PROFESA KYANDO
Member
- Jul 24, 2012
- 81
- 6
[h=2][/h] Ijumaa, Agosti 24, 2012 05:46 Na waandishi Wetu, Mikoani
KINDUMBWENDUMBWE cha kuwania nafasi ya uongozi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimezidi kushika kasi huku baadhi ya wagombea wakiweka wazi mikakati yao.
Hata hivyo mchuano mkali ukitarajiwa kuwa kati ya Mwenyekiti wa sasa anayemaliza muda wake Clement Mabina na aliyekuwa Mbunge wa Ilemela (CCM), Antony Diallo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana baada ya kurejesha fomu ya kuwania nafasi ya Uenyekiti Mkoa wa Mwanza, Dk. Antony Diallo, alisema endapo atafanikiwa kuwa Mwenyekiti wa chama hicho atapiga marufuku matumizi ya magari ya chama kutumika kwa shughuli binafsi.
Alisema hatua hiyo itakuwa ni njia ya kukipunguzia chama gharama za uendeshaji.
Diallo, ambaye pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), anayemaliza muda wake alisema kuna baadhi ya viongozi wamekuwa wakitumia mali za chama yakiwemo magari kwa ajili ya shughuli binafsi badala ya magari hayo kutumika kukiimarisha chama.
"Kama wewe ni Mwenyekiti gari hilo linapashwa kukuchukua siku ya vikao rasmi na shughuli rasmi, Mwenyekiti wa chama sio Mwenyekiti mtendaji gari la nini unataka ukae nalo na ulitumie kwa shughuli zako binafsi,huku ni kunibebesha chama mzigo wa gharama.
Chama kinahitaji mtu ambaye atakiongoza kama taasisi na sio kama mali yake binafsi,pia inahitajika mtu ambaye atawaunganisha wanachama na sio kuwagawa na mtu huyo ni mimi Dk Diallo, alisema.
Katika hatua nyingine Katibu wa ccm wilaya ya Nyamagana Deogratius Rutta amekwaa kisiki baada ya kuangushwa vibaya katika kuwnaia nafasi ya ujumbe wa mkutano mkuu wa ccm taifa kupitia nafasi tatu za wazazi.
Katibu huyo aliibuka na kura 71 ambapo washindi watatu waliopatikana ni Samson Ntambi, Raphael Shilatu pamoja na Emanuel Nzungu.
Dk. Kigwangalla: Uongozi siyo mvi
Kwa upande wake mbunge wa Nzega mkoani Tabora, Dk. Hamisi Kigwangalla (CCM), amesema uongozi unahitaji uwezo na hekima ya mtu na siyo kigezo cha umri mkubwa.
Dk. Kigwangalla ambaye amejitosa kuwania nafasi ya Uenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), ALISEMA ana uwezo wa kuiongoza Jumuiya hiyo ambayo hivi sasa ina taswira ya watu waliokula chumvi.
Uongozi siyo mvi, bali ni jambo linalohitaji uwezo na hekima ya mtu bila kujali umri wake wa uzee au ujana, alisisitiza Dk. Kigwangalla ambaye ni kijana mwenye umri wa miaka 37.
Alikuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ya CCM Mkoa wa Mwanza, mara baada ya kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa na CCM kugombea nafasi ya uenyekiti wa Jumuiya hiyo ngazi ya Taifa.
Wakati hayo yakiendelea Watanzania wametakiwa kuelewa kuwa ufisadi haupo ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) peke yake bali hata katika vyama vya Upinzani pio.
Kauli hiyo ilitolewa Mjini Dodoma jana ,na Katibu wa Fedha na Uchumi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma, Haidery Gulamali wakati akichukua fomu ya kugombea ujumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicho ngazi ya taifa.
Gulamali alisema ipo tabia imejengeka kuwa ufisadi upo ndani yaCCM pekee jambo ambalo sio la kweli na kuwa ufisadi ni hulka ya mtu binafsi.
Kwa kuwa CCM ndicho chama kinachotawala na ndicho chenye wanachama wengi nchini,ufisadi lazima uonekane pamoja na kwamba hata katika vyama vya upinzani upo, alisema.
Gulamali alimpongeza Rais Jakaya Kikwete na uongozi wa Chama hicho kwa uamuzi wa kuwaondoa wabunge na wafanyakazi wengine wa Serikali katika uongozi ndani ya chama kwa kuwa kufanya hivyo chama kitaweza kuisimamia Serikali vizuri ikiwemo kupambana na ufisadi.
Alisema ameamua kugombea nafasi hiyo kwa sababu anatimiza wajibu wake kama mwanachama wa kushika nafasi mbalimbali za uongozi kuwakilisha watanzania.
Naye mwandishi wetu kutoka mkoani Mara anaripoti kuwa wana CCM watakiwa kukubaliana na matokeo ya uchaguzi kama njia ya kuimarika kwa demokrasia ndani ya chama hicho.
Kauli hiyo imetolewa na Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa (NEC) kutoka Mkoa wa Mara Vedastus Mathayo, ambapo alisema njia ya kukubali matokeo ya uchaguzi itaepusha kuepusha makundi ambayo yanaweza kujitokeza na kuibua malumbano yasiyo na msingi.
Kauli hiyo aliitoa hii jana, alipokuwa akifungua mkutano mkuu wa uchaguzi wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM Musoma Mjini (UWT) katika ukumbi wa mikutano wa CCM katika Makao makuu ya chama hicho Mjini Musoma.
Alisema mwanachama yeyote anapoingia katika kinyang'anyiro cha uchaguzi ni budi kukubaliana matokeo ya namna mbili kushinda na kushindwa na kuacha kujiingiza katika makundi ya kutafuta mchawi mara baada ya uchaguzi.
Katika hatua nyingine Mjumbe huyo wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa (NEC) Vedastus Mathayo alichukua fomu ya kutetea nafasi yake katika Ofisi ya CCM Musoma Mjini na kusema kila Mwanachama wa Chama hicho anayo haki ya kuomba nafasi yeyote ya uongozi ndani ya Chama.
Habari hii imeandikwa Na John Maduhu na Christopher Gamaina, Mwanza, Debora Sanja, Dodoma na Shomari Binda, Musoma.
KINDUMBWENDUMBWE cha kuwania nafasi ya uongozi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimezidi kushika kasi huku baadhi ya wagombea wakiweka wazi mikakati yao.
Hata hivyo mchuano mkali ukitarajiwa kuwa kati ya Mwenyekiti wa sasa anayemaliza muda wake Clement Mabina na aliyekuwa Mbunge wa Ilemela (CCM), Antony Diallo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana baada ya kurejesha fomu ya kuwania nafasi ya Uenyekiti Mkoa wa Mwanza, Dk. Antony Diallo, alisema endapo atafanikiwa kuwa Mwenyekiti wa chama hicho atapiga marufuku matumizi ya magari ya chama kutumika kwa shughuli binafsi.
Alisema hatua hiyo itakuwa ni njia ya kukipunguzia chama gharama za uendeshaji.
Diallo, ambaye pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), anayemaliza muda wake alisema kuna baadhi ya viongozi wamekuwa wakitumia mali za chama yakiwemo magari kwa ajili ya shughuli binafsi badala ya magari hayo kutumika kukiimarisha chama.
"Kama wewe ni Mwenyekiti gari hilo linapashwa kukuchukua siku ya vikao rasmi na shughuli rasmi, Mwenyekiti wa chama sio Mwenyekiti mtendaji gari la nini unataka ukae nalo na ulitumie kwa shughuli zako binafsi,huku ni kunibebesha chama mzigo wa gharama.
Chama kinahitaji mtu ambaye atakiongoza kama taasisi na sio kama mali yake binafsi,pia inahitajika mtu ambaye atawaunganisha wanachama na sio kuwagawa na mtu huyo ni mimi Dk Diallo, alisema.
Katika hatua nyingine Katibu wa ccm wilaya ya Nyamagana Deogratius Rutta amekwaa kisiki baada ya kuangushwa vibaya katika kuwnaia nafasi ya ujumbe wa mkutano mkuu wa ccm taifa kupitia nafasi tatu za wazazi.
Katibu huyo aliibuka na kura 71 ambapo washindi watatu waliopatikana ni Samson Ntambi, Raphael Shilatu pamoja na Emanuel Nzungu.
Dk. Kigwangalla: Uongozi siyo mvi
Kwa upande wake mbunge wa Nzega mkoani Tabora, Dk. Hamisi Kigwangalla (CCM), amesema uongozi unahitaji uwezo na hekima ya mtu na siyo kigezo cha umri mkubwa.
Dk. Kigwangalla ambaye amejitosa kuwania nafasi ya Uenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), ALISEMA ana uwezo wa kuiongoza Jumuiya hiyo ambayo hivi sasa ina taswira ya watu waliokula chumvi.
Uongozi siyo mvi, bali ni jambo linalohitaji uwezo na hekima ya mtu bila kujali umri wake wa uzee au ujana, alisisitiza Dk. Kigwangalla ambaye ni kijana mwenye umri wa miaka 37.
Alikuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ya CCM Mkoa wa Mwanza, mara baada ya kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa na CCM kugombea nafasi ya uenyekiti wa Jumuiya hiyo ngazi ya Taifa.
Wakati hayo yakiendelea Watanzania wametakiwa kuelewa kuwa ufisadi haupo ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) peke yake bali hata katika vyama vya Upinzani pio.
Kauli hiyo ilitolewa Mjini Dodoma jana ,na Katibu wa Fedha na Uchumi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma, Haidery Gulamali wakati akichukua fomu ya kugombea ujumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicho ngazi ya taifa.
Gulamali alisema ipo tabia imejengeka kuwa ufisadi upo ndani yaCCM pekee jambo ambalo sio la kweli na kuwa ufisadi ni hulka ya mtu binafsi.
Kwa kuwa CCM ndicho chama kinachotawala na ndicho chenye wanachama wengi nchini,ufisadi lazima uonekane pamoja na kwamba hata katika vyama vya upinzani upo, alisema.
Gulamali alimpongeza Rais Jakaya Kikwete na uongozi wa Chama hicho kwa uamuzi wa kuwaondoa wabunge na wafanyakazi wengine wa Serikali katika uongozi ndani ya chama kwa kuwa kufanya hivyo chama kitaweza kuisimamia Serikali vizuri ikiwemo kupambana na ufisadi.
Alisema ameamua kugombea nafasi hiyo kwa sababu anatimiza wajibu wake kama mwanachama wa kushika nafasi mbalimbali za uongozi kuwakilisha watanzania.
Naye mwandishi wetu kutoka mkoani Mara anaripoti kuwa wana CCM watakiwa kukubaliana na matokeo ya uchaguzi kama njia ya kuimarika kwa demokrasia ndani ya chama hicho.
Kauli hiyo imetolewa na Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa (NEC) kutoka Mkoa wa Mara Vedastus Mathayo, ambapo alisema njia ya kukubali matokeo ya uchaguzi itaepusha kuepusha makundi ambayo yanaweza kujitokeza na kuibua malumbano yasiyo na msingi.
Kauli hiyo aliitoa hii jana, alipokuwa akifungua mkutano mkuu wa uchaguzi wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM Musoma Mjini (UWT) katika ukumbi wa mikutano wa CCM katika Makao makuu ya chama hicho Mjini Musoma.
Alisema mwanachama yeyote anapoingia katika kinyang'anyiro cha uchaguzi ni budi kukubaliana matokeo ya namna mbili kushinda na kushindwa na kuacha kujiingiza katika makundi ya kutafuta mchawi mara baada ya uchaguzi.
Katika hatua nyingine Mjumbe huyo wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa (NEC) Vedastus Mathayo alichukua fomu ya kutetea nafasi yake katika Ofisi ya CCM Musoma Mjini na kusema kila Mwanachama wa Chama hicho anayo haki ya kuomba nafasi yeyote ya uongozi ndani ya Chama.
Habari hii imeandikwa Na John Maduhu na Christopher Gamaina, Mwanza, Debora Sanja, Dodoma na Shomari Binda, Musoma.