Likitokea kosa kwenye diesel Engine Machine Kimakosa ukaweka Petrol ina maana hiyo machine itakuwa imekufa ama kuna namna unaweza rekebisha?
I stupidly put petrol in my 10 KVA silent Diesel Generator.....naogopa hata kuliwasha.
Ushauri
Pole sana mkuu ila hilo sio jambo la kutisha kihivyo, kwanza kabisa usiliwashe hilo jenereta, tafuta fundi mzuri amwage mafuta yote na asafishe tanki. Kisha afanye pia quick check ya pump na diesel filter. Baada ya hapo liwashe tu, litapiga mzigo kama kawa.
usiiwashe, wasiliana na mtaalamu wa diesel engine aisafishe engine ya hiyo generator ili kuondoa petrol yote iliyoingia ndani
Acha tu ndugu yangu! Haya matatizo yamenikumba bila kujua.
Mkuu huyo fundi gani anaekwambia unnue pampu na filltar mpya Dieasal haina tabu. na madam hukuliwasha hata kama uliwasha haliwezi kuleta tabu nikutoa petroli iliyomo kwenye tanki nakuweka dizeli haihitaji kusafisha hiyo kazi unaweza kufanya mwenyewe haihitaji fundi mkuu, mashine ya petroli ukitia dieasel ndio itahitaji kusafishwa kwakuwa kwakuwa diesel ni nzito au mafta ya taa. lakini mashine ya dieasel haina shida petrol ni nyepesi sana haitazuru kitu mkuu wala usinunue pampu. na filltar isafishe tu
Nadhani shida ni Mgawo wa DOWANS na mmiliki wake ninamjua! Kikwete aliyesema hamjui Brg Alli Hadaiwi
Dowans hawajaleta mgao hapa, Dowans walikuja kutatua mgao. Be realistic. Adawi kakosa nini wakati mitambo iko pale Ubungo? wacha! kuwa na ukweli katika dhamira zako. Kukosa ukweli mpaka mind imezowea kujidanganya mnatia petroli sehemu ya kuwekwa diesel.
Jinsi tulivyokuwa na akili finyu, mitambo ipo uwani, tunashindwa kuitumia, kwa upumbavu wetu tu, mwisho wa siku tunadaiwa halafu tunalaumu. Dowans na Adawi tungewajuwa Nyerere asingeteketeza uchumi wetu? Na angewacha mashirika yawe binafsi toka enzi zake? Nyerere mwenyewe kakubali kuwa alifanya makosa, halafu nyinyi mnakataa hata aliyokubali mwenyewe. Mnashangaza sana!