DIWANI wa Chama cha Wananchi (CUF) Kata ya Kibada, amesema kauli ya Mbunge wa Kigamboni, Dk. Faustine Ndungulile, kuwa ni miongoni mwa madiwani wanne waliohongwa na Waziri wa Ardhi ili kuunga mkono ujenzi wa mji mpya wa Kigamboni haina athari kwake.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana diwani huyo, Juma Nkumbi alisema kauli ya mbunge huyo inaonyesha ni jinsi gani alivyofilisika kisiasa mbele ya jamii.
Alisema kutokana na mbunge huyo kushindwa kwake kutoa ushahidi dhidi ya kauli yake hiyo, moja kwa moja imekidhihirishia chama chake kuwa hakuhusika na kitendo hicho.
Nkumbi alisema mbunge huyo amekuwa akitapatapa, kutafuta umaarufu baada ya kupoteza imani kwa wananchi wa jimbo hilo kutokana na kushindwa kwake kwa makusudi kusimamia kero zao.
Aliongeza kuwa kauli ya Dk. Ndungulile ni ya kutaka kuwachonganisha wananchi wa Kigamboni ambao hawapingi mradi huo isipokuwa wanataka tathmini ya mali zao ifanyike kwa kuzingatia haki na walipwe vizuri.
Nkumbi alisema kwa kudhihirisha kuwa mradi huo unakubalika, ni hivi karibuni wenyeviti wa mitaa wa jimbo hilo, walimtembelea bungeni, na kumweleza mbunge wa Temeke, Abas Mtemvu, ambaye ni mwenyekiti wa wabunge wa Dar es Salaam kuwa kauli za Dk. Ndungulile ni mawazo yake binafsi.
Akichangia hotuba ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi juzi, Dk. Ndungulile alidai kuwa madiwani hao wanne Juma Nkumbi (Kibada), Suleiman Mathew (Vijibweni), Albert Luambano (Tungi) na Doto Msawa, walihongwa na waziri ili wakubali mradi wa mji mpya wa Kigamboni.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.