Waziri Dkt. Mwigulu atangaza bungeni kukopa Trilioni 6

Rege

Senior Member
Jul 9, 2022
112
140
Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amesema kuwa Serikali inatarajia kukusanya na kutumia jumla ya shilingi trilioni 47.424 katika mwaka 2024/2025.

Dkt. Nchemba amesema hayo Bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha Mapendekezo ya Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2024/25.

Amesema kuwa makusanyo hayo yatatokana na vyanzo mbalimbali yakiwemo mapato ya ndani, michango kutoka kwa washirika wa maendeleo na mikopo.

"Mapato ya ndani yanakadiriwa kuwa shilingi trilioni 34.436 sawa na asilimia 72.6 ya bajeti yote, washirika wa maendeleo wanatarajiwa kuchangia shilingi trilioni 4.291 sawa na asilimia 9.0 ya bajeti, serikali inatarajia kukopa shilingi trilioni 6.141 kutoka soko la ndani na shilingi trilioni 2.555 kutoka soko la nje," amesema Waziri Dkt. Nchemba.

Dkt. Nchemba amesema kuwa maoteo ya bajeti ya serikali ya mwaka 2024/25 yamezingatia mwenendo wa ukusanyaji mapato, matarajio ya ukuaji wa uchumi, hali ya uchumi wa dunia pamoja na mikakati ambayo Serikali inaendelea kuchukua katika kuongeza mapato ya ndani.


Untitled.jpg
 
Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amesema kuwa Serikali inatarajia kukusanya na kutumia jumla ya shilingi trilioni 47.424 katika mwaka 2024/2025.

Dkt. Nchemba amesema hayo Bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha Mapendekezo ya Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2024/25.

Amesema kuwa makusanyo hayo yatatokana na vyanzo mbalimbali yakiwemo mapato ya ndani, michango kutoka kwa washirika wa maendeleo na mikopo.

"Mapato ya ndani yanakadiriwa kuwa shilingi trilioni 34.436 sawa na asilimia 72.6 ya bajeti yote, washirika wa maendeleo wanatarajiwa kuchangia shilingi trilioni 4.291 sawa na asilimia 9.0 ya bajeti, serikali inatarajia kukopa shilingi trilioni 6.141 kutoka soko la ndani na shilingi trilioni 2.555 kutoka soko la nje," amesema Waziri Dkt. Nchemba.

Dkt. Nchemba amesema kuwa maoteo ya bajeti ya serikali ya mwaka 2024/25 yamezingatia mwenendo wa ukusanyaji mapato, matarajio ya ukuaji wa uchumi, hali ya uchumi wa dunia pamoja na mikakati ambayo Serikali inaendelea kuchukua katika kuongeza mapato ya ndani.


View attachment 2806720
Ni dalili nzuri hatutakopa saanaa trin 6 sio nyingi kwa budget ya 42 trin.

Ingawa natamani serikali ije na budget na mpango wa uboreshwaji wa nyumba za makazi mfano mazese sijui tandale na ze like pajengwe kisasa wananchi wapangishwe kwa gharama nafuu kwa sehemu itasaidia kuifanya inchi yetu kuwa na muonekano mzuri.. na kutoonekana ni kama kijiji kikubwaaa hivi.
 
tangu hizi bajeti zianze kusomagwa kila mwaka huwa sioni kitu kinachoonekana kwa kila mtanzania kwamba kimekuwa achieved, sana sana wanakusanya hela ya kutumia wao.

Kwa mfano tatizo la umeme sasa ni sugu aka donga ndugu, miaka 30 na ushee tangu neno mgawo lianze kutumika rasmi, hili tatizo kwa sasa lishakuwa jambo la kawaida kiasi kwamba kiongozi haogopi kulisemea - yaani badala ya mgawo sasa hivi CCM wamekuja na kaulimbiu yao kwamba ni "upungufu wa umeme"

Kazi tunayo watz.
 
Baada ya mwaka CAG atakuja na taarifa zenye ufisadi wa kutisha kama kawaida na waliokwapua watatetewa na viongozi pamoja na wabunge na hawata chukuliwa hatua yoyote kama kawaida, na mahitaji ya msingi kama umeme bado hayatopata ufumbuzi na tutaambiwa ilitumika pesa nyingi kwa ajili ya marekebisho, bongo bahati mbaya kweli 🤦🤦🤦
 
Back
Top Bottom