kajembejr
JF-Expert Member
- Jul 31, 2015
- 1,291
- 1,321
Magufuli hana shida tatizo mfumo aliopo
nayeye anayo yakwake ambayo ni matokeo ya mfumo huo unao usema. ..ndani ya ccm ndugu usitegemee kupata msafi, ona sasa mzee warioba kesha tekwa. ..
Magufuli hana shida tatizo mfumo aliopo
*Asema kitanda chenye kunguni hakichomwi moto *Ataka wananchi waichague CCM, aahidi kushughulikia mchwa
Bakari Kimwanga na Raphael Okello, Bunda
MGOMBEA urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli amewaangukia wananchi na kuwaomba wasikiadhibu chama chake katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi ujao.
Mgombea huyo amewaomba wananchi kuichagua CCM na kuahidi kuwashughulikia watu ambao amewaita kuwa ni mchwa, endapo watampa ridhaa.
Akihutubia mamia ya wananchi wa mji wa Bunda mkoani Mara jana, Dk. Magufuli alisema amejipanga vizuri kuwateketeza mchwa hao mara tu baada ya kuingia madarakani.
Nawaoamba wananchi msiiadhibu CCM, kwa kuwa nimejipanga kuwashughulikia mchwa serikalini.
Nawaomba wana Bunda msiipe CCM adhabu kama ambavyo huwezi kuchoma kitanda kinachoingiliwa na kunguni, badala yake utachoma kunguni, acheni tuwachome kunguni walioko serikalini, alisema Magufuli.
Kuhusu suala la kuwapatia wananchi wa Bunda maji, Dk. Magufuli alisema.
Niwaahidi wanabunda, mtapata maji ndani ya miezi mitatu tangu kuunda baraza langu la mawaziri kama waziri wa maji atashindwa kutekeleza ahadi hii, waziri huyo atageuka kuwa maji, alisema huku akishangiliwa na mamia ya wananchi.
Alisema kila sehemu ambayo amekuwa akipita, amekuwa na kazi ya kuwaombea msamaha wagombea ubunge na udiwani na kuwasihi wananchi wawachague ili kama akiingia madarakani wasaidie kuleta maendeleo.
AMANI
Katika hatua nyingine Dk. Magufuli amepuuza hoja za baadhi ya watu wanaodai ametoa kauli za vitisho kwa wananchi kwa kuhusisha uchaguzi na vurugu za nchi ya Libya.
Akiwa katika Wilaya za Butiama, Bunda na Serengeti, kwa nyakati tofauti, Dk. Magufuli, alisema kamwe hataacha kuzungumzia amani japo kuna watu wanachukizwa na kauli yake.
Alisema ataendelea kuhubiri amani ya nchi, kwani asipofanya hivyo ni bora asichaguliwe kuwa rais wa awamu ya tano.
Nimeanzia Butiama kutokana na historia ya amani ya nchi hii. Najua wapo watu eti wanasema nisihubiri amani ya nchi nasema nitaendelea kuisemea wakati wote.
Iwe usiku, mchana na hata wakati wote nitazungumzia amani, nisipohubiri amani basi sisitahili kuwa rais.
leo Mama Maria Nyerere yupo nchini Namibia anapokea tuzo ya amani kwa sababu ya amani ya nchi yetu kutokana na misingi imara iliyowekwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, alisema.
Kauli hiyo imekuja siku moja baada ya Kituo cha Haki za Binadamu na Msaada wa Kisheria (LHRC) pamoja na wasomi mbalimbali, kumtaka mgombea huyo kuacha kutumia mifano ya nchi za Libya na Misri katika kampeni zake.
Itakumbukwa katika nchi hizo, machafuko yalisababisha Kiongozi wa Libya, Kanali Muamar Gaddafi kungolewa madarakani, huku nguvu ya umma nayo ikimuondoa madarakani Rais wa Misri, Hosni Mubarak.
Dk. Magufuli alisema amedhamiria kuwatumikia Watanzania kwa vitendo na atahakikisha anaunda baraza la mawaziri dogo, lakini lenye uadilifu.
JAJI WARIOBA
Naye Waziri Mkuu mstaafu Jaji Joseph Warioba, jana aliibuka kwenye kampeni za Dk. Magufuli na kuwashangaza watu wanaobeza maendeleo yaliyopatikana katika miaka 54 ya uhuru.
Jaji Warioba, alitoa kauli hiyo kwenye uwanja wa Mwenge kijijini Butiama alipopewa nafasi ya kusalimia.
Alisema umefika wakati watu wanaomtumia kama dira Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere katika kampeni zao wajitafakari zaidi.
Bila kutaja jina la mtu, Jaji Warioba alisema wakati wa mchakato wa urais ndani ya CCM kila mgombea alikwenda katika kaburi la Mwalimu Nyerere aliyezikwa eneo la Mwitongo na kuanza mikakati yake.
Wengine katika kampeni zao wanatumia maneno ya Mwalimu kama wamechanganyikiwa. Huwezi kumtumia Mwalimu Nyerere kama dira halafu unasema CCM haijafanya kitu, aliijenga Tanzania kwenye misingi na wote waliomfuata wanapita kwenye misingi yake, alisema Jaji Warioba.
Alisema hatua ya nchi kupoteza maadili ilitokana na uamuzi wa baadhi ya viongozi kuwa na uhusiano na matajiri.
Kwa nini aombe msamaha kwani Waziri Mkuu ndiye Mwenyekiti wa baraza la mawaziri? Ameishawaambia kuwa mamlaka ya juu ilitoa maagizo kuwa mkataba wa Richmond usainiwe kama kawaida, acheni unafiki kwa nini hamtaki kumuwajibisha Kikwete kwa hili?
Anaomba radhi kwa lipi wakati ilani ilyopita wametekeleza kwa asilimia 95 na kuhusu mchwa mbona walisema ni propaganda za upinzani acha tukutane oct 25
Mkuu hawa jamaa wanakera sana tatizo wamejaza Ndugu, watoto mjomba, shangaz huko serikalini alaf risimoja ndio anaamua nan awe rais huyu dogo ndo aliyeharibu
mkuu unajua nafasi ya waziri mkuu kwa mujibu wa katiba? pia kwa nini hataki kusema hiyo mamlaka ya juu ni nani? makamu wa Rais au Rais? kwa nini asimtaje hadharani kama kweli ana nia ya kweli?
tumia akili wewe,unategemea Joni kidevu aseme hatafuta,atapataje kura sasa.hoja hapa ni kwamba wameshaaìdi mara ngapi?Ni kweli kabisa mkuu, lakini John kasema anaenda kufuta huo mtindo, kasema mkwewe ataendelea kuwa mwalimu na watoto wake wataendelea na maisha yao, nadhani tumjaribu huyu jamaa.