Dikteta Iddi Amin alikusanya kodi kwa "task force", hatujifunzi

Dikteta Iddi Amin alikusanya kodi kwa "task force", hatujifunzi

KooZito

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2020
Posts
397
Reaction score
1,378
Nimewasikia wabunge wakiionya Serikali ya Magufuli kuacha kukusanya kodi kwa "task force" yani Polisi, TRA na Afisa wa Usalama Taifa.

Matokeo yake pesa zao zinaporwa, wanafunga biashara, wanajiondokea. TRA wanadanganya eti biashara zinafungwa lakini zinafunguliwa nyingi. Uongo wa mchana.

Ndugu zangu nimefanya ziara ya kimya kimya jijini Dar. Ukweli tangazo la "To Let" sasa ni kila mahali maana waliokuwemo wamefunga biashara kwa kuogopa kesi za uhujumu uchumi na pesa zinapokwa Benki.

Iddi Amin alijaribu mtindo huu wa ukusanyaji wa kodi kwa "task force". Matokeo yake wafanyabiashara wa ki-Asia wakakimbia Uganda na kwenda kwingine duniani hasa Canada.

Alipoingia madarakani Yoweri Museven akigundua tatizo hilo. Ni mtaalamu wa Tanzania wa uchumi aliyekwenda Uganda na kushauri kuanzishwa URA. Leo, Uganda unaongoza EAC kwa ukusanyaji wa kodi kwa hiari na maelewano. Wametoa elimu ya kodi si Polisi.

Ziara yangu kupitia umoja wa wafanyabiashara wa ki-Asia wapatao 639 tayari wamefunga na kuondoka nchini. Wengine 29 wameanza kufunga watajiondokea.

Mwisho sekta ya biashara itazama. Serikali iwe makini kwenye hili. Uhujumu uchumi isiwe rungu.

Ilimgharimu Museveni kuwabembeleza waliokimbia kurejea Uganda akakaa nao kirafiki akiwaambia, "tushirikiane kuijenga upya Uganda". Tujitafakari.
 
Kodi lazima ilipwe eti wafanya biashara 600+ wa kiasia umewatoa wapi na uliukuwa unaandika kila mmoja hizi hoja za vijiwe vya kahawa hizi leo zinapelekwa bungeni

Hawa magabachori kina manji wacha wakimbie tu na TRA kila siku inavuka kiwango cha ukusanyaji

Mwambieni mbowe alipe kodi la sivyo akimbie na yeye
 
Kodi lazima ilipwe eti wafanya biashara 600+ wa kiasia umewatoa wapi na uliukuwa unaandika kila mmoja hizi hoja za vijiwe vya kahawa hizi leo zinapelekwa bungeni...
Kiongozi sometimes ni vyema sana kuushirikisha mwili mzima wakati unajadili na kuandika uzi mbali mbali. Ukitumia mahaba peke yake ukaacha akili ni shida, ukitumia mahaba ukaacha busara pia ni shida na hata ukitumia mahaba ukaacha ukweli ni shida sana. Jipe muda, jipe nafasi, chambua mada kisha itazame kwa 3d alafu toa majibu yako.

Huo ndio uungwana mkuu. Nikutakie mchana mwema kiongozi.
 
Kiongozi sometimes ni vyema sana kuushirikisha mwili mzima wakati unajadili na kuandika uzi mbali mbali. Ukitumia mahaba peke yake ukaacha akili ni shida, ukitumia mahaba ukaacha busara pia ni shida na hata ukitumia mahaba ukaacha ukweli ni shida sana. Jipe muda, jipe nafasi, chambua mada kisha itazame kwa 3d alafu toa majibu yako.

Huo ndio uungwana mkuu. Nikutakie mchana mwema kiongozi.
Wauza unga kama wewe mnadhani akitoka Magufuli mtaachiwa mchezee nchi
 
Kodi lazima ilipwe eti wafanya biashara 600+ wa kiasia umewatoa wapi na uliukuwa unaandika kila mmoja hizi hoja za vijiwe vya kahawa hizi leo zinapelekwa bungeni

Hawa magabachori kina manji wacha wakimbie tu na TRA kila siku inavuka kiwango cha ukusanyaji

Mwambieni mbowe alipe kodi la sivyo akimbie na yeye
Ungeacha wajadili wenye akili kwanza.
 
Kodi lazima ilipwe eti wafanya biashara 600+ wa kiasia umewatoa wapi na uliukuwa unaandika kila mmoja hizi hoja za vijiwe vya kahawa hizi leo zinapelekwa bungeni

Hawa magabachori kina manji wacha wakimbie tu na TRA kila siku inavuka kiwango cha ukusanyaji

Mwambieni mbowe alipe kodi la sivyo akimbie na yeye

Mimi maenyewe nilifunga toka 2016 niko zangu kitwe nasafirisha mzigo, unafika bandarini nalipa kama transit navusha nakonde nashusha kitwe nauzia wacongo na siko peke yangu tuko 12 tuliokuja huku na maduka tulifunga muendelee kuangalia hiyo milango tutakutana krismasi then tunarudi kupiga kazi huku, karibu Zambia, ulibwaanji?
 
Mataga wangejua yatatokea haya tungekuwa nao mbele kutetea nchi yetu lakini waliamua kutaka sifa sasa tunaumia wote.
 
Mimi maenyewe nilifunga toka 2016 niko zangu kitwe nasafirisha mzigo, unafika bandarini nalipa kama transit navusha nakonde nashusha kitwe nauzia wacongo na siko peke yangu tuko 12 tuliokuja huku na maduka tulifunga muendelee kuangalia hiyo milango tutakutana krismasi then tunarudi kupiga kazi huku, karibu Zambia, ulibwaanji?
TBL na TCC wamepunguza uzalishaji kwa asilimia 30
 
Mleta mada unayosema kuhusu ukusanyaji wa kodi ni ya kweli lakini la wafanya biashara wenye asili ya Asia kuondoka Uganda chanzo hakikua kodi ila ni roho mbaya tu ya Iddi Amin aliwafukuza na kuwapa Waganda maduka na mali za Waasia.

Waganda hawa hawakua na elimu wala ujuzi wa biashara na matokeo yake biashara zilikufana uchumi wa Uganda uliyumba.

Waasia ni wafanya biashara wazuri, hata Oman, Canada, Ulaya na Marekani wameshamiri. Tatizo la Wahindi hata kwao India wanajua sana ku dodge kodi. Wanasema India kama wafanya biashara wote wangelipa kodi uchumi wao ungeshindana na uchumi wa Ujerumani.
 
TBL na TCC wamepunguza uzalishaji kwa asilimia 30

Ninaweza kukutajia kwa uhakika tulioondoka kisa madhira ya kukadiliwa kodi kubwa, nakumbuka nilitoka siku hiyo TRA mkoa fulani wa kikodi nimechanganyikiwa, nilikaa wiki nzima ndani ikabidi niandike kufunga biashara, ndio nikaona ushauri wa kujiongeza ili nisitoke barabarani hali ikitulia nitarudi, hakuna mtu asiependa kulipa kodi ili nchi yake isonge mbele lakini unajikuta umekuja na mtaji huku unalipia kodi nchi nyingine na sio nchi yako inauma lakini utafanyeje,
 
Mtu ukiwa unavusha mzigo au harakati za kuuclear zinafanyika huku roho inakuuma kuona unapeleka mzunguko wa pesa nchi nyingine kisa makadirio ambayo sio rafiki, mzunguko kwenye biashara unaonekana ni tsh. Mil 30 ukadiriwe mil 70 hapo inabidi ujichange uondoke kama hivi walau mtu uwe barabarani hakuna jinsi
 
Kiongozi sometimes ni vyema sana kuushirikisha mwili mzima wakati unajadili na kuandika uzi mbali mbali. Ukitumia mahaba peke yake ukaacha akili ni shida, ukitumia mahaba ukaacha busara pia ni shida na hata ukitumia mahaba ukaacha ukweli ni shida sana. Jipe muda, jipe nafasi, chambua mada kisha itazame kwa 3d alafu toa majibu yako.

Huo ndio uungwana mkuu. Nikutakie mchana mwema kiongozi.
Mkuu watu wa type hii, utaumiza kichwa, Tanzania Kuna kizazi Cha ajabu, sijui ni chipsi na kuku za kisiasa ndo zinaalibu kizazi hiki, mtu anaangalia alipo bila kuangalia kesho Kama vile ataishi milele, bongo zetu hatuzishughulishi, kila kitu sawa, kizazi hiki hakijiamini, upeo wa kupembua Mambo ,hasara ,faida, zake hakuna, mpaka Sasa Hata elim za vyuo hazisaidi ,tupo tupo tunaenda ili mladi ushabiki tu,
HOJA YAKO INA MASHIKO SANA, TENA SANA MKUU
 
Back
Top Bottom