ALWATAN KIZIGO
JF-Expert Member
- Dec 21, 2012
- 539
- 642
Kinara wa biashara za magendo Wilayani Kilwa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashahuri ya Wilaya ya Kilwa Ndugu. Abuu Musa Mjaka (CUF) amekamatwa na Mbao za Magendo vipande 400 Nyumbani kwake.
Taarifa ambazo zimethibitishwa na mkuu wa wilàya ya Kilwa,Christopher Ngubiagai zimeeleza kwamba diwani huyo wa kata ya Masoko(CUF) anatuhumiwa kukutwa na vipande vya mbao takribani 400 ambazo vimevunwa bila ya kufuata utaratibu wa kisheria.
"Huyo mheshimiwa nikweli amekamatwa usiku huu.Yupo kituo cha polisi cha Kilwa Masoko.At amekutwa na mbao takribani 400 ambazo zilikuwa nyumbani kwake.Lakini hakuonesha nyaraka zinazoonesha kuwa ni halali," alisema Mwenyekiti huyo wa Kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Kilwa.
Wilaya ya Kilwa ni miongoni mwa Wilaya zinazoongoza kwa biashara haramu ya magendo ya maliasili kna ndio maana Ofisi ya Mkuu wa Wilaya imeamua kupambana na Biashara za Magendo kwa udi na uvumba.
Taarifa ambazo zimethibitishwa na mkuu wa wilàya ya Kilwa,Christopher Ngubiagai zimeeleza kwamba diwani huyo wa kata ya Masoko(CUF) anatuhumiwa kukutwa na vipande vya mbao takribani 400 ambazo vimevunwa bila ya kufuata utaratibu wa kisheria.
"Huyo mheshimiwa nikweli amekamatwa usiku huu.Yupo kituo cha polisi cha Kilwa Masoko.At amekutwa na mbao takribani 400 ambazo zilikuwa nyumbani kwake.Lakini hakuonesha nyaraka zinazoonesha kuwa ni halali," alisema Mwenyekiti huyo wa Kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Kilwa.
Wilaya ya Kilwa ni miongoni mwa Wilaya zinazoongoza kwa biashara haramu ya magendo ya maliasili kna ndio maana Ofisi ya Mkuu wa Wilaya imeamua kupambana na Biashara za Magendo kwa udi na uvumba.