Dhana ya elimu

Shayu

Platinum Member
May 24, 2011
608
1,653
Leo ningependa tujiulize wote kwa pamoja ni nini haswa maana ya elimu ? Tujiulize, tutafakari, tujaribu kupata majibu, ni nini haswa maana ya elimu? Na kwanini watu wanapelekwa shule ? Na kwanini tunaamua kupeleka shule watoto wetu? Na ni kwanini taifa hupeleka watu wake shule.



Ni nini maana ya elimu?



pengine tunaweza kufikiri elimu ni maarifa kazi peke yake ambayo yatatupatia kipato. Lakini elimu ni zaidi ya hapo tulipozoea. Ya kwamba tunaenda shule kusudi tupate kazi kusudi tupate pesa kwaajili ya matumizi yetu ya kila siku.

Elimu ni ukuzaji wa ufahamu za binadamu (enlightment ). Ukuzaji wa ufahamu huu ambao unapaswa kumpelekea binadamu na kumfanya binadamu kutenda katika usahihi , ili kumfanya binadamu awe binadamu bora zaidi na mwenye kuzalisha na mwenye faida kwake binafsi kwa taifa lake na kwa familia yake.


Aweze kuangalia familia vizuri na ku manage familia yake vizuri. awe na mahusiano mazuri na jamii inayomzunguka na awe pia na mahusiano mazuri na taifa lake na aweze kuwa mtu bora na mzalishaji kwa taifa lake. Ndio msingi wa elimu.

Elimu sio skills za kazi peke yake. Lakini ukaacha mambo mengine ya msingi anbayo ni kukuza ufahamu wa binadamu ( Elinlightment) ya akili ya binadamu. Ili aweze ku act katika usahihi.


Aweze awe na uwezo wa kuchanganua kati ya sahihi na potofu na aweze kufuata jambo ambalo ni sahihi. Mtu huyu ni mtu ambaye mwenye elimu. Mwenye uwezo wa kufahamu na kuchanganua mambo na kutenda katika usahihi.

Mwenye uwezo wa ku manage familia yake vizuri, mwenye uwezo wa kuwa na mahusiano mazuri na jamii inayomzunguka, mwenye uwezo wa kuwa raia bora na mtu bora ambaye anazalisha katika taifa lake.


Hatuwezi kuwapa watu elimu bila kuangalia tabia za watu wetu. Ni muhimu elimu yetu pamoja na kuangalia skills za kazi za watu wetu lakini ijenge tabia zao. Ili ziwe na manufaa kwa taifa sio hasara. Kama tunawapa skills za kazi watu wetu lakini wanakuwa hawana manufaa kwa taifa letu basi hiyo elimu ina kasoro iangaliwe upya.



Elimu bora ni ile inayomfanya mtu kutenda katika usahihi. Ni elimu ambayo sisi kama taifa tunapaswa kuijenga. Na watoto wetu watakuwa wenye akili kama wakipata elimu kama hiyo. Ni elimu ambayo itawalinda dhidi ya maangamizi, itawalinda dhidi ya uovu.. Lakini pia itawapa skills za kazi.



Kwahiyo tukitengeneza watu kama hao tutapata viongozi wazuri, tutapata watu wenye skills mbalimbali wazuri lakini pia waaminifu na wenye maadili na nidhamu ya kutosha.


Vinginevyo elimu ambayo unampa tu mtu skills za kazi pasipo mambo mengine yaliyojazia hapo ni sawasawa na kutwanga maji kwenye kinu. Elimu bila maadili ni sawasawa na mtu bila kingo. Haitokuwa na faida. Itakufa tu.



Maana ya elimu ni kuondokana na matendo ya kijinga yasiyo na faida. Dhana ya elimu ni kuondokana na ujinga. Na tunapima faida ya kitu kutokana na matokeo ya kila matendo tunayofanya. Ili twende mbele kama taifa lazima tuelimike. Tuachane na ujinga na tutende katika usahihi.

Kwahiyo ni uhimu sana tunapowapa skills za kazi na tunapotoa elimu kuangalia tabia na dihamu za watu wetu. Nidhamu huleta mwelekeo iwe kwa taifa au kwa mtu binafsi.
 


Ni jambo jema lakini ni vizuri tukajiuiza tunahitaji elimu ya aina gani?

Maana kama hatutalielewa hili kwanza ni dhahiri tutaishia kupingana na mipango ya kitaifa ama kukinzana kimahitaji na uwepo wa fursastahiki katika lile tunalolichuchumilia



Mahitaji ya elimu ni mengi na aina a elimu pia ni nyingi mfan

  1. Maendeleo katika mapinduzi ya kiteknojia (Advance Technology)
  2. Sayani ya uchumi
  3. Tafitiza kisayansi
  4. Maendeleoya teknolojia katika masuala ya kiulinzi
  5. Sayansiya biashara
  6. SayansiTiba
  7. Sayansiya michezo
  8. Ueledi na ujuzi (uhandisi, mipango, masuala ya kijamii n.k)
  9. Sayansi ya sanaa na Michezo
Katika hayo niliyoyataja hapo juu, siyo yote ni mambo yanayoweza kusimama kila moja kwa upekee wake,yapo mambo ambayo yanategemeana lakini inapokuja dhana ya kimaendeleo ni lazimakuna mambo ambayo yatasimama kama yenyewe (core values), mfano, Kilimo, Tafiti zakisayansi, Sayansi ya tiba, mapinduzi ya kiteknolojia (teknohama), Uchumi namengineyo.


Ni vizuri pia kutambua ili kufanikiwa katika jambo lolotehapo ju ni lazima kuwepo mipango thabiti, ni lazima kuwepo na utambuzi na upembuzi wa kinakwamba tunahitaji nini? ili tuelekee wapi?. Kimsing hapa ndipo inapokuwa dira yakitaifa. Na hapa ndipo taifa linapo feli.


Ndugu zangu ni lazima tutambue kuwa kila senti inayopatkanakatika taifa ina thamani kubwa sana hivyo kuitumia vizuri tena kwa mipangostahiki ndiyo tunu iliyotukuka, ni lazima iwepo mipango ambayo baada ya mudalazima itengeneze umbo la pembetatu sawa iliyotazama juu ili kilakinachofanyika chini kiweze kushabihiana na kingine hivyo kukaribiana katika kila hatuainayotekelezeka kuelekea juu.


Ninamaanisha hivi, mfano kama tunaamua kuwekeza katikakilimo, basi lazima tuwekeze pia katika viwanda vya dhana au embejeo za kilimo,madawa ya kilimo, wataalamu wa kilimo, viwanda vya ku-process mazao ya kilimon.k pengine ni lazima tuwekeze pia katika mifugo na ufugaji ili kile kinachozalishwakatika kilimo kama makapi basi tukitengeneze kifae katika mifugo ya kisasa. Hapautaona mipango inahitajika (intergration of events)


Kama tunaamua kuweeza katika Sayansi ya Tiba, ni lazimatuwekeze pia katika viwanda na sayansi y viwanda, tuwekez katika viwanda vya madawa ya binadamu, vifaa tiba, sayansi ya utafiti,biashara na miundo mbinu. Ni dhahiri tutahitaji pia wataalamu madaktari, manesina wataalamu wa kimaabara hivyo ninapozungumzia miundo mbinu utaona kunakazi yaziada, kuhakikisha kuwa kila linalofanyika lina mahusiano ya moja kwa moja


Hivyo basi tukirudi katika ajenda yetu ya msingi yaani "elimu"utaona kwamba siyo tu suala la kujenga shule za kata, wala kujenga maabara nchinzima inawezekana hicho kisiwe kitu tunachohitaji kwa sasa, ndio maana nasisitizakujitambua kama taifa tunahitaji nini ili tuelekee wapi. Sibezi juhudu zilizopolakini napingana kabisa na kukosekana kwa mipango anuai na dira ya taifa


Mambo haya yote yanahitaji uwekezaji, tena uwekezaji wa niaya dhati katika misingi endelevu. Mara baada ya yote jamii ijajikita katika Nyanjambalimbali kutegemeana na malengo, msukumo na fursa zitakazokuwepo kwa wakatihuo kutokana na kipi ndio kipaumbele cha kitaifa


Kinachoendelea sasa ni matendo ya kutapatapa tunajaribukushika hiki na kile katika kunusuru maisha lakini kiujumla hakuna tunachokifanya zaidi ya kupoteza rasilimali, muda na kudumaza mfumo. Ni wazi mtakubaliana na mimi kwamba hatutaendelea kama tutaendelea kuukmbatia mfumo waelimu wa sasa
Nitaendelea.....
 
Back
Top Bottom