95. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha awamu ya tatu tumeweza kupata mafanikio mengi katika kukuza uchumi wetu. Hata hivyo, ili kuweza kufikia malengo ya Dira ya Taifa 2025, na kuweza kulingana na nchi zenye kipato cha kati, uchumi wa nchi unatakiwa kukua kwa kiwango kisichopungua asilimia 8 juu ya kiwango cha ongezeko la idadi ya watu. Kiwango cha ongezeko la idadi ya watu kinakua kwa asilimia 2.9. Hivyo hatuna budi kuboresha na kuendelea kusimamia utekelezaji wa Sera na mikakati yetu ili tuweze kufikia malengo makuu ya Dira ya Taifa 2025, kama ilivyokusudiwa.
96. Mheshimiwa Spika, napenda kuelezea kuwa tegemeo kubwa la kuleta mabadiliko ya kiuchumi nchini liko kwa wananchi wenyewe ambao wanatakiwa kutumia fursa zilizopo na kukabili vikwazo kwa lengo la kuongeza tija kwa kasi kubwa na kukuza uchumi wetu ili tuondokane na umasikini tulio nao. Hivyo ni wajibu wa kila mmoja wetu kuchukia umasikini na kuhimizana kufanya kazi kwa bidii na kutumia kwa umakini, fursa na rasilimali zilizo katika uwezo wetu ili kujiletea maendeleo. Serikali itaendelea na jukumu la kuunga mkono juhudi za wananchi kwa kuandaa sera na mikakati ya kuelekeza namna ya kuratibu, kusimamia pamoja na kutathmini ili tuwe na maendeleo yenye kuwiana katika kila ngazi. Nina hakika kuwa kila mmoja wetu akitimiza wajibu wake sawasawa tutakuwa na kasi ya ukuaji wa uchumi unaopanda mwaka hadi mwaka na kufikia malengo yetu ya Dira ya taifa 2025, na kufanikisha kupunguza umasikini kwa kiwango kikubwa. Hakika, Serikali ya Awamu ya Nne, itayalinda na itayaendeleza mafanikio ya Awamu ya Tatu kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya.
Katika kongamano la Taasisi za kidini nchini, lililofanyika Whitesand mgeni rasmi akiwa Dr J.M Kikwete rais wa J.M Tanzania, Waziri mwenye dhamana ya Madini yetu Prof. Muhongo ametuhakikishia kwamba kufikia mwaka 2025 Tanzania itakuwa imetoka kwenye umasikini nakuwa kwenye kiwango chakati.. Akisema kwakujiamini kuwa Kilimo ambao ndio uti wa mgongo umeshindwa kutukomboa, ufugaji umeshindwa pia, kasema yeye mtu wakanda ya Ziwa uvuvi nao haujawakomboa. Lakini Neema hii ya Gesi asilia itatutoa kwenye umasikini kwani wizara yake haina Mlarushwa, Hakuna Mhaini wala Mlaghai pale Wizarani kwake.
Kwahyo wadau tuombe Mungu mipango iende sawa.
Sio tukae tuombe Mungu tu,tunataka matunda ya gesi na mafuta kila mtanzania ayaone na kuneemeka nayo. Kwa kuanzia,bei ya umeme ishuke haraka sana! Ndipo tutaelewana.
Kwahyo wadau tuombe Mungu mipango iende sawa.
SOUTH SUDAN CONTRADICTION 6: Its $1800 per-capita income highest in EA but girls 15-19 yrs more likely 2 die in childbirth than finish high sch
SOUTH SUDAN CONTRADICTION 5: Its $1800 per-capita annual income highest in region, but it has world's 2nd-highest maternal mortality rate
SOUTH SUDAN CONTRADICTION 4: Its $1800 per-capita annual income highest in Eastern Africa, but 75% of its pple have no access to toilets
SOUTH SUDAN CONTRADICTION 3: Its $1800 per-capita annual income highest in Eastern Africa, but it has 75% illiteracy rate
SOUTH SUDAN CONTRADICTION 2: Its $1800 per-capita annual income highest in Eastern Africa, but, 47% of population suffers malnutrition
SOUTH SUDAN CONTRADICTION 1: Its $1800 per-capita annual income highest in Eastern Africa, but its 51% poverty rate also the highest
Hajasema tarehe ngapi ili tuisubiri kwa hamu?
MAOMBI MAZITO YANAHITAJIKA NA MUUJIZA WA PEKEE
Mkuu swat nimekusoma vizuri kuwa niwajibu wetu kuhakikisha tunapata matunda ya Gesi hata kama sio mimi na wewe lakini hata kwa vizazi vinavyokuja..
Lakini usisahau pia M/Mungu ni mjuzi wa wote kwa yote na tunapaswa kumuomba mipango yetu tuliojiwekea inakwenda sawa.
Katika kongamano la Taasisi za kidini nchini, lililofanyika Whitesand mgeni rasmi akiwa Dr J.M Kikwete rais wa J.M Tanzania, Waziri mwenye dhamana ya Madini yetu Prof. Muhongo ametuhakikishia kwamba kufikia mwaka 2025 Tanzania itakuwa imetoka kwenye umasikini nakuwa kwenye kiwango chakati.. Akisema kwakujiamini kuwa Kilimo ambao ndio uti wa mgongo umeshindwa kutukomboa, ufugaji umeshindwa pia, kasema yeye mtu wakanda ya Ziwa uvuvi nao haujawakomboa. Lakini Neema hii ya Gesi asilia itatutoa kwenye umasikini kwani wizara yake haina Mlarushwa, Hakuna Mhaini wala Mlaghai pale Wizarani kwake.
Kwahyo wadau tuombe Mungu mipango iende sawa.