Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,499
Aliyekuwa mtia nia wa ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika jimbo la Mvomero mkoani Morogoro, Dkt. Albanie Marcossy, amejitokeza na kumtaka hadharani mwanachama wa chama hicho, Humphrey Polepole, kupuuzwa na wanachama wengine kwa madai kuwa kauli zake za hivi karibuni zimejaa "vihoja vya kuungaunga" vinavyolenga kuidhoofisha demokrasia nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari siku ya Ijumaa kufuatia kauli mbalimbali ambazo zimekuwa zikitolewa na Polepole Dkt. Marcossy amesema: “Huenda kuna visa na visasi nyuma yake, kuna vitu alivitarajia vifanyike havijafanyika, na kwasababu hiyo anadhani anaweza kutumia umma kutingisha au kuudhoofisha mchakato wa kidemokrasia wa kufikia uchaguzi na kufanya uchaguzi. Huenda kuna walengwa nyuma yake, na ndiyo maana ameanza kuropoka sasa na kutaja baadhi ya majina ya watu”.
Kwa mujibu wa Marcossy, kauli za Polepole zinafanana na zile zilizokuwa zikitolewa na baadhi ya wanaharakati na vyama vya upinzani vilivyopinga kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu mwaka huu. Amesema kauli hizo ni jaribio la kumchafua Rais na kutaka CCM igeuke dhidi ya utaratibu wake wa uchaguzi.
Amesisitiza kuwa uchaguzi ni msingi wa demokrasia na kwamba Polepole anapaswa kupuuzwa kwa kuwa hana tena mchango chanya kwa chama.
Polepole, ambaye alijiuzulu hivi karibuni kutoka nafasi ya ubalozi nchini Cuba, alitoa waraka mzito akilalamikia kile alichokiita “kukosekana kwa haki ndani ya CCM” na “ukiukwaji wa desturi za chama”, na tangu wakati huo amekuwa akijitokeza kuzungumzia mambo mbalimbali yanayoihusu CCM.
Wakati baadhi ya wapinzani wakimpongeza kwa ujasiri, ndani ya CCM anatajwa kuzidi kupoteza mvuto na kupewa sifa ya kuwa msaliti wa itikadi.
Video: Jambo TV
Akizungumza na waandishi wa habari siku ya Ijumaa kufuatia kauli mbalimbali ambazo zimekuwa zikitolewa na Polepole Dkt. Marcossy amesema: “Huenda kuna visa na visasi nyuma yake, kuna vitu alivitarajia vifanyike havijafanyika, na kwasababu hiyo anadhani anaweza kutumia umma kutingisha au kuudhoofisha mchakato wa kidemokrasia wa kufikia uchaguzi na kufanya uchaguzi. Huenda kuna walengwa nyuma yake, na ndiyo maana ameanza kuropoka sasa na kutaja baadhi ya majina ya watu”.
Kwa mujibu wa Marcossy, kauli za Polepole zinafanana na zile zilizokuwa zikitolewa na baadhi ya wanaharakati na vyama vya upinzani vilivyopinga kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu mwaka huu. Amesema kauli hizo ni jaribio la kumchafua Rais na kutaka CCM igeuke dhidi ya utaratibu wake wa uchaguzi.
Amesisitiza kuwa uchaguzi ni msingi wa demokrasia na kwamba Polepole anapaswa kupuuzwa kwa kuwa hana tena mchango chanya kwa chama.
Polepole, ambaye alijiuzulu hivi karibuni kutoka nafasi ya ubalozi nchini Cuba, alitoa waraka mzito akilalamikia kile alichokiita “kukosekana kwa haki ndani ya CCM” na “ukiukwaji wa desturi za chama”, na tangu wakati huo amekuwa akijitokeza kuzungumzia mambo mbalimbali yanayoihusu CCM.
Wakati baadhi ya wapinzani wakimpongeza kwa ujasiri, ndani ya CCM anatajwa kuzidi kupoteza mvuto na kupewa sifa ya kuwa msaliti wa itikadi.