Selous
JF-Expert Member
- Jan 13, 2008
- 1,325
- 144
Dk. Slaa abeba makombora 20
CCM nao waandaa mamluki kummaliza
na Waandishi wetu
MGOMBEA urais kupitia Chama cha Maendeleo na Demokrasia (CHADEMA), Dk. Wilbrod Slaa, ameandaa makombora yapatayo 20 yatakayotumika kukimaliza Chama Cha Mapinduzi (CCM) na mgombea wake, Rais Jakaya Kikwete, kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.
Tayari Rais Kikwete na chama chake wameanza kushtuka kuhusu makombora hayo, kwani yamefanyiwa utafiti wa kina na yatatumika kuanika uozo uliokithiri uliofanywa na Serikali ya Awamu ya Nne; na yatatumika kama silaha ya Dk. Slaa katika kuusaka urais.
Vyanzo vya habari kutoka ndani ya chama hicho kikubwa cha upinzani nchini, vimeliambia Tanzania Daima Jumatano kuwa hata hivyo Dk. Slaa hatalipua mabomu hayo hadi kampeni zitakapoanza rasmi mwishoni mwa mwezi huu.
Chanzo cha habari kilisema: Anachokifanya Dk. Slaa hivi sasa ni kujitambulisha kama mgombea, pia kuomba kudhaminiwa, hajaanza kampeni. Atakapoanza mtaona mambo mazito yenye ushahidi wa nyaraka zinazoonyesha ufisadi uliofanywa na viongozi wa serikali katika kipindi hiki cha miaka mitano.
Katika baadhi ya mikutano yake ya hadhara ya kuomba kura, Dk. Slaa mwenyewe amekuwa akiwaambia wananchi kuwa ana mambo mazito yanayohusu ufisadi wa serikali. Baadhi ya mambo hayo amekuwa akiyahoji bungeni kila alipopata nafasi, lakini hayajawahi kupatiwa majibu.
Dk. Slaa ambaye amejipatia umaarufu kutokana na kufanyia utafiti kila jambo analolizungumza, amekuwa akiwaahidi wananchi kuwa kwa vile yuko kwenye mikutano ya kuomba udhamini, ataanza kufyatua makombora hayo wakati wa kampeni.
Itakumbukwa kuwa Dk. Slaa ndiye aliyelipua bungeni bomu la ufisadi mkubwa kupitia Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA); na ndiye alitaja orodha ya mafisadi 11 wakiwamo Rais Kikwete, aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu, Daudi Ballali, Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, Mwanasheria Mkuu wa Serikali wa zamani, Andrew Chenge, waziri wa fedha wa zamani, Basil Mramba na makatibu wakuu, Patrick Rutabanzibwa na Gray Mgonja. Baadhi yao wako mahakamani; wengine tuhuma zao zinaendelea kuchunguzwa.
Walitajwa pia Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono, Rais mstaafu, Benjamin Mkapa na aliyekuwa waziri wa nishati na madini, Nazir Karamagi.
Na ingawa viongozi wakuu walianza kwa kumbeza na kuwateta mafisadi, hivi sasa nao wanajitapa kuwa wameshughulikia ufisadi.
Tangu alipotangaza kuwania urais, Dk. Slaa amewashtua viongozi wakuu na wanachama wa CCM, kiasi kwamba kwa nyakati tofauti Mwenyekiti wake, Rais Kikwete na Katibu Mkuu, Yusuph Makamba, wametoa kauli zinazoonyesha kiwewe walichonacho.
Dk. Slaa, ambaye alifanya kazi kubwa katika Bunge la Tisa, hakuwa akitajwa sana kugombea urais, lakini baada ya CHADEMA kufanikiwa kumshawishi aingie kwenye mbio za Ikulu, ameonekana kuongeza nguvu na umaarufu wa CHADEMA, chama ambacho sasa ndicho kinaonekana tishio kwa CCM.
Hata juzi Rais Kikwete aliporejea kwenye ofisi ndogo za makao makuu ya CCM baada ya kuchukua fomu ya kugombea tena urais, aliwaonya wana CCM wasidharau upinzani, bali wajiandae kufanya kampeni kali ili waweze kushinda.
Aliwaasa waachane na kauli kwamba CCM itatawala milele.
Tanzania Daima limezungumza na vigogo kadhaa wa CCM ambao wamekiri, bila kutaka majina yao yatajwe, kuwa wasipokaa vizuri Dk. Slaa anaweza kujenga wimbi la harakati zinazoweza kuifanya CCM ijikute nje ya serikali au ishinde kwa taabu.
Tayari zipo taarifa zisizothibitishwa kwamba CCM imeshaanza kujipanga kumkabili Dk. Slaa, kwa kuandaa majeshi ya kukodi na kufadhili ili yakisaidie kumshambulia kampeni zitakapoanza, kama njia ya kumpunguza makali.
Baadhi ya viongozi wa vyama vidogo vya siasa na vyombo vya habari vyenye uhusiano na CCM wametajwa kuhusika na njama hizo kwa kupewa ujira mdogo na CCM.
Miongoni mwa hoja wanazoandaa kutumia kama silaha zao ni imani ya Dk. Slaa, ili kumpambanisha na wananchi wasiofuata imani yake; na masuala binafsi kuhusu familia yake.
Hata hivyo, baadhi ya wachambuzi wameonya kuwa iwapo CCM na vyama hivyo watafanya kosa la kuingiza udini katika siasa za nchi, watakuwa wanajichimbia kaburi refu, maana matokeo ya kampeni chafu za viwango hivyo ni mabaya kwa wote, na yanaweza kugeuka silaha kwa wasio madarakani.
Wameonya pia kuwa iwapo masuala ya kifamilia yatageuzwa silaha ya kisiasa kwa wagombea, yanaweza kujitokeza masuala mazito dhidi ya walio madarakani, ambao watakuwa wamempatia Dk. Slaa kombora la nyongeza la 21.
Tayari, baadhi ya makada wa CCM na watumishi wa Ikulu wameshaanza kutumia vyombo vya habari kusambaza uvumi na propaganda dhidi ya Dk. Slaa ili kumchonganisha na wanachama na viongozi wenzake.
Katika hatua nyingine, mwasisi wa mageuzi nchini na mwanasheria maarufu, aliyejiunga na CHADEMA hivi karibuni, Mabere Marando, amesema ana mafaili ya viongozi wa kitaifa yenye sahihi zao, yakionyesha jinsi walivyohusika na kashfa mbalimbali za ufisadi serikalini.
Akihutubia mamia ya wananchi kwenye Uwanja wa Mwembetogwa, mkoani Iringa na Mbeya jana, kwa nyakati tofauti kwa ajili ya kuwaomba ridhaa ya kumdhamini mgombea urais wa chama hicho, Dk. Slaa, Marando alisema ana mafaili ambayo akiyaanika hadharani yatagusa wengi, akiwamo kiongozi mkuu ambaye hakumtaja jina.
Kuna watu wameanza chokochoko eti kwamba uamuzi wangu wa kuingia CHADEMA ni kutaka kudhoofisha vita dhidi ya ufisadi ambayo imekuwa ukiendeshwa na chama hiki, leo (jana) napenda kuwaambia bila woga wowote kwamba pale ofisini kwangu kuna mafaili ya viongozi wa serikali, tena yakiwa na sahihi ya kiongozi mkuu (hakumtaja jina), nikiyaanika haya, hawatajaribu hata kidogo kuchokoza tena, eti mtu ukianza kupata umaarufu wanasema nimeanza jamani nasema mimi sidanganyiki, alisema Marando.
Alisema kwa kipindi kirefu, amekuwa akihusishwa na taarifa kuwa yeye ni ofisa usalama, hivyo amekwenda kufanya uchunguzi CHADEMA, Marando alisema: Kweli mimi ni afisa usalama niliyesomea maeneo mengi, yakiwamo nchini Cuba, nilifaulu vizuri na kuwa tegemeo kwa taifa, hata wakati najiandaa kuondoka kwenye kazi hii, walitaka kunizuia eti kwa kisingizio kwamba maadili hayaniruhusu.
Nikiwa kule sikula kiapo cha kunizuia kuingia kwenye siasa ndiyo maana nikaamua kuingia kwenye upinzani, nimeingia CHADEMA nikiwa nimedhamiria kuandika historia nyingine kwa ajili ya kuwakomboa Watanzania, alisema Marando.
Alisema kama chokochoko hizo zitaendelea atafumua mabomu mazito ya kesi mbalimbali ambazo ziko mezani mwake, hali ambayo itasababisha kampeni za uchaguzi wa rais, wabunge na madiwani kuchimbika.
Akihutubia mkutano huo, Dk. Slaa aliwasihi wakazi wa Mkoa wa Iringa kuacha tabia ya kila uchaguzi kuipigia kura CCM, kwa kuwa imewageuza kuwa mtaji wao kila kukicha.
Nawaambia kama tulivyofanya ukombozi kwenye halmashauri nyingine, tumepeleka ukombozi mkubwa, lakini wananchi wa mkoa huu mnapaswa kubadilika kwa vile tangu mfumo wa vyama vingi umeingia nchini, hamjawahi kutoa mbunge wa upinzani, alisema Dk. Slaa.
Alisema amekamata barua zilizotumwa na CCM makao makuu kwenda kwa wakuu wa wilaya kote nchini, zikiwaagiza kukusanya wafanyabiashara wote kila mkoa kuhakikisha wanaichangia CCM fedha kwa ajili ya kampeni za Uchaguzi Mkuu.
Dk. Slaa alipowasili mkoani hapa, alipokewa kwa maandamano makubwa yaliyotikisa mji wa Iringa kutokana na kupita mitaa mbalimbali kabla ya kuingia kwenye uwanja wa mkutano.
Mara baada ya mkutano huo, Dk. Slaa akitumia ndege ya kukodi aliwasili majira ya saa 11:3 jioni kwenye Uwanja wa Ndege wa Mbeya ambako alipokewa na mamia ya wananchi, waliosababisha shughuli mbalimbali kusimama.
Mamia ya wananchi wakiwemo watu wazima, vijana na watoto, huku wakikimbia mchakamchaka kwa umbali wa zaidi ya kilomita mbili na nusu wakiimba nyimbo za mpisheni rais apite, kiboko ya mafisadi ametua Mbeya. Kadiri msafara huo ulivyosonga mbele, vijana wakiwa na mabango yaliyosomeka Dk. Slaa ulizaliwa uikomboe Tanzania, mafisadi chali, Dk. Slaa mtetezi wa wanyonge, chaguo la Watanzania, mdogo mdogo baba mpaka Ikulu. Dk. Slaa na msafara wake leo wanatarajiwa kuwasili katika mikoa ya Ruvuma, Lindi na Mtwara kwa ajili ya kuendelea kuomba ridhaa ya udhamini wa wananchi kwa ajili ya kugombea urais.
CCM,
Ole wenu mcheze na hisia za watu at this point. Mnachukua kodi zetu kwa ajili ya kutununua just for your primaries. tunajua jinsi mlizofanya na video za haya masibusi zipo na akili inayotumika inajulikana.
Kuna watu wanauchungu na hii nchi na next move kwa taarifa yenu labda mkataze mobile ofisini kwenu.
Hatutaki machafuko ila ujangili wenu tena ukiongozwa na wale wanaojifanya wanajua kuchangia while wamevaa ngozi ya kondoo wamekwisha. Haiwezekani wao kuwa na vipande viwili eti kwa kuwa mnataka kuhalalisha vitumike ndo mtuharibu.
Nasema tena tumechoka, na hatuna pa kukimbilia zaidi ya hapa hapa. Bora mkaanza nyie kuondoka kuliko tuwalazimishe, Ole wenu nyie vibaraka, maana mngefikiria hata vizazi nyenu msingefanya hivyo. idios.
CCM nao waandaa mamluki kummaliza
na Waandishi wetu
MGOMBEA urais kupitia Chama cha Maendeleo na Demokrasia (CHADEMA), Dk. Wilbrod Slaa, ameandaa makombora yapatayo 20 yatakayotumika kukimaliza Chama Cha Mapinduzi (CCM) na mgombea wake, Rais Jakaya Kikwete, kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.
Tayari Rais Kikwete na chama chake wameanza kushtuka kuhusu makombora hayo, kwani yamefanyiwa utafiti wa kina na yatatumika kuanika uozo uliokithiri uliofanywa na Serikali ya Awamu ya Nne; na yatatumika kama silaha ya Dk. Slaa katika kuusaka urais.
Vyanzo vya habari kutoka ndani ya chama hicho kikubwa cha upinzani nchini, vimeliambia Tanzania Daima Jumatano kuwa hata hivyo Dk. Slaa hatalipua mabomu hayo hadi kampeni zitakapoanza rasmi mwishoni mwa mwezi huu.
Chanzo cha habari kilisema: Anachokifanya Dk. Slaa hivi sasa ni kujitambulisha kama mgombea, pia kuomba kudhaminiwa, hajaanza kampeni. Atakapoanza mtaona mambo mazito yenye ushahidi wa nyaraka zinazoonyesha ufisadi uliofanywa na viongozi wa serikali katika kipindi hiki cha miaka mitano.
Katika baadhi ya mikutano yake ya hadhara ya kuomba kura, Dk. Slaa mwenyewe amekuwa akiwaambia wananchi kuwa ana mambo mazito yanayohusu ufisadi wa serikali. Baadhi ya mambo hayo amekuwa akiyahoji bungeni kila alipopata nafasi, lakini hayajawahi kupatiwa majibu.
Dk. Slaa ambaye amejipatia umaarufu kutokana na kufanyia utafiti kila jambo analolizungumza, amekuwa akiwaahidi wananchi kuwa kwa vile yuko kwenye mikutano ya kuomba udhamini, ataanza kufyatua makombora hayo wakati wa kampeni.
Itakumbukwa kuwa Dk. Slaa ndiye aliyelipua bungeni bomu la ufisadi mkubwa kupitia Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA); na ndiye alitaja orodha ya mafisadi 11 wakiwamo Rais Kikwete, aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu, Daudi Ballali, Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, Mwanasheria Mkuu wa Serikali wa zamani, Andrew Chenge, waziri wa fedha wa zamani, Basil Mramba na makatibu wakuu, Patrick Rutabanzibwa na Gray Mgonja. Baadhi yao wako mahakamani; wengine tuhuma zao zinaendelea kuchunguzwa.
Walitajwa pia Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono, Rais mstaafu, Benjamin Mkapa na aliyekuwa waziri wa nishati na madini, Nazir Karamagi.
Na ingawa viongozi wakuu walianza kwa kumbeza na kuwateta mafisadi, hivi sasa nao wanajitapa kuwa wameshughulikia ufisadi.
Tangu alipotangaza kuwania urais, Dk. Slaa amewashtua viongozi wakuu na wanachama wa CCM, kiasi kwamba kwa nyakati tofauti Mwenyekiti wake, Rais Kikwete na Katibu Mkuu, Yusuph Makamba, wametoa kauli zinazoonyesha kiwewe walichonacho.
Dk. Slaa, ambaye alifanya kazi kubwa katika Bunge la Tisa, hakuwa akitajwa sana kugombea urais, lakini baada ya CHADEMA kufanikiwa kumshawishi aingie kwenye mbio za Ikulu, ameonekana kuongeza nguvu na umaarufu wa CHADEMA, chama ambacho sasa ndicho kinaonekana tishio kwa CCM.
Hata juzi Rais Kikwete aliporejea kwenye ofisi ndogo za makao makuu ya CCM baada ya kuchukua fomu ya kugombea tena urais, aliwaonya wana CCM wasidharau upinzani, bali wajiandae kufanya kampeni kali ili waweze kushinda.
Aliwaasa waachane na kauli kwamba CCM itatawala milele.
Tanzania Daima limezungumza na vigogo kadhaa wa CCM ambao wamekiri, bila kutaka majina yao yatajwe, kuwa wasipokaa vizuri Dk. Slaa anaweza kujenga wimbi la harakati zinazoweza kuifanya CCM ijikute nje ya serikali au ishinde kwa taabu.
Tayari zipo taarifa zisizothibitishwa kwamba CCM imeshaanza kujipanga kumkabili Dk. Slaa, kwa kuandaa majeshi ya kukodi na kufadhili ili yakisaidie kumshambulia kampeni zitakapoanza, kama njia ya kumpunguza makali.
Baadhi ya viongozi wa vyama vidogo vya siasa na vyombo vya habari vyenye uhusiano na CCM wametajwa kuhusika na njama hizo kwa kupewa ujira mdogo na CCM.
Miongoni mwa hoja wanazoandaa kutumia kama silaha zao ni imani ya Dk. Slaa, ili kumpambanisha na wananchi wasiofuata imani yake; na masuala binafsi kuhusu familia yake.
Hata hivyo, baadhi ya wachambuzi wameonya kuwa iwapo CCM na vyama hivyo watafanya kosa la kuingiza udini katika siasa za nchi, watakuwa wanajichimbia kaburi refu, maana matokeo ya kampeni chafu za viwango hivyo ni mabaya kwa wote, na yanaweza kugeuka silaha kwa wasio madarakani.
Wameonya pia kuwa iwapo masuala ya kifamilia yatageuzwa silaha ya kisiasa kwa wagombea, yanaweza kujitokeza masuala mazito dhidi ya walio madarakani, ambao watakuwa wamempatia Dk. Slaa kombora la nyongeza la 21.
Tayari, baadhi ya makada wa CCM na watumishi wa Ikulu wameshaanza kutumia vyombo vya habari kusambaza uvumi na propaganda dhidi ya Dk. Slaa ili kumchonganisha na wanachama na viongozi wenzake.
Katika hatua nyingine, mwasisi wa mageuzi nchini na mwanasheria maarufu, aliyejiunga na CHADEMA hivi karibuni, Mabere Marando, amesema ana mafaili ya viongozi wa kitaifa yenye sahihi zao, yakionyesha jinsi walivyohusika na kashfa mbalimbali za ufisadi serikalini.
Akihutubia mamia ya wananchi kwenye Uwanja wa Mwembetogwa, mkoani Iringa na Mbeya jana, kwa nyakati tofauti kwa ajili ya kuwaomba ridhaa ya kumdhamini mgombea urais wa chama hicho, Dk. Slaa, Marando alisema ana mafaili ambayo akiyaanika hadharani yatagusa wengi, akiwamo kiongozi mkuu ambaye hakumtaja jina.
Kuna watu wameanza chokochoko eti kwamba uamuzi wangu wa kuingia CHADEMA ni kutaka kudhoofisha vita dhidi ya ufisadi ambayo imekuwa ukiendeshwa na chama hiki, leo (jana) napenda kuwaambia bila woga wowote kwamba pale ofisini kwangu kuna mafaili ya viongozi wa serikali, tena yakiwa na sahihi ya kiongozi mkuu (hakumtaja jina), nikiyaanika haya, hawatajaribu hata kidogo kuchokoza tena, eti mtu ukianza kupata umaarufu wanasema nimeanza jamani nasema mimi sidanganyiki, alisema Marando.
Alisema kwa kipindi kirefu, amekuwa akihusishwa na taarifa kuwa yeye ni ofisa usalama, hivyo amekwenda kufanya uchunguzi CHADEMA, Marando alisema: Kweli mimi ni afisa usalama niliyesomea maeneo mengi, yakiwamo nchini Cuba, nilifaulu vizuri na kuwa tegemeo kwa taifa, hata wakati najiandaa kuondoka kwenye kazi hii, walitaka kunizuia eti kwa kisingizio kwamba maadili hayaniruhusu.
Nikiwa kule sikula kiapo cha kunizuia kuingia kwenye siasa ndiyo maana nikaamua kuingia kwenye upinzani, nimeingia CHADEMA nikiwa nimedhamiria kuandika historia nyingine kwa ajili ya kuwakomboa Watanzania, alisema Marando.
Alisema kama chokochoko hizo zitaendelea atafumua mabomu mazito ya kesi mbalimbali ambazo ziko mezani mwake, hali ambayo itasababisha kampeni za uchaguzi wa rais, wabunge na madiwani kuchimbika.
Akihutubia mkutano huo, Dk. Slaa aliwasihi wakazi wa Mkoa wa Iringa kuacha tabia ya kila uchaguzi kuipigia kura CCM, kwa kuwa imewageuza kuwa mtaji wao kila kukicha.
Nawaambia kama tulivyofanya ukombozi kwenye halmashauri nyingine, tumepeleka ukombozi mkubwa, lakini wananchi wa mkoa huu mnapaswa kubadilika kwa vile tangu mfumo wa vyama vingi umeingia nchini, hamjawahi kutoa mbunge wa upinzani, alisema Dk. Slaa.
Alisema amekamata barua zilizotumwa na CCM makao makuu kwenda kwa wakuu wa wilaya kote nchini, zikiwaagiza kukusanya wafanyabiashara wote kila mkoa kuhakikisha wanaichangia CCM fedha kwa ajili ya kampeni za Uchaguzi Mkuu.
Dk. Slaa alipowasili mkoani hapa, alipokewa kwa maandamano makubwa yaliyotikisa mji wa Iringa kutokana na kupita mitaa mbalimbali kabla ya kuingia kwenye uwanja wa mkutano.
Mara baada ya mkutano huo, Dk. Slaa akitumia ndege ya kukodi aliwasili majira ya saa 11:3 jioni kwenye Uwanja wa Ndege wa Mbeya ambako alipokewa na mamia ya wananchi, waliosababisha shughuli mbalimbali kusimama.
Mamia ya wananchi wakiwemo watu wazima, vijana na watoto, huku wakikimbia mchakamchaka kwa umbali wa zaidi ya kilomita mbili na nusu wakiimba nyimbo za mpisheni rais apite, kiboko ya mafisadi ametua Mbeya. Kadiri msafara huo ulivyosonga mbele, vijana wakiwa na mabango yaliyosomeka Dk. Slaa ulizaliwa uikomboe Tanzania, mafisadi chali, Dk. Slaa mtetezi wa wanyonge, chaguo la Watanzania, mdogo mdogo baba mpaka Ikulu. Dk. Slaa na msafara wake leo wanatarajiwa kuwasili katika mikoa ya Ruvuma, Lindi na Mtwara kwa ajili ya kuendelea kuomba ridhaa ya udhamini wa wananchi kwa ajili ya kugombea urais.
CCM,
Ole wenu mcheze na hisia za watu at this point. Mnachukua kodi zetu kwa ajili ya kutununua just for your primaries. tunajua jinsi mlizofanya na video za haya masibusi zipo na akili inayotumika inajulikana.
Kuna watu wanauchungu na hii nchi na next move kwa taarifa yenu labda mkataze mobile ofisini kwenu.
Hatutaki machafuko ila ujangili wenu tena ukiongozwa na wale wanaojifanya wanajua kuchangia while wamevaa ngozi ya kondoo wamekwisha. Haiwezekani wao kuwa na vipande viwili eti kwa kuwa mnataka kuhalalisha vitumike ndo mtuharibu.
Nasema tena tumechoka, na hatuna pa kukimbilia zaidi ya hapa hapa. Bora mkaanza nyie kuondoka kuliko tuwalazimishe, Ole wenu nyie vibaraka, maana mngefikiria hata vizazi nyenu msingefanya hivyo. idios.