Dhana ya USALITI ndani ya CHADEMA na Hatma ya Demokrasia ndani ya vyama vya Siasa

Mbogela

JF-Expert Member
Jan 28, 2008
1,384
257
Kwa kifupi ningependa nitoe wosia kwa vyama vya SIASA hasa vyama vya Upinzani na hasa CHADEMA.

Imetokea kasumba ambayo imekuwa inakuwa kwa kasi ya ajabu ndani ya vyama vya upinzani. Ndani ya vyama vya upinzani umetokea upepo wa kutokuaminiana, kumetokea wimbi kubwa la kutuhumiana USALITI miongoni mwa wanachama. Mtu akionekana kuwa amekuwa na mawazo tofauti na wenzake hata anapokuwa tofauti na kundi dogo tu ndani ya Chama au na kiongozi mmoja tu ataitwa msaliti na kundi la upande wa pili. Wakati mwingine hata utofauti wa Hoja humfanya mwanachama mmoja aitwe msaliti.

Mtiririko wa matukio ya kuitana wasaliti ndani ya CHADEMA nilianza kuyasikia uchaguzi wa BAVICHA, baadaye tukayasikia akituhumiwa mheshimiwa Shibuda, yakaenda kwa Mh. Zitto Kabwe, yakamaliza na kuwachinjia baharini akina Mtela Mwampamba na Juliana Shonza na kundi lake,

Historia inanikumbusha ni suala la tuhuma za Usaliti zilizoisambaratisha NCCR- Mageuzi, chama kilichokuwa maarufu miaka yetu ya 90. Kundi la Mrema liliwatuhumu kundi la Mabere Marando kuwa ni wasaliti na Kundi la Mabere Marando lilimtuhumu Augustino Mrema na kundi lake kuwa wanatumiwa na CCM na Serikali. Kutokana na tuhuma hizo, viongozi na wanachama wa kila kundi wakawa busy na kupanga mashambulizi dhidi ya kundi lingine kila kukicha. Hatima yake ni kurushiana viti na majaribio ya kutaka kuuana katika Hotel ya Mkonge huko Tanga na huo ukawa ndio mwanzo wa kifo cha NCCR-MAGEUZI.

Ninaona tatizo hili linainyemelea CHADEMA, tatizo hili linahitaji kutibiwa, CHADEMA inahitaji kujenga demokrasia ya kukosoana bila kuchukiana na kuhisiana vibaya. Wanachama wa CHADEMA wamekuwa waoga kutoa mawazo yatakayokinzana na wanachama wenzao na hasa viongozi fulani fulani kwa kuogopa kuitwa wasaliti.

Na kutokana na udhaifu huu ni rahisi sana adui kupenya. Kwa mfano katika mkanda wa video unaonyesha Lwakatare akipanga njama za kuteka, kushambulia na kudhuru mtu. Sababu inayotajwa kuandaliwa kwa mkakati huo ni Zitto Kabwe. Kuwa Mh. Lwakatare alikuwa anapanga njama za kigaidi dhidi ya mwandishi wa habari kwa kile kilichosemwa ukaribu wake na Zitto. Sasa unajiuliza shida iko wapi kuwa karibu na Zitto Kabwe, majibu katika video hiyo hiyo yanasema anadhofisha juhudi za chama, kwa kifupi ni msaliti.

Sijui kama video hiyo ya kweli au si ya kweli, na wala sihitaji kujua hilo, Lakini, Sababu ya hisia za USALITI ndio chanzo cha uwepo wa video hiyo. Sasa kama video hiyo ni ya kweli, basi utaona kuwa idara nzima ya ulinzi na usalama chini ya Lwakatare ilivyopoteza dira, Badala ya kushughulikia ulinzi na usalama wa chama kutoka kwa maadui wa kweli imejikita kwenye hofu hofu ya kusalitiwa. Kama hiyo video sio ya kweli utaona kuwa maadui wametumia kuwepo kwa hali ya kutokuaminiana ndani ya CHADEMA na hivyo imewezekana kutengeneza video hiyo kwasababu ya mwanya uliotengenezwa na CHADEMA yenyewe, mwanya wa hisia za usaliti.

Sasa hivi ndani ya CHADEMA ili uonekane wewe ni mwanaharakati wa kisiasa wa kweli, na mpenzi wa CHADEMA wa kweli ni lazima uongelee watu wanaohujumu jitihada za chama, lazima uzungumzie watu unaodhani hawako upande wenu. Sasa wanachama wa CHADEMA hawazungumzii tena Itikadi ya chama, Hawazungumzi tena hoja za mipango mikakati ya chama inayohusiana na maendeleo ya kijamii, kisiasa na kiuchumi, watu wako busy na nani anatuangusha wapi na kwa vipi na wasababu zipi.

Sasa badala ya kuwa kwenye mapambano dhidi ya mpinzani wa CHADEMA anayefahamika CCM mapambano yamebadirishwa na kuwa ni mapambano kati ya kundi moja la CHADEMA dhidi ya kundi lingine la CHADEMA, hii ni HATARI sio tu kwa CHADEMA yenyewe bali hata kwa ustawi wa Demokrasia ya nchi yetu na Afrika kwa ujumla.

Niwasihi viongozi wa ngazi ya juu wa CHADEMA warudishe ajenda muhimu kwenye meza za mazungumzo za wanachama wao, kufanya juhudi za makusudi za kuondoa hisia za hujuma na usaliti na kuwafanya wanachama wajione wao ni kitu kimoja, wenye nia na lengo moja wanaoenda njia moja.
 
CCM ndio wanaojaribu kuonyesha ndani ya CHADEMA kuna usaliti lakiniukwel ni kwamba ndani ya CHADEMA hakuna usaliti
 
tatizo la chadema ni kuwa hakuna mawazo huru. padre anaongoza kama yuko madhabahuni, hamna kuhojiwa. na kila mmoja anatakiwa akatubu dhambi zake. sasa fikiria kiyo hali na wengine wamezoea kutubu moja kwa moja kwa muumba wa vyote akiwemo padre.
Ni sawa na kumshangaa baba yako kuendelea kuomba nyumba kwa mama yako wakati alimtolea mahari na amesha shiriki maisha yake nawewe mara nyingi kiasi kwamba tangu uzaliwe hujaona kama wao sio ndugu.tehetehe
 
Usaliti unatoka nje ya chadema, watu hawataki kusoma historia, usaliti uko Ccm wanatumia njaa za watu ninachoshukuru sasa CDM wanaanza kutambua. CDM ni dhahabu kwa waTz na sasa inapitishwa kwenye moto ikitoka humo tayari kwa kushika dola 2015
 
Mkuu Mbogela nakupongeza sana kwa mada yako, umepangilia vizuri mtiririko wa hoja, hukuonesha ushabiki wa chama chochote bali umesukumwa na uzalendo halisi wa nchi yako. Yeyote anayependa mabadiriko yenye tija kwa taifa letu atakuelewa sababu kwa sasa chama kilicho na nguvu na kuaminika kuwa mbadala wa CCM ni CDM lakini baadhi ya viongozi na washabiki wao hawapendi kupokea mawazo huru yasio na muelekeo wa kishabiki kama yako. Mtazamo huu usipobadilika lengo la mabadiliko halitatimia.
 
Ni ushauri mzur hakika.
Ila cdm hakuna usaliti,maneno ya usaliti yanaletwa na magamba wanaoigiza ucdm.
Mf:mh.zzk ni mzalendo sana na cdm,ni mtu muelewa sana,mvumilivu,mwenye hekima na mwenyekujitambua.
Alisha apa kutong'oka cdm.
Na anatambua athar za usaliti.
KWA KIFUPI NIKWAMBA MAGAMBA WAJUE KUWA CDM HAKUNA MAKUNDI KAMA WALIYONAYO WAO. Wanayo takribani ma3,na yanazidi kuongezeka.
CDM CHAMA.
 
Kwani ni kwanini NDANI ya CCM Wanamfanyia MIZENGWE Edward Lowassa? na NDIE aliyefanya CAMPAIGN ya hali ya JUU kuwezesha KIKWETE kuwa RAIS wa Jamhuri; Sasa kwani kwa CCM hiyo sio USALITI ndani ya CHAMA?
 
Katika post yako yote I pick the third paragraph from the bottom; hiyo ndio mwiba kwa CHADEMA NA itawaangamiza kisiasa. Wanashabikia kumtukuza padri wao na kuamini kila asemalo na atakalo bila ya kuwa "objective"... Hii ni sherehe kwa CCM manake ndio anguko la CDM linaanzia hapo. Badala ya kujenga chama in a forward-looking manner wanakaa kuendeleza uhasama wa makundi [dealing with the alleged dissidents] na kuwasulubu watu on the basis of who supports who! Viva CCM. IKULU MTAISIKIA REDIONI.ENDELEENI KUANDAAMANA NA KUPANGA MIKAKATI YA KUTEKA WATU.
 
tatizo la chadema ni kuwa hakuna mawazo huru. padre anaongoza kama yuko madhabahuni, hamna kuhojiwa. na kila mmoja anatakiwa akatubu dhambi zake. sasa fikiria kiyo hali na wengine wamezoea kutubu moja kwa moja kwa muumba wa vyote akiwemo padre.

na wewe great thinker?

jenga hoja ueleweke vizuri
 
Mtazamo wangu ni kuwa CDM inakaribia kuushinda usaliti ndio maana unaona watu wanafumaniwa kabla mipango yao haijafika mwisho. Katika historia ya huko nyuma vyama vilikuwa vinakufa ndo inakuja kujulikana ilikuwa ni usaliti. Lakini kwa CDM kuwepo hai hadi sasa ni kuwa usaliti unawahi kugunduliwa.
Jambo la pili nashangaa sana watu wenye hoja ya upande wa pili wanamuattack sana Dr. Slaa, najiuliza why?? Kwanini yeye personally?? Kuna hadi mtu anajaribu kumvika madaraka ya uenyekiti na kutaka kuonyesha upungufu wake ktk uongozi wakati sio mwenyekiti. Ni ukweli usiopingika kuwa Dr.Slaa ni mwiba sana kwa CCM na hii ni kutokana na uwezo wake mkubwa kiakili, kihoja, kwa kujiamini, kimsamo na tunu nyingine ambazo viongozi wengi hawana.
Yanayoendelea sasa hivi CDM ni njia ya kukikomaza chama na ikumbukwe kuwa ili dhahabu iwe nzuri sharti ipite kwenye moto mkali.......ili CDM kiwe chama imara lazima kipite na kushinda misukosuko ya namna hii.
 
CDMA kushika dola 2015?
Ni ishara gani zinazoonyesha hivyo?
Mbona chadema haijakubalika Kama ilivyowahi kukubalika nccr mageuzi ,Na haikushika dola?
Watanzania tunaendelea kufuatilia Kwa makini matumizi mabaya mno ya madaraka Na Mali ndani ya chama , wanachama wanafukuzwa kibabe Na kuondokewa kwenye uongozi bila kufuata taratibu, eti Ni wasaliti Kwa vile wamehoji matumizi ya pesa Za ruzuku zinazotolewa Na serekali kila mwezi!
 
Kwani ni kwanini NDANI ya CCM Wanamfanyia MIZENGWE Edward Lowassa? na NDIE aliyefanya CAMPAIGN ya hali ya JUU kuwezesha KIKWETE kuwa RAIS wa Jamhuri; Sasa kwani kwa CCM hiyo sio USALITI ndani ya CHAMA?

Ni kweli kuwa inawezekana ndani ya CCM Lowassa akaonekana ametengwa au anafanyiwa fitina, Lakini huwezi kusikia kuna wanachama wa CCM wanakaa chini kupanga mikakati ya kummaliza Lowassa, huwezi kusikia wana CCM wamekaa chini kuwamaliza marafiki wa Lowassa, na kutokana na hilo hata CHADEMA haina uwezo wa kupandikiza mbegu ya Chuki kwa wanaCCM dhidi ya Lowassa, Unajua kwanini? kwasababu CCM wenyewe linapokuja suala la wao kwa wao hawatoi mwanya wa mtu wa nje ku-dictate terms. Tofauti na CHADEMA, ikitokea leo mwana CCM akasimama akasema kuwa John Mnyika alionekana anakula lunch na Nnape huko Iringa, CHADEMA wote wanainua kuomba maelezo kwa Mnyika kwanini ulionekana aunakula na Nnape, ikisika leo kuwa kuwa Nasari anataka kumuoa Mtoto wa Aden Rage au wa Rostam Aziz, hilo litakuwa ni kosa mbele ya wanachama wa CHADEMA na watataka Nasari apokonywe kadi ya CHADEMA mara moja. Na hili ndio tatizo kubwa ndani ya CHADEMA kwa sasa. Vijana ahawataki kusikia mtu yeyeto yupo karibu na wanaCCM ahata kama ni ndugu zake.
 
CCM ndio wanaojaribu kuonyesha ndani ya CHADEMA kuna usaliti lakiniukwel ni kwamba ndani ya CHADEMA hakuna usaliti
Kutokana na kosa moja la kuiacha Ajenda ya Usaliti iabaki inaelea elea hewani ndani ya CHADEMA, Matokeo yake ndio kesi ya Lwakatare, na haya ni matokeo ya kati, kuna matokeo ya mwisho, matokeo ya mwisho yanatokana na kesi hii kuwa input ya kuzalisha matokeo hayo.
1. Sasa hivi CHADEMA makao makuu imeshadivert attention yake kwenda kwenye kesi ya Lwakatare, utaona matumizi ya Rasilimali nyingi kama Muda, Pesa, watu (Mawakili 5 plus watendaji) viatelekezwa kwenye kesi hii.
2.Mwaka huu CHADEMA inauchaguzi wa ndani, hakuna kiongozi atakayeupa uchaguzi huo asilimia 100 ya attention, they will have to split their attention kwenye kesi na uchaguzi,Matokeo yake tutapata viongozi wabovu au wasio sahihi,
3. Mwakani tuna uchaguzi wa serikali za Mitaa, viongzi wetu badala ya kuwa busy kuandaa na kusimamia mikakati watakuwa busy na kesi hii, matokeo yake kushindwa uchaguzi wa serikali za mitaa.

4. Kubwa zaidi matokeo ya kesi hii, ikithibitishwa kuwa video ile ni ya Lwakatare, na pia maneno yake ni kosa la jinai na jinai hiyo inaangukia katika makosa ya kesi za KIGAIDI, Je matokeo hayo yatakuwa na impact gani kwenye image ya CHADEMA kwenye public? Pia kumbuka kesi hii inaweza ikatupelekea mpaka around 2015 ndio iaamuliwe.
 
Ni kweli kuwa inawezekana ndani ya CCM Lowassa akaonekana ametengwa au anafanyiwa fitina, Lakini huwezi kusikia kuna wanachama wa CCM wanakaa chini kupanga mikakati ya kummaliza Lowassa, huwezi kusikia wana CCM wamekaa chini kuwamaliza marafiki wa Lowassa, na kutokana na hilo hata CHADEMA haina uwezo wa kupandikiza mbegu ya Chuki kwa wanaCCM dhidi ya Lowassa, Unajua kwanini? kwasababu CCM wenyewe linapokuja suala la wao kwa wao hawatoi mwanya wa mtu wa nje ku-dictate terms. Tofauti na CHADEMA, ikitokea leo mwana CCM akasimama akasema kuwa John Mnyika alionekana anakula lunch na Nnape huko Iringa, CHADEMA wote wanainua kuomba maelezo kwa Mnyika kwanini ulionekana aunakula na Nnape, ikisika leo kuwa kuwa Nasari anataka kumuoa Mtoto wa Aden Rage au wa Rostam Aziz, hilo litakuwa ni kosa mbele ya wanachama wa CHADEMA na watataka Nasari apokonywe kadi ya CHADEMA mara moja. Na hili ndio tatizo kubwa ndani ya CHADEMA kwa sasa. Vijana ahawataki kusikia mtu yeyeto yupo karibu na wanaCCM ahata kama ni ndugu zake.

Kwani IMEWAHI kutokea HIVYO au unazungumzia NDOTO za ALINACHA? ni kweli MNYIKA alikula chakula na NAPE na wakataka MAELEZO? Ndieo huyo huyo NAPE na PRINCE RIZ1 walio-question elimu ya MNYIKA? hata hivyo MNYIKA na NNAPE walisha kaa pamoja na kupigwa picha PAMOJA na Hakuna Maswali? Angalia Picha CHINI...

Uliufuatilia MKUTANO MKUU wa CCM; Kulikuwa kuna kuhongana na kuhakikisha watu wanaomkubali LOWASSA wasichaguliwe... Angalia kweli Neema ya KIKWETE baada ya LOWASSA kumfanyika CAMPAIGN toka 1995 ili awe RAIS ndio MALIPO anayoyapata? Kufukuzwa CC ya CCM; PRINCE RIZ1 kusema ataandika KITABU kuhusu VITENDO BABA yake alivyofanyiwa na RAFIKI zake NDANI ya CCM... HAUONI ni kwasababu kiko MADARAKANI ndio Maana HAUSIKII UNYAMA wao LAZIMA ULE au UTAKUFA ... so u have to KISS SOME... to SURVIVE!!!! CCM is the CAUSE....

images
 
thread hii imekwenda shule!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! tatizo la mashabiki wa chdm ni kwamba huwa hawapendi ushauri kama huu. wanataka wasikie ukimsifu slaa na mbowe. hapo watakupa tano.

chdm fuateni ushauri wa thread hii. kubalini kuwa ndani ya chama kunafuka moshi
 
thread hii imekwenda shule!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! tatizo la mashabiki wa chdm ni kwamba huwa hawapendi ushauri kama huu. wanataka wasikie ukimsifu slaa na mbowe. hapo watakupa tano.

chdm fuateni ushauri wa thread hii. kubalini kuwa ndani ya chama kunafuka moshi

Hahahahahahaa....

Mmeshaondolewa kwenye hoja ya msingi ya wanafunzi kufeli kwa 94% na issue ya kuteswa Kibanda kwa style ya Ulimboka,sasa mpo busy na movie la kichina la CHADEMA na usaliti.

Watanzania ndivyo tulivyo, na mwakani watafeli 98% labda wagawiwe marks kama tende wakati wa mfungo wa Ramadhani.
 
Back
Top Bottom