Dhana ya kulinda viwanda vya ndani ni potofu

JERUSALEMU

JF-Expert Member
Sep 19, 2012
3,114
3,541
Salamu wanajamvi!

Tatizo la nchi yetu kiuchumi ni kubwa kuliko wengi wetu tunavyo dhani.Uchumi wa nchi yetu kila wakati unakutana na dhoruba kali labda kwasababu wachumi wetu mahali fulani wanakosea kufikiri vizuri.

Hivi unawezaje kupanga bei elekezi ya bidhaa fulani bila kujiridhisha kwa hakika kama uzalishaji na upatikanaji wa bidhaa husika sokoni uko vizuri?Leo hii bei ya sukari katika baadhi ya maeneo imefika tshs 3000/ kwa kilo moja yaani shs 1200 zaidi ya bei elekezi.

Kulinda viwanda vya ndani wakati uzalishaji wake wa bidhaa ni hafifu ni kurudisha nyuma maendeleo.Wazo hili linatoka wapi? mbona viwanda vingine vya ndani havilidwi dhidi ya bidhaa kutoka nje?Viwanda vya sabuni, mafuta ya kupikia, viwanda vya nguo nk mbona viliachwa kupambana na nguvu ya soko bila kulindwa na serikali? Inakuwaje leo serikali inaturudisha nyuma kewa kisingizio cha kulinda viwanda vya ndani?

Marekani ina viwanda vya kila aina ya bidhaa lakini hawajawahi kuzuia bidhaa zenye ubora unao hitajika kuingia ndani ya marekani kwa kisingizio cha kulinda viwanda vya ndani.Nchi yeyu inapakana na nchi nyingi zinazo zalisha sukari na kama wafanya biashara wangeruhusiwa kuingiza bidhaa hii kutoka katika nchi hizi nauhakika bei ya sukari ingekuwa shs 1200 tu.
 
Elimu bora ni ile inayomfanya msomi kupambana na mazingira anayoishi ili ayaboreshe kutoka hali duni - Kwa mtazamo huu wanaojiita wasomi kwa sekta ya uchumi hawakupata elimu iliyo bora, walisoma hili waweze kupata maksi za juu kwenye mtihani wao wa mwisho.

Wale walosoma na kuelewa wakijaribu kutoa ushauri wanadharauliwa .....wapo wengi lakini hawana nafasi kwenye serikali ya mafisadi.
 
Salamu wanajamvi!

Tatizo la nchi yetu kiuchumi ni kubwa kuliko wengi wetu tunavyo dhani.Uchumi wa nchi yetu kila wakati unakutana na dhoruba kali labda kwasababu wachumi wetu mahali fulani wanakosea kufikiri vizuri.

Hivi unawezaje kupanga bei elekezi ya bidhaa fulani bila kujiridhisha kwa hakika kama uzalishaji na upatikanaji wa bidhaa husika sokoni uko vizuri?Leo hii bei ya sukari katika baadhi ya maeneo imefika tshs 3000/ kwa kilo moja yaani shs 1200 zaidi ya bei elekezi.

Kulinda viwanda vya ndani wakati uzalishaji wake wa bidhaa ni hafifu ni kurudisha nyuma maendeleo.Wazo hili linatoka wapi? mbona viwanda vingine vya ndani havilidwi dhidi ya bidhaa kutoka nje?Viwanda vya sabuni, mafuta ya kupikia, viwanda vya nguo nk mbona viliachwa kupambana na nguvu ya soko bila kulindwa na serikali? Inakuwaje leo serikali inaturudisha nyuma kewa kisingizio cha kulinda viwanda vya ndani?

Marekani ina viwanda vya kila aina ya bidhaa lakini hawajawahi kuzuia bidhaa zenye ubora unao hitajika kuingia ndani ya marekani kwa kisingizio cha kulinda viwanda vya ndani.Nchi yeyu inapakana na nchi nyingi zinazo zalisha sukari na kama wafanya biashara wangeruhusiwa kuingiza bidhaa hii kutoka katika nchi hizi nauhakika bei ya sukari ingekuwa shs 1200 tu.
Marekani hawazuii kuingiza bidhaa kama in ubora lakini zinalipiwa kodi stahiki. Tanzania uigizaji wa sukari ilikuwa dili la wateule fulani no walikuwa hawalipi kodi stahiki
 
Salamu wanajamvi!

Tatizo la nchi yetu kiuchumi ni kubwa kuliko wengi wetu tunavyo dhani.Uchumi wa nchi yetu kila wakati unakutana na dhoruba kali labda kwasababu wachumi wetu mahali fulani wanakosea kufikiri vizuri.

Hivi unawezaje kupanga bei elekezi ya bidhaa fulani bila kujiridhisha kwa hakika kama uzalishaji na upatikanaji wa bidhaa husika sokoni uko vizuri?Leo hii bei ya sukari katika baadhi ya maeneo imefika tshs 3000/ kwa kilo moja yaani shs 1200 zaidi ya bei elekezi.

Kulinda viwanda vya ndani wakati uzalishaji wake wa bidhaa ni hafifu ni kurudisha nyuma maendeleo.Wazo hili linatoka wapi? mbona viwanda vingine vya ndani havilidwi dhidi ya bidhaa kutoka nje?Viwanda vya sabuni, mafuta ya kupikia, viwanda vya nguo nk mbona viliachwa kupambana na nguvu ya soko bila kulindwa na serikali? Inakuwaje leo serikali inaturudisha nyuma kewa kisingizio cha kulinda viwanda vya ndani?

Marekani ina viwanda vya kila aina ya bidhaa lakini hawajawahi kuzuia bidhaa zenye ubora unao hitajika kuingia ndani ya marekani kwa kisingizio cha kulinda viwanda vya ndani.Nchi yeyu inapakana na nchi nyingi zinazo zalisha sukari na kama wafanya biashara wangeruhusiwa kuingiza bidhaa hii kutoka katika nchi hizi nauhakika bei ya sukari ingekuwa shs 1200 tu.
Siasa kwenye utaalamu ni shida
Salamu wanajamvi!

Tatizo la nchi yetu kiuchumi ni kubwa kuliko wengi wetu tunavyo dhani.Uchumi wa nchi yetu kila wakati unakutana na dhoruba kali labda kwasababu wachumi wetu mahali fulani wanakosea kufikiri vizuri.

Hivi unawezaje kupanga bei elekezi ya bidhaa fulani bila kujiridhisha kwa hakika kama uzalishaji na upatikanaji wa bidhaa husika sokoni uko vizuri?Leo hii bei ya sukari katika baadhi ya maeneo imefika tshs 3000/ kwa kilo moja yaani shs 1200 zaidi ya bei elekezi.

Kulinda viwanda vya ndani wakati uzalishaji wake wa bidhaa ni hafifu ni kurudisha nyuma maendeleo.Wazo hili linatoka wapi? mbona viwanda vingine vya ndani havilidwi dhidi ya bidhaa kutoka nje?Viwanda vya sabuni, mafuta ya kupikia, viwanda vya nguo nk mbona viliachwa kupambana na nguvu ya soko bila kulindwa na serikali? Inakuwaje leo serikali inaturudisha nyuma kewa kisingizio cha kulinda viwanda vya ndani?

Marekani ina viwanda vya kila aina ya bidhaa lakini hawajawahi kuzuia bidhaa zenye ubora unao hitajika kuingia ndani ya marekani kwa kisingizio cha kulinda viwanda vya ndani.Nchi yeyu inapakana na nchi nyingi zinazo zalisha sukari na kama wafanya biashara wangeruhusiwa kuingiza bidhaa hii kutoka katika nchi hizi nauhakika bei ya sukari ingekuwa shs 1200 tu.
Siasa kwenye utaalamu ni shida
 
Wanalinda viwanda vya ndani vya sukari,
kwanini wasilinde na vya mafuta ya kujipaka,au ya kupikia ili viwanda vyetu vya samli na mafuta ya pamba vinyanyuke?
 
Wanalinda viwanda vya ndani vya sukari,
kwanini wasilinde na vya mafuta ya kujipaka,au ya kupikia ili viwanda vyetu vya samli na mafuta ya pamba vinyanyuke?
ukisikia double standard ndio hiyo.Wanasema wanalinda viwanda vya ndani mbona ni sukari tu? mbona hatusikii wakiwazuia walimu na wataalamu wengine kuja kufanya kazi Tanzania kwa kisingizio cha kulinda wahitimu wa ndani?
 
  • Thanks
Reactions: 999
Kupanga bei na kuzuia bidhaa ya nje, pamoja na kuzuia export ni ubwege hata kama viwanda vya ndani vinazalisha bidhaa nyingi kiasi gani.
 
Ila tusilaumu sana wasomi wetu wakuu,ni kweli huwa kuna mahali wanachemka ila pia tusisahau kuwa mara nyingi maushauri yao hayasikilizwi, hasa linapokuja suala la kutaka sifa kwenye siasa au mwanasiasa fulani anapoona huo ushauri unamuweka mbali na ulaji...........kama hili la sukari naamini kabisa sifa za kisiasa ndio zimetufikisha hapa.
 
hivi viwanda vikizidi kulindwa havitaona umuhimu wa kuwekeza kwenye teknolojia mpya ambayo hupunguza gharama za uzalishaji na kuongeza ubora. sukari ya brazil ni cheap kuliko ya kilombero sababu ya teknolojia. hakuna maendeleo kama hakuna ushindani.
 
Elimu bora ni ile inayomfanya msomi kupambana na mazingira anayoishi ili ayaboreshe kutoka hali duni - Kwa mtazamo huu wanaojiita wasomi kwa sekta ya uchumi hawakupata elimu iliyo bora, walisoma hili waweze kupata maksi za juu kwenye mtihani wao wa mwisho.

Wale walosoma na kuelewa wakijaribu kutoa ushauri wanadharauliwa .....wapo wengi lakini hawana nafasi kwenye serikali ya mafisadi.
sina la kuongeza hapa.
 
Marekani hawazuii kuingiza bidhaa kama in ubora lakini zinalipiwa kodi stahiki. Tanzania uigizaji wa sukari ilikuwa dili la wateule fulani no walikuwa hawalipi kodi stahiki
Kwa hiyo kuzuia sukari isiingie nchini ndo kunafanya kodi ikusanywe vizuri?
 
Huu ni upumbavu Na akili ndogo Za viongozi wetu, hata Kama inahitaji mabadiliko ya viwanda hayawezi kupatikana kwa miezi Sita, Nchi inaingizwa umasikini wa hiyari? Kama kuna suala la kulinda kwanini uzuie baadhi ya bidhaa tuu?

Magu anaharaka sana ya mabadiliko bila ya kutathimini ni kiasi gani uwezo wetu wa uzalishaji wa bidhaa hizo. Tukijipanga vizuri tutafika taratibu.
 
Back
Top Bottom