Wiston Mogha
Senior Member
- Feb 13, 2014
- 149
- 96
Dk. Bashiru mjamaa anayeishi kibepari
Na Wiston Mogha
IPO wapi ile akili kubwa aliyokuwa nayo Dk. Bashiru Ally? msomi aliyekuwa akikemea wazi wazi namna dola inavyovibeba vyama tawala. Leo naye amelambishwa asali ya kukaa kwenye VX na kusahau kila kitu.
Huyu sio yule aliyekuwa anazungumza kwa lafudhi tamu ya kiswahili lakini sasa amekuwa anatoa lafudhi chafu ya chooni na hata kuhoji Udaktari wake ameupataje? leo hataki eti tume huru, leo hataki demokrasia ya kuchagua na kuchaguliwa itamalaki kwenye nchi ambayo wazee wetu waliipigania kwa nguvu kubwa.
Hawezi kukemea tena? na ndio maana leo anafanya vichekesho vitupu huku Kigoma, kabebwa na Polisi kuzuia mkutano wa Zitto Kabwe ambaye ni Mbunge wa Kigoma Mjini huku akiwa kwenye magari ya serikali.
Kuhusu magari ya serikali ndio imekuwa mshangao mkubwa sana kwangu leo. Sikujua kama gari za ofisi za serikali zinaweza kutumika kwenye msafara wa kisiasa. Nimeshangaa kuona gari za tanroads zikitumika kumbeba katibu mkuu na wanachama wa CCM. Ajabu kubwa ni kuona mkuu wa mkoa kwenye msafara wa chama akitumia gari ya ofisi yenye namba za *RC KGM* akipeperusha kabisa bendera kwenye msafara wa chama. Wapi tunaelekea?
Leo akemei namna CCM inavyobebwa na dola kwa kugharamikiwa kila kitu ikiwemo taasisi za serikali kutoa msaada kwao kwa kila kitu.
Dk. Bashiru sio yule mjamaa aliyekuwa anahubiri upendo na siasa za kimshikamano bali sasa anahubiri siasa za kumpambania Mwenyekiti wao
Na Wiston Mogha
IPO wapi ile akili kubwa aliyokuwa nayo Dk. Bashiru Ally? msomi aliyekuwa akikemea wazi wazi namna dola inavyovibeba vyama tawala. Leo naye amelambishwa asali ya kukaa kwenye VX na kusahau kila kitu.
Huyu sio yule aliyekuwa anazungumza kwa lafudhi tamu ya kiswahili lakini sasa amekuwa anatoa lafudhi chafu ya chooni na hata kuhoji Udaktari wake ameupataje? leo hataki eti tume huru, leo hataki demokrasia ya kuchagua na kuchaguliwa itamalaki kwenye nchi ambayo wazee wetu waliipigania kwa nguvu kubwa.
Hawezi kukemea tena? na ndio maana leo anafanya vichekesho vitupu huku Kigoma, kabebwa na Polisi kuzuia mkutano wa Zitto Kabwe ambaye ni Mbunge wa Kigoma Mjini huku akiwa kwenye magari ya serikali.
Kuhusu magari ya serikali ndio imekuwa mshangao mkubwa sana kwangu leo. Sikujua kama gari za ofisi za serikali zinaweza kutumika kwenye msafara wa kisiasa. Nimeshangaa kuona gari za tanroads zikitumika kumbeba katibu mkuu na wanachama wa CCM. Ajabu kubwa ni kuona mkuu wa mkoa kwenye msafara wa chama akitumia gari ya ofisi yenye namba za *RC KGM* akipeperusha kabisa bendera kwenye msafara wa chama. Wapi tunaelekea?
Leo akemei namna CCM inavyobebwa na dola kwa kugharamikiwa kila kitu ikiwemo taasisi za serikali kutoa msaada kwao kwa kila kitu.
Dk. Bashiru sio yule mjamaa aliyekuwa anahubiri upendo na siasa za kimshikamano bali sasa anahubiri siasa za kumpambania Mwenyekiti wao