Tua Ngoma
JF-Expert Member
- Apr 14, 2015
- 3,102
- 8,006
Dj fetty ametangaza kuachana na utangazaji na kuwa Mjasiriamali kuanzia leo
==================
SURPRISE! Aliyekuwa mmoja wa watangazaji wa kipindi maarufu cha burudani XXL cha Clouds FM, Fatma Hassan ‘Dj Fetty' leo Sept.15,2015 amewaaga rasmi wasikilizaji na wafanyakazi wenzake kwa madai ya kuachana na kazi ya utangazaji ili kuendeleza biashara zake mpya (Duka la Nguo la Fettylicious lililopo Dar free market).
Siku kadhaa zilizopita, Mwanachama mmoja wa JamiiForums katika jukwaa la Celebrities alihoji kuhusu ukimya wa Dj Fetty kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM, hakika leo majibu yake yamepatikana!
Fetty amesikika kwenye kipindi hicho leo kwa mara ya mwisho kama sehemu ya kusema kwaheri.
Mtangazaji mwenza, Adam Mchomvu alipojaribu kuchombeza kwa kumhoji Dj fetty ni sababu ipi iliyomfanya aamue kuacha kazi yake ya muda mrefu kwa ajili ya biashara ya duka la nguo lililoanza juzi tu, huku akitolea mfano wa duka la Born 2 Shine lililoanza muda mrefu lakini mmiliki wake (B12) hakufikia uamuzi wa kuacha kazi, Fetty akajibu kwa ufupi tu kuwa 'majukumu hayafanani' na kila mtu ana namna anavyoshughulikia majukumu yake.
Katika hatua nyingine, kwa masikitiko makubwa mtangazaji huyo mahiri na mwenye mvuto wa kipekee katika utangazaji wa kizazi kipya alionekana mwenye majonzi na alishindwa kujizuia kutoa machozi na kufikia hatua ya kuvaa miwani ili kuficha taswira ya huzuni aliyonayo!
Pia, kuonyesha ni namna gani ameguswa na kuondoka kwa Dj Fetty, B-Dozen amekaririwa akisema,"Nakupenda sana fettythebest na siku ukitaka kuja kwenye #Xxl we niambie utakuja tu mana bado tunakuhitaji".
Kipindi cha XXL ambacho huongozwa na B Dozen akishirikiana na Adam Mchomvu sasa kimepata member mpya, Kennedy The Remedy aliyechukua nafasi ya Fetty akitokea East Africa Radio (The Cruise).
Kennedy The Remmedy ameungana rasmi na familia ya XXL.
==================
SURPRISE! Aliyekuwa mmoja wa watangazaji wa kipindi maarufu cha burudani XXL cha Clouds FM, Fatma Hassan ‘Dj Fetty' leo Sept.15,2015 amewaaga rasmi wasikilizaji na wafanyakazi wenzake kwa madai ya kuachana na kazi ya utangazaji ili kuendeleza biashara zake mpya (Duka la Nguo la Fettylicious lililopo Dar free market).
Siku kadhaa zilizopita, Mwanachama mmoja wa JamiiForums katika jukwaa la Celebrities alihoji kuhusu ukimya wa Dj Fetty kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM, hakika leo majibu yake yamepatikana!
Fetty amesikika kwenye kipindi hicho leo kwa mara ya mwisho kama sehemu ya kusema kwaheri.
Mtangazaji mwenza, Adam Mchomvu alipojaribu kuchombeza kwa kumhoji Dj fetty ni sababu ipi iliyomfanya aamue kuacha kazi yake ya muda mrefu kwa ajili ya biashara ya duka la nguo lililoanza juzi tu, huku akitolea mfano wa duka la Born 2 Shine lililoanza muda mrefu lakini mmiliki wake (B12) hakufikia uamuzi wa kuacha kazi, Fetty akajibu kwa ufupi tu kuwa 'majukumu hayafanani' na kila mtu ana namna anavyoshughulikia majukumu yake.
Katika hatua nyingine, kwa masikitiko makubwa mtangazaji huyo mahiri na mwenye mvuto wa kipekee katika utangazaji wa kizazi kipya alionekana mwenye majonzi na alishindwa kujizuia kutoa machozi na kufikia hatua ya kuvaa miwani ili kuficha taswira ya huzuni aliyonayo!
Pia, kuonyesha ni namna gani ameguswa na kuondoka kwa Dj Fetty, B-Dozen amekaririwa akisema,"Nakupenda sana fettythebest na siku ukitaka kuja kwenye #Xxl we niambie utakuja tu mana bado tunakuhitaji".
Kipindi cha XXL ambacho huongozwa na B Dozen akishirikiana na Adam Mchomvu sasa kimepata member mpya, Kennedy The Remedy aliyechukua nafasi ya Fetty akitokea East Africa Radio (The Cruise).
Kennedy The Remmedy ameungana rasmi na familia ya XXL.