Tetesi: Diamond kumjengea bonge la jumba na kumpa baadhi ya mali zake baba yake wa kambo

Hance Mtanashati

JF-Expert Member
Sep 7, 2016
17,415
21,111
Kwa habari zilizo chini ya kapeti ni kwamba mwanamuziki ambaye pia ni mfanyabiashara mkubwa hapa nchini na Africa kwa ujumla Diamond Platnums Chibu Di Chibu De a.k.a Muuza Karanga anataka kumjengea bonge moja la jumba mithili ya kasri baba yake wa kambo pamoja na kumuingiza katika baadhi ya mali zake ili apewe muongozo mzuri wa baba yake huyo wa kambo.

Haya yote yamefanyika kutokana na Bi Sandra kumng'ang'aniza sana Dai ingawaje mwanzoni ilikuwa ngumu kukubali ila mwishoe Diamond aliamua kukubali ili tu amridhishe mama yake maana ametoka naye mbali sana na amemlea kwa shida hivyo basi hawezi kumpinga jambo lolote atakalo ambiwa.

Diamond kwa kiasi fulani hana furaha kabisa kwa huyu baba yake wa kambo ila tu anajitahidi kufosi furaha ili asimkwaze bi Sandra.

Mpaka sasa hilo kasri halijajulikana litaenda kushushwa wapi ila litakuwa miongoni mwa sehemu zilizotulia nje ya Dar.

Screenshot_2017-12-16-17-55-29.jpg

Hapa wakiwa na wajukuu zao, Nillan na Tiffa.

Halafu nilipata habari kwamba Bi Sandra alikuwa wa kwanza kumtongoza jamaa na kumpa ahadi kedekede kama atakubali kuwa naye. Jamaa alitia ngumu mwishoye akalainika.

Ila kwa kweli Bi Sandra mwishowe amtie jakamoyo Diamond bure ashindwe kutengeneza ngoma nzuri kwa stress kama hizi na fedheha.

Haya cc wambea wote mje hapa tujadiliane.
 
Inshort huyu kaka naskia ni mjanja sana yani yupo kimaslahi zaidi. Na nnasikia huyu mama kwa sasa ni mjamzito na soon anatarajia kujifungua yaani huyu kaka ndio anayefaidi hela za diamond kwa sasa kupitia mgongo wa mama yake bi sandra

Kiukweli mapenzi hayana umri so tumuacheni na maisha yale wapendwa ila huyu mama aache kujianika tu mitandaoni maaana anatia aibu sana
 
Back
Top Bottom