Dkt. Mwigulu: Bado tupo Uchumi wa Kati

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,817
4,566

1686837810715.png

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Bungeni Dodoma amewasilisha Bungeni taarifa ya Hali ya Uchumi wa Kitaifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa wa Mwaka 2023/2024 ambapo moja ya mambo aliyoyasema ni kwamba Tanzania bado imeendelea kuwa Nchi ya uchumi wa kati ngazi ya chini.

“Kutokana na hatua madhubuti zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali thamani ya pato ghafi la Taifa linatarajiwa kufikia dola za Marekani bilioni 85.42 mwaka 2023/24, Mwaka 2022, pato ghafi la Taifa (kwa bei za mwaka husika) lilikuwa shilingi trilioni 170.3 (sawa na Dola za Marekeni bilioni 77.6) ikilinganishwa na shilingi trilioni 156.4 mwaka 2021 (sawa na Dola za Marekani billioni 69.94)”

“Aidha, kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, idadi ya Watu Tanzania Bara ilikuwa 59,851,347 ikilinganishwa na makadirio ya idadi ya Watu 57,724,380 mwaka 2021, hivyo Pato la Taifa kwa Mtu (GDP per capital) kwa mwaka 2022 lilikuwa shilingi 2,844,641 ikilinganishwa na shilingi 2,708,999 mwaka 2021, sawa na ongezeko la asilimia 5.0. Kiasi hicho ni sawa na dola za Marekani 1,229.1 mwaka 2022 kwa mtu kwa mwaka ikilinganishwa na dola za Marekani 1,173.3 mwaka 2021, hali hii inaendelea kuifanya Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati ngazi ya chini”
 
Back
Top Bottom