana na Boss wake? Wasilete utani kwenye maisha ya watu.
 
Ficha ujingawako kidogo, amesema "matukio" Sasa kama huna akili ndio unaweza kuweka justification zako kulingana na uelewa wako.

Mzee ameongelea matukio kwa ujumlawake, kama hujamuelewa stop crying, uliza ueleweshwe.
..who cried you fool, hayo matukio ameyafahamu leo?
 
View attachment 3324455"Napenda niwahakikishie watanzania na wapenda amani na usalama kuwa tayari serikali kupitia Wizara ya Mambo ya ndani imeviagiza vyombo vya dola kuwatafuta, kuwakamata na kuwachukulia hatua kali za kisheria waliohusika na tukio hili na wale wote watakaothibitika kujihusisha na matukio kama haya hapa nchini ambayo hayakubaliki kabisa mahali popote.

Nawaomba sana Mahashamu Maaskofu na wote walioumizwa na tukio hili baya (kushambuliwa kwa Padri Charles Kitima, Katibu Mkuu Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania) kujikabidhi kwa Mungu pale tunapoumizwa na udhalimu kama tunavyosoma katika Waraka wa kwanza wa Petro, sura ya pili aya ya kumi na tisa ambayo inasema "maana huu ndiyo wema hasa, mtu akivumilia huzuni kwa kumkumbuka Mungu pale ateswapo isipo haki"

Aidha nawasihi sana watanzania wote tuendelee kupendana na kusimama pamoja kulaani matendo haya mabaya yasiyoakisi Tanzania yetu inayosifika kama kisiwa cha Amani."-Makamu wa Rais Dkt. Philip Isdor Mpango akizungumza kwenye Sherehe za uzinduzi wa Jimbo Jipya la Katoliki Bagamoyo leo Mei 04, 2025.
Hakuna aliyewahi kufanikiwa kuwasaka na kuwakamata majambazi wa Serikali.
 
Back
Top Bottom