Diwani wa kata ya kijitonyama (Dsm) ambaye pia ni mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Ally maua kupitia CHADEMA Juma Athman Uloleulole, amedakwa na polisi na kufikishwa kituoni kwa kosa la kumdhalilisha kijinsia yatima na baadaye kumuomba rushwa ya ngono.
yatima huyo aitwaye Sylvia Kigola (19) alienda kulalamika polisi kwamba alipoenda kwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Ally maua kuandikiwa barua ya dhamana kwa ajili ya kwenda kuomba kazi ndipo mwenyekiti huyo alimgeuzia kibao na kumbaka.
Amefunguliwa kesi jalada no.KJN/RB/1117/2012.
Tukio hilo lilishuhudiwa na waandishi mbalimbali wa habari akiwemo wa ITV.
Source:taifa letu Tarehe 17.02.2012 ukurasa wa kwanza.
My take:Ni aibu kwa kiongozi wa umma kufanya kitendo kama hiki.hatua kali za kisheria zichukuliwe baada ya kuthibitika.