Digital na Tanzania

Digital na Tanzania

DIBA Kims

Member
Joined
Dec 28, 2012
Posts
7
Reaction score
3
Leo asubuhi rafikizangu wa kijijini wameniambia kua Tanzania inaingia vita na Malawi2013 ndiyo maana serikali ina himiza haraka watu waingie kwenye Digital ili wale wenye uwezo mdogo wasijue mambo yanakwendaje. Hivyo wakeomba ni wathibitishie kama si kweli au kweli. Na mimi nahitaji mawazo yenu wanajamii ciz hata mimi juu ya Teknolojia mpya sawa lakin wananchi wanaumia kwa kubebeshwa mzigo wa gharama za kuishi
 
Leo asubuhi rafikizangu wa kijijini wameniambia kua Tanzania inaingia vita na Malawi2013 ndiyo maana serikali ina himiza haraka watu waingie kwenye Digital ili wale wenye uwezo mdogo wasijue mambo yanakwendaje.

.....duh......

....Uamuzi wa kubadili mfumo wa utangazaji wa televisheni kwenda mfumo wa digitali sio uamuzi wa Tanzania peke yake,ni uamuzi wa dunia kupitia shirika la Mawasiliano Duniani(ITU),ukizingatia kuwa mawimbi hayana mpaka hivyo mashirikiano kimataifa ni muhimu,hasa maeneo ya mipakani,mwisho wa urushaji matangazo ya analojia duniani ni 2015...

....lakini nchi za Afrika Mashariki,Tanzania ikiwemo zikaamua mwisho wa urushaji wa analojia kwa nchi hizi iwe ni 31/12/2012,ikizingatiwa kuwa kwenye nchi maskini kama zetu changamoto za kushindwa kumeet deadline zinawezekana,hivyo atleast mwisho ukiwa miaka 3 kabla ya deadline ya dunia,then miaka hiyo 3 kabla ya deadline ya dunia itatumia kuboresha mapungufu yatakayojitokeza....


...Umuhimu wa kwenda digitali kwanza ni matumizi mazuri ya masafa,kwenye analojia kila televisheni statiob ilihitaji kuwa na safa(frequency) yake,lakini kwenye digitali safa moja linaweza likabeba stations ata zaidi ya 200,hivyo kwa kwenda digitali uhaba wa masafa ya televisheni unaisha,lakini pia masafa mengine yaliyokuwa yanatumia na televisheni yatatumiwa kwa shughuli zingine,mitandao ya internet,na baadae redio za digitali,kwa ujumla wake hatua hii itaibua fursa kubwa zaidi ya kuanzishwa kwa vituo vingi zaidi vya televisheni na hivyo kuongeza ajira,kodi kwa serikali na upataji wa taarifa/habari nyingi zaidi,kwa picha bora zaidi zisizo na chenga kwa wananchi...


...Sio hivyo tu lakini pia kwa kuwa teknolojia zingine za mawasiliano kupitia simu na computer tayari ni za digitali,kwa televisheni kuwa digitali kitaalamu kuna uwezekano sasa wa kuunganisha utendaji wa vifaa hivi,huduma za kimawasiliano zinazopatikana kupitia computer na simu zitaweza kupatikana kupitia televisheni yako ya digitali..


...Na ifahamike kuwa majumbani mwetu tunapata matangazo ya televisheni kupitia sattelite aka ungo,cable au antenna aka chadema,watakaoathiriwa na mabadiliko hayo ni wake tu wanaotumia antenna kupata matangazo ya televisheni,wale wanaotumia ungo na wale wanaotumia cable wataendelea na nyungo na cable zao bila kuathiriwa kwa lolote,wale wanaotumia antenna ndio watapaswa kuwa na televisheni ya digital au kununua king'amuzi ili kiwassidie kupata matangazo ya digitali kupitia televisheni zao za analojia..
 
Kikwete alikuwa sahihi. Viwanda vya kuzalisha uongo bongo vimeshamiri.. Siyo kweli kwa sababu huu ni mpango wa kimataifa. kufika mwaka 2015 television zote zinatakiwa kuwa digital. Marekani walifanya hii 2009. Pili kwa Tanzania wanaanza na mikoa baadhi. Tatu watu wengi wa vijijini wenye television wamekua wakiangalia tv kupitia satelite, hao wataendelea hivyo.

Gharama za maisha haziepukiki ndugu yangu ndo maisha
 
Mwambieni MMK aje awasaidie kuwatoa ujinga wabongo,
 
Junior MemberArray


Join Date : 28th December 2012
Posts : 1
Rep Power : 0
Likes Received0
Likes Given0
 
great thinker lazima uwe unaweza kupambanua mambo,sasa hili wewe haujalipima kwenye kichwa chako unalileta jamvini,pimeni kwanza mambo ndiyo muandike.
 
Shule ni muhimu sana hasa kwa watu kama nyie.
 
Nikweli naelewa juu ya umuhimu wa digital nimejaribu kuweka kwenu ili mjue watanzania wengi hasa wa vijijin wanawaza nini juu ya mabadiliko ya digital
 
Zigo lote hili la lawama mnalomtupia huyu jamaa , ni matokeo ya kuchagua CCM.
 
Back
Top Bottom