Dk. Slaa akamata nyaraka ya siri ya serikali

Nchi hii tunacheza michezo ya hatari kweli. Hainiingii akilini kama tunaweza kuthubutu kushabikia kitendo cha mtu kuiba nyaraka ya serikali wenyewe tunasema 'akamata'. Kuiba nyaraka ya serikali ni jambo la hatari kwa uhai wa taifa lolote haijalishupi umefanywa na nani? Leo Dr. Slaa anaiba nyaraka ya Serikali na tunamshangilia.

Mbinu hii itatumika dhidi ya Serikali ya CHADEMA siku itakapojaaliwa kuingia madarakani. Mchezo huu ukiendelea, hakuna Serikali itakayotawala. Kitendo hiki kinadhoofisha Serikali na sio kitendo ch kushabikia hata kidogo, na ndio maana kuna sheria ya bunge dhidi ya kitendo hicho. Bahati nzuri Serikali yenyewe in huruma huruma hivi.

Lakini la pili ni kuwa, tunataka sasa kuhalalisha ushiriki wa watumishi wa umma kwenye siasa. Hii ni hatari nyingine. Kitendo cha kunajisi utumishi wa umma na siasa, aidha kusaidia Chama Tawala au Chama cha Upinzani ni kitendo cha hatari na kukemea. Watumishi wa umma wakifanya kazi kisiasa hakuna maendeleo yatakayopatikana na hatari ya hujuma aidha dhidi ya wapinzani au serikali inaweza kuwa kitu cha kawaida.

Sioni tatizo lolote kuhusu Waraka huo wa kukataza watumishi wa umma kutoshiriki shughuli za siasa. Waraka haukatazi mtumishi wa umma kuwa mwanachama, kinachokatazwa ni kuwa kiongozi wa chama au kufanya shughuli za chama cha siasa mahala pa kazi. Waraka huu unawasaidia pia CHADEMA kuliko tunavyotaka kuaminishwa.

Watumishi wa Umma wakiamua kutumika dhidi ya CHADEMA ustawi wa Chama hicho utakuwa mashakani. Inawezekana walioko kwenye utumishi wa umma wakawa CCM wengi kuliko CHADEMA kama ambavyo inawezekana pia wakawa CHADEMA wengi kuliko CCM. Lengo la Waraka huu ni kulinda maslahi ya umma wote na haki yao ya kupata haki na huduma kutoka katika utumishi wa umma bila kujali itikadi.

Pengine nielezwe humu ni nchi gani na wapi ambapo utumishi wa umma wanaruhusiwa kujihusisha na siasa za vyama mahala na wakati wa kazi? Kwa nini sisi tuwe wa kwanza?

Tusikubali kutumiwa kuhalalisha mbinu haramu kwa sababu tu ya kutaka kufikia maslahi yetu ya kisiasa. CHADEMA wakumbuke, mbinu hizo hizo zitatumika dhidi yao wakiwa madarakani.
Acha ubabaishaji bwana, hayo ulikuwa wapi kuyasema siku zote ambazo ccm ilikuwa na wafuasi serikalini? umesahau kuwa ni ccm hii hii imekuwa ikifukuza kazi watu wenye mwelekeo wa kuwa wapinzani na kuwaacha watu wengi tu wakijitangaza kuwa wanaccm na huku wanafanya kazi. Unajifanya huelewi kuwa waraka huo unawalenga watu gani? Kama una uchungu na nchi hii ipige vita sana ili iondoke madarakani ikapate muda wa kujitathmini upya lakini sio kutaka kuhalalisha ufirauni wa ccm kwa kichaka cha nyaraka za uma. Halafu inaonesha hujui kuwa ccm ilishakufa umebaki mwangwi ndo maana unasema eti serikali ina huruma huruma, tangu lini ccm wakawa na huruma mafisadi wakubwa wametufanya sie tusipige hatua za maendeleo mpaka vinchi uchwara kama kenya vinatushinda. Waambie wamshike na kumfunga Slaa kama wana ubavu. wanashindwa hata kumkalisha mahabusu Lema watamweza Slaa!
 
Yaani hapo umenena ndugu, kwanza yeye mwenyewe anajuta kuacha kugombea Ubunge, kwa sababu anazikosa posho. Hujachelewa mzee Slaa gombea tu 2015 ubunge maana uraisi huupati ng'oooo. Labda Zitto Kabwe sio wewe ambaye umejaa Ukatoliki na Uchaga na Ukanda. Tunataka aliyeshiba U-Tanzania.
Aliyejaa ukatoliki hawezi kuwa rais, ila aliyejaa uislam ndo anatakiwa kuwa rais.
 
Sasa kaka mbona kauli yako inatujumuisha wote.,au wewe unatuona wote hatunazo,na KAMA hujazaliwa TZ humu unafanya nini..!!.
au unisahihishe labda ulikuwa na maana kwamba hujazaliwa Tanzania upande wa wala ubwabwa..??.
Hujamwelewa Patali. kasome vizuri post aliyokuwa anaijibu.
 
kama hizi ndio zinaitwa ndio nyaraka za siri za serikali basi hiyo si serikali ya watu, na sio kosa kuwa nazo kwa njia yeyote ile. siri za serikali ni kwa maslahi ya umma, kama zitakuwa ni kinyume na maslahi yao, hazina uhalali wa kuitwa siri au nyaraka za serikali
 
baba uovu huo wa kutumia itikadi za chama kama kigezo cha kupata kazi kupanda cheo nk umeanza kuvisikia leo? Mzee acha kujificha nyuma ya shina la mchicha jambo hili lipo tangu enzi za chama kimoja any way naamini waraka huo ungetokea chadema ungeupinga vibaya mno pia inaonyesha wazi kuwa hukusoma vizuri maelezo ya mleta mada rudia tena kusoma majibu mengi ya maswali yako yapo huko mf kuwataka waorodheshe idadi ya watumishi wanaounga mkono upinzani nafasi zao kazini yaani vyeo nk na si kufanya siasa maeneo ya kazi kama unavyotaka kututafsiria

sheba umelaniwa sina lugha ya kukubembeleza dr. Yuko makini na wewe na kikundi chako mmezaliwa kutawaliwa tu ndiyo maana nchi imewashinda tunajua ujinga wenu. Watu tunaishi kama tuko jehanum halafu wewe unashabikia upumbavu wa ccm eti kaiba nyara za serikali kwa taarifa yako hao waliokabidhiwa kuzitunza ndiyo waliompa baada ya kukinai ushenzi wa ccm. Kama huna cha kuandika kaa pembeni na umbumbumbu wako umesababisha nitumie lugha chafu kwa sababu huna akili watanzania tunateseka ndani ya nchi yetu wengine wanaishi kama wako peponi na kudhibiti maisha ya watu milioni arobaini na wewe kwa upumbavu wako unasema ccm iko sahihi jiulize kidogo tu dc ni mjumbe wa kamati ya chama kwa nini? Pumbavu
 
aliyejaa ukatoliki hawezi kuwa rais, ila aliyejaa uislam ndo anatakiwa kuwa rais.

umelaniwa wewe hatuangalii dini ya mtu tunaangalia nani anatetea watanzania sasa kwa sababu umebipu nataka ujuwe kuwa nyie mlioko kwenye hiyo dini unayoiona wewe ndiyo sahihi mumezaliwa kutawaliwa na utawala hamuuwezi duniani kote kama hujui kamuulize aliyekupa hiyo kitu unayoita dini.
 
sheba umelaniwa sina lugha ya kukubembeleza dr. Yuko makini na wewe na kikundi chako mmezaliwa kutawaliwa tu ndiyo maana nchi imewashinda tunajua ujinga wenu. Watu tunaishi kama tuko jehanum halafu wewe unashabikia upumbavu wa ccm eti kaiba nyara za serikali kwa taarifa yako hao waliokabidhiwa kuzitunza ndiyo waliompa baada ya kukinai ushenzi wa ccm. Kama huna cha kuandika kaa pembeni na umbumbumbu wako umesababisha nitumie lugha chafu kwa sababu huna akili watanzania tunateseka ndani ya nchi yetu wengine wanaishi kama wako peponi na kudhibiti maisha ya watu milioni arobaini na wewe kwa upumbavu wako unasema ccm iko sahihi jiulize kidogo tu dc ni mjumbe wa kamati ya chama kwa nini? Pumbavu

"Responding to a disagreement by personal or national abuse does not help either. It does not influence our opponents, or the onlookers, in our favour. For a disagreement is either the result of a genuine conflict of interest, or it is the result of misunderstanding, shouting will make it worse, while careful argument can end the disagreement to the satisfaction of both sides......if you are forced to be really nasty, don't shout;use ridicule instead. Ridicule is argument; and it requires knowledge!" Mwalimu J.K. Nyerere, Argue Dont Shout, 1969
 
Hongera Slaa, kwa kukamata nyaraka za siri...

Vipi zile karatasi za kupigia kura ulizozikamata Tunduma zilikuwa kontena ngapi?

Dalili ya kuparanganyika kwa akili za binadamu ni pale unapoona unayeongea naye hawezi kuelewa kinachoongelwa wala kutofautisha mada. Unaongelea kilimo, yeye anachangia hoja ya utamaduni, unaongelea miundombinu ya barabara, yeye anaongelea mapishi. Kumjua punguuani, kama hatembei uchi, ni lazima umsemeshe.
 
mwongo huyo, akawadanganye hukohuko kanisani alikokuwa akitumika, mzushi huyu siwezi kumuamini hata kidogo, tangu azushe issue ya kontena la kura, mfuko wa cement kuwa 5000 na mengine mengi simwamini huyu.

mpuuzi wewe1 huna tofauti na anayeita mbinu chafu za ccm nyaraka za serikali.
 
Wewe kila dalili zinaonyesha umetumwa na CCM kuyasema hayo na inavyoonekana waliokutuma nao wamechoka kama ulivyochoka,mawazo yote yanaonekana ni ya kizamanizamani,hivi jamani nauliza chama maiti nacho bado kinaongea?,Tunakutahadhalisha uzisome alama zote za nyakati,Waliokutuma kama ni sisiemu au KUF waambie sisi tuko makini kwa kila kauli na hatua tunazo tembea,Subirini 2015 tunawapokonya tena 25% ili mubaki na 35,hamna jipya nyie mmefulia kama ...............................................
Nchi hii tunacheza michezo ya hatari kweli. Hainiingii akilini kama tunaweza kuthubutu kushabikia kitendo cha mtu kuiba nyaraka ya serikali wenyewe tunasema 'akamata'. Kuiba nyaraka ya serikali ni jambo la hatari kwa uhai wa taifa lolote haijalishupi umefanywa na nani? Leo Dr. Slaa anaiba nyaraka ya Serikali na tunamshangilia.

Mbinu hii itatumika dhidi ya Serikali ya CHADEMA siku itakapojaaliwa kuingia madarakani. Mchezo huu ukiendelea, hakuna Serikali itakayotawala. Kitendo hiki kinadhoofisha Serikali na sio kitendo ch kushabikia hata kidogo, na ndio maana kuna sheria ya bunge dhidi ya kitendo hicho. Bahati nzuri Serikali yenyewe in huruma huruma hivi.

Lakini la pili ni kuwa, tunataka sasa kuhalalisha ushiriki wa watumishi wa umma kwenye siasa. Hii ni hatari nyingine. Kitendo cha kunajisi utumishi wa umma na siasa, aidha kusaidia Chama Tawala au Chama cha Upinzani ni kitendo cha hatari na kukemea. Watumishi wa umma wakifanya kazi kisiasa hakuna maendeleo yatakayopatikana na hatari ya hujuma aidha dhidi ya wapinzani au serikali inaweza kuwa kitu cha kawaida.

Sioni tatizo lolote kuhusu Waraka huo wa kukataza watumishi wa umma kutoshiriki shughuli za siasa. Waraka haukatazi mtumishi wa umma kuwa mwanachama, kinachokatazwa ni kuwa kiongozi wa chama au kufanya shughuli za chama cha siasa mahala pa kazi. Waraka huu unawasaidia pia CHADEMA kuliko tunavyotaka kuaminishwa.

Watumishi wa Umma wakiamua kutumika dhidi ya CHADEMA ustawi wa Chama hicho utakuwa mashakani. Inawezekana walioko kwenye utumishi wa umma wakawa CCM wengi kuliko CHADEMA kama ambavyo inawezekana pia wakawa CHADEMA wengi kuliko CCM. Lengo la Waraka huu ni kulinda maslahi ya umma wote na haki yao ya kupata haki na huduma kutoka katika utumishi wa umma bila kujali itikadi.

Pengine nielezwe humu ni nchi gani na wapi ambapo utumishi wa umma wanaruhusiwa kujihusisha na siasa za vyama mahala na wakati wa kazi? Kwa nini sisi tuwe wa kwanza?

Tusikubali kutumiwa kuhalalisha mbinu haramu kwa sababu tu ya kutaka kufikia maslahi yetu ya kisiasa. CHADEMA wakumbuke, mbinu hizo hizo zitatumika dhidi yao wakiwa madarakani.
 
vijana umefika wakati wa kuchambua na kutafakari kwa kina kauli za huyu kasisi sipendi wala sitaki kuamini kama anaweza kucheza na akili zenu kiasi hicho kweli " common sense is not common to all!!!
 
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk.Wilbrod Slaa, ameiumbua tena serikali ya Chama cha Mapinduzi(CCM) kwa kufichua waraka maalumu wenye lengo la kudhibiti na kufuatilia kwa makini nyendo za watumishi wa serikali wanaoshabikia vyama vya upinzani.

Akihutubia juzi katika mkutano wa hadhara uliyofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Nzovwe na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa watu, Dk. Slaa alisema waraka huo kupitia Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi ) unawataka Makatibu Tawala wa Mikoa yote nchini kufuatilia na kupeleka takwimu za wafanyakazi wanaojihusisha na siasa sehemu za kazi.

Alisema ili kutimiza azma hiyo wametakiwa kuorodhesha kila mtumishi kwa majina kamili, kazi anayofanya, cheo kazini, itikadi ya siasa na cheo alichonacho ndani ya chama husika lengo likiwa ni kuwapata watumishi wanachama wa vyama vya siasa pinzani nchini.

Dk. Slaa ambaye alikuwa akishangiliwa kila wakati na umati mkubwa watu, alisema hatua hiyo ya serikali ni ya hatari kubwa, na akaitaka kusitisha na kuacha kuwatisha wananchi walio huru ndani ya nchi yao.

Alisema kinachojaribu kufanywa na serikali ni kutaka kudhoofisha nguvu ya upinzani, jambo litakalosababisha kuzuka kwa vurugu.

“Mchezo huu si mzuri na hauwezi kuvumilika hata kidogo kwa kuwa nchi hii ni yetu sote na yenye kutawaliwa kwa mfumo wa vyama vingi na hawa watumishi wanaruhusiwa kuendesha siasa wakati wa nje ya kazi, kwa nini serikali iamue kutoa waraka huu?” alihoji.

Dk. Slaa alisema ndani ya waraka huo kuna maelekezo kuwa Katibu Tawala yeyote atakayeshindwa kutekeleza majukumu hayo aliyopewa na wizara basi jina lake litapelekwa kwa Katibu Mkuu wa Wizara ili ashughulikiwe ipasavyo.

Alisema CHADEMA itaendelea na maandamano nchi nzima kupinga baadhi ya mambo ya kifisadi ambayo serikali inayafanya na kamwe hawataogopa kufanya hivyo hata kama watakamatwa na polisi na kupelekwa mahakamani.

Aidha Dk. Slaa katika suala zima la uundwaji wa Katiba mpya alisema Chama cha Mapinduzi kupitia kikao chake cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kilitoa waraka uliowataka viongozi wa chama hicho ngazi zote kusimamia zoezi hilo katika kuhakikisha mawazo yote yatakayotolewa na wananchi yawe kwa manufaa ya CCM.

Alisema alifikiri kuwa mchakato wa Katiba ni kwa manufaa ya Watanzania wote kumbe CCM inauchukulia kwa manufaa yake na si ya wananchi.

“Tazameni, yaani haya ni mambo ya ajabu kabisa yanayofanywa na viongozi hawa, badala ya kujadili mambo ya mustakabali wa nchi juu ya hali ngumu ya maisha kwa wananchi, wao wanapanga ni jinsi gani watatekeleza azma yao ndani ya Katiba mpya kwa maslahi ya CCM na si ya Watanzania,” alisema.

SOURCE:TANZANIA DAIMA

mambo kweli! hivi ni chama gani kitakacho pewa dhamana ya kutawala na baadaye kikakubaliana na mtumishi anayekuwa kuwa na waajiri wawili? ktk maana ya kuzuia mipango ya serikali na wakati mwingine kuuza siri za serikali(mwajiri). pili katiba si mali ya chama chochote yaani si ccm wala cdm, iweje mkakati uwe kwa maslahi ya ccm, na ile proposal ya cdm kwa rais unataka kusema ilibeba maslahi ya cdm? na iweje kuwataka wananchi hususani cdm wagomee kusikiliza na kutoa maoni yao, huoni unazuia haki ya huyu mtu kwa upande mmoja? je kama cdm mnawachukuliaje watumishi wanaoleta kwenu siri za serikali? jibu ukiamini oneday utakuwa chama tawala na ccm upinzani.
 
Redio WPFW Washington dc itafuatilia kwa karibu sana na kuwaeleza wa wananchi wa marekani kuhusu pesa zao wanazotoa za mfuko wa milenium.Kama serikali ya Tanzania kama kweli wanafanya hivyo watakua wamekwisha.Nipo kwenye hii Redio Na nitakuwa mbele mpaka capital hill ,ili kuongea ukweli ili tunyimwe pesa.
 
acha utumwa wa mawazo kaka. Kinachozungumziwa hapa ni siasa mahali pa kazi na sio siasa wakati wa kazi. Wewe ungetumia akili yako vizuri kufikiri, ungegundua ni nini ccm wanaogopa na ndio maana wanatunga sera za ajabu. Nakupa mfano wa walimu: Wana matatizo mengi na serikali imeyafumbia macho kwa muda mrefu. Kwa kuwa imani yao kwa serikali imeshuka, si ajabu ukawasikia now and then wakisema hili na lile kuhusu harakati za cdm na ukombozi wa wanyonge. Hili ndilo linaloiumiza kichwa ccm na serikali yake.
kwa kuongezea, mimi ni mwalimu na ni mwanachama wa cdm. Na ninafundisha nimemajor kwenye masomo ya lugha ila nimeamua kufundisha civics kwa kuwa nitapata wigo wa kugusia masuala ya siasa. Katika kipindi changu najitahidi kuzalisha wanachama wapya for future generation for cdm.
 
kama hizi ndio zinaitwa ndio nyaraka za siri za serikali basi hiyo si serikali ya watu, na sio kosa kuwa nazo kwa njia yeyote ile. siri za serikali ni kwa maslahi ya umma, kama zitakuwa ni kinyume na maslahi yao, hazina uhalali wa kuitwa siri au nyaraka za serikali
mkuu selikali hii si selikali ya watu, ni selikali ya NEC ndo maana hizo wanazoziita nyaraka za siri za selikali zimekaa ki ccm ccm.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom