baada ya chadema kushindwa kuvuna wanachama wa ccm wilayani sengerema,katibu mkuu wa chadema dk wilbroad slaa amewatimua viongozi 33 na kuvunja kamati ya utendaji ya chama hicho wilayani sengerema.
viongozi hao walitimuliwa usiku wa manane kwenye kikao cha ndani na hawakutakiwa kugombea tena uongozi ndani ya chadema katika uchaguzi wa kuziba nafasi zao na badala yake aliyejiunga na chama hicho ni aliyekuwa diwani wa kata ya ibisabageni hamisi tabasamu
viongozi hao wamefukuzwa kwa kushindwa kuwashawishi wananchi wengi wakiwemo wanaccm kujitokeza katika mkutano wa dk slaa uliofanyika jumamosi iliyopita mjini humo.
miongoni mwa waliotimuliwa yumo said shabani ambaye ni mwenyekiti wa jimbo la sengerema,rafiki rufunga ambaye ni katibu na manyama mayeye ambaye ni katibu mwenezi.
katibu wa chadema mkoa wa mwanza wilson mushumbushi aliyedaiwa kuhudhuria kikao hicho alipotakiwa kuzungumzi sakata hilo alidai liko juu ya uwezo wake na kuthibitisha kutimuliwa kwa viongozi hao wa wilaya.
CHANZO: Gazeti la Uhuru
viongozi hao walitimuliwa usiku wa manane kwenye kikao cha ndani na hawakutakiwa kugombea tena uongozi ndani ya chadema katika uchaguzi wa kuziba nafasi zao na badala yake aliyejiunga na chama hicho ni aliyekuwa diwani wa kata ya ibisabageni hamisi tabasamu
viongozi hao wamefukuzwa kwa kushindwa kuwashawishi wananchi wengi wakiwemo wanaccm kujitokeza katika mkutano wa dk slaa uliofanyika jumamosi iliyopita mjini humo.
miongoni mwa waliotimuliwa yumo said shabani ambaye ni mwenyekiti wa jimbo la sengerema,rafiki rufunga ambaye ni katibu na manyama mayeye ambaye ni katibu mwenezi.
katibu wa chadema mkoa wa mwanza wilson mushumbushi aliyedaiwa kuhudhuria kikao hicho alipotakiwa kuzungumzi sakata hilo alidai liko juu ya uwezo wake na kuthibitisha kutimuliwa kwa viongozi hao wa wilaya.
CHANZO: Gazeti la Uhuru