Daimler
JF-Expert Member
- Sep 11, 2018
- 556
- 973
Mkuu wa Kitengo cha Political Science, UDSM, Dk. Benson Bana.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dare es Salaam na Mchambuzi wa masuala ya kisiasa nchini, Dk. Benson Bana, amepinga kauli iliyotolewa na Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Bashiru Ally kuwa, kushuka kwa wapiga kura kumetokana na rushwa na kutowajibika; na kudai kuwa, suala la watu kushiriki au kutoshiriki uchaguzi ni hiari. "Nadhani alichokuwa akimaanisha ni watu kujengewa uwezo namna ya kuona umuhimu na thamani ya kushiriki uchaguzi ili kuchagua kiongozi wanayemtaka."