Dhambi ya Deo Filikunjombi (mb) Ludewa

Dhambi ya Deo Filikunjombi (mb) Ludewa

paul nsangu

Senior Member
Joined
Nov 23, 2012
Posts
179
Reaction score
32
wanajf,

Naomba tafadhari leo ni mjulisheni mh. Filikunjombe dhambi yake huko jimboni kwake kama atakuwa amesahau basi namwomba aje na majibu haya kwa wananchi wa tarafa ya mwambao wa ziwa Nyasa, yaani vijji vya Makonde,Lifuma,Nsisi na Lupinga.

Dhambi yako kubwa pamoja na kukubalika kwako ni umewasahau kabisa wakisi kule ziwa Nyasa yaani kimawasiliano wako nyuma wakisi hawawezi hata kidogo kuwasiliana kwa njia ya simu tangu mawasiliano haya yaanze hapa Tz. Sasa mh. hivi una furahi sana unapoona Wakisi toka Makonde na Lifuma wapande milima ya Mambuhesa kilomita takriban 75 kwenda kijiji cha Mawengi kupiga simu?

Hivi wewe unaona ni vizuri hvo,kumbuka wewe una heshima kubwa sana hapa tz kutokana na umahiri wako pale bungeni sasa kwanini usiwajengee mnara wa mawasiliano pale Makonde? wakisi nao wakawa na mawasiliano.

Tafadhari naomba majibu yako juu ya hili kwani mwaka 2015 sio mbali kabisa utakuwa na wakati mgumu sana kule kwani Wakisi sio watu wa kuwapuuza hivi hawakawii kubadilika wale nami nitaungana nao katika kuijenga CHADEMA kule kuanzia sasa.

Mh. naomba majibu kuna mkakati wa kujenga mnara wa simu za mkononi ktk eneo hilo la mwambao?

nsangupaul@gmail.com
naomba kuwasilisha wakuu
 
Mbunge kwa sasa yuko bize anajadili swala la Muungano na Zanzibar!

Ludewa ni baadae!
 
Hivi Ludewa si ina Mkurugenzi,DC, Afisa Maendeleo ya jamii, n.k,kwa nini Mbunge awe mwarobaini wa kila kitu?
 
Kama ni hilo tu basi vuta subira kwani huyu ni mbunge wa taifa. Sote tunamtegemea yeye kuwasilisha vilio vyetu kwa serikali
 
Mbunge anajenga minara??? wapigie watu wa minara , au wapigie akina vodacom watawaletea watu wa minara
 
Kama ni hilo tu basi vuta subira kwani huyu ni mbunge wa taifa. Sote tunamtegemea yeye kuwasilisha vilio vyetu kwa serikali

ni kweli.... mradi umewasilisha hapa jf atakusikia na atakufikia....sina wasiwasi na hili jembe!
 
Hata kama ma DC wapo na wenye mitandao wapo, i5 mbunge ni wajb wake kuwasemea wananchi na kuwashawishi wenye mitandao kuwa kuna watumiaji wa cm wakutosha ili washawishke kujenga. Mbunge alione hili
 
Hata kama ma DC wapo na wenye mitandao wapo, i5 mbunge ni wajb wake kuwasemea wananchi na kuwashawishi wenye mitandao kuwa kuna watumiaji wa cm wakutosha ili washawishke kujenga. Mbunge alione hili

Alishawasemea, km unavyojua alishasema 'serikali yenyewe imevaa miwani ya mbao' wht do u expect?
 
Mbunge hata akijenga mnara hauwezi kufanya kazi mpaka kampuni husika washirikiane naye cha msingi wasiliana na mb wako awasiliane na kampuni ya cm waje kufanya visibility study and geomarketing wakiona italipa watasimamisha mnara kama haitolipa basi mbunge itabd haipeleke kwa waziri ili serikali ijenge huo mnara na sio tena kampuni ya cm asikwambie mtu kujenga mnara m1 si chini ya mil300 na maintanance kosti kwa mwezi si chini ya mil2...Kazi ya kujenga mnara ni ya kampuni ya cm na serikali wala sio ya mbunge.
 
amesikia huyo ni mbunge makini pia watu kampuni za mawasiliano changamkeni wateja hao hapo wamejitokeza wenyewe.
 
wanajf,

Naomba tafadhari leo ni mjulisheni mh. Filikunjombe dhambi yake huko jimboni kwake kama atakuwa amesahau basi namwomba aje na majibu haya kwa wananchi wa tarafa ya mwambao wa ziwa Nyasa, yaani vijji vya Makonde,Lifuma,Nsisi na Lupinga.

Dhambi yako kubwa pamoja na kukubalika kwako ni umewasahau kabisa wakisi kule ziwa Nyasa yaani kimawasiliano wako nyuma wakisi hawawezi hata kidogo kuwasiliana kwa njia ya simu tangu mawasiliano haya yaanze hapa Tz. Sasa mh. hivi una furahi sana unapoona Wakisi toka Makonde na Lifuma wapande milima ya Mambuhesa kilomita takriban 75 kwenda kijiji cha Mawengi kupiga simu?

Hivi wewe unaona ni vizuri hvo,kumbuka wewe una heshima kubwa sana hapa tz kutokana na umahiri wako pale bungeni sasa kwanini usiwajengee mnara wa mawasiliano pale Makonde? wakisi nao wakawa na mawasiliano.

Tafadhari naomba majibu yako juu ya hili kwani mwaka 2015 sio mbali kabisa utakuwa na wakati mgumu sana kule kwani Wakisi sio watu wa kuwapuuza hivi hawakawii kubadilika wale nami nitaungana nao katika kuijenga CHADEMA kule kuanzia sasa.

Mh. naomba majibu kuna mkakati wa kujenga mnara wa simu za mkononi ktk eneo hilo la mwambao?

nsangupaul@gmail.com
naomba kuwasilisha wakuu

Ujumbe huu nimeunakili kutoka Timeline ya Facebook wall ya Mbunge wako filikunjombe soma na uelewe
Deo Filikunjombe

May 7 via mobile

Serikali Kujenga Minara ya Simu Ludewa

Dodoma: Serikali imesema itaanza ujenzi wa minara ya simu katika maeneo ya Wilaya ya Ludewa yasiyofikiwa na huduma za mawasiliano ya simu kwa mwaka huu wa fedha 2013/14.

Taarifa hiyo ilitolewa bungeni jana na Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Charles Kitwanga wakati akijibu swali la Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe (CCM).

Katika swali lake, Filikunj
ombe alitaka kujua mpango wa Serikali kujenga minara ya simu eneo la mwambao wa Ziwa Nyasa na Milimani. Filikunjombe alisema wananchi wanalazimika kupanda juu ya miti kupata mawasiliano.

Waziri Kitwanga alisema ujenzi wa minara hiyo utagharimiwa kupitia fedha za Benki ya Dunia (WB), zabuni ya kwanza itatangazwa Mei mwaka huu.

Alivitaja vijiji ambavyo havina mawasiliano kuwa ni Chanjale, Lumbila, Nkanda, vijiji vya Kata ya Madilu, Lupingu, Ntumbati, Nindi, vijiji vya Kata za Kilondo, Makonde na Madope.

"Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCAF) inaendelea na jitihada zake kuhakikisha maeneo yote nchini hususan vijijini yanapata huduma za mawasiliano ya simu," alisema Kitwanga.

Naibu waziri huyo alisema lengo ni kuhakikisha maeneo yasiyofikiwa na watoa huduma yanafikiwa kwa kutumia mbinu mbalimbali, ikiwamo ruzuku inayotolewa na UCAF kushawishi kampuni za simu kupeleka mawasiliano maeneo hayo.



Jambo la kushangaza unashindwa kujua nini kinaendelea katika Mwambao wa Ziwa Nyasa, kwa nini huwasiliani na Mbunge wako wakati hata akina yakhe tunajua haya ambayo Munge wako ameposti kwenye wall yake anayowasiliana na wapiga kura wake juu ya suala unaloliongelea. Unaishi mawinguni au jimboni unakoongelea halafu usijue kinachoendelea?

Majuzi Kinana na Nape walipotembelea huko Ludewa pamoja na Filikunjombe, vijiji unavyovisema walimbeba juu juu Filikunjombe mbele ya Kinana na Nape kwa kumsifia kutimiza ahadi zake, na alitangaza ujumbe huo hapo juu ambao wengi wetu tulishausikia mipango ya kujengwa minara ya simu huko. Labda una kingine si haya unayoongelea.

 
Hii sio kazi ya Mbunge ndugu yangu!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Nakumbuka wiki kama tatu zilizopita kulikuwa na Ujumbe ulipokwenda Ludewa hasa maeneo ya Ziwa Nyasa, mojawapo ya maazimio yalikuwa ni kujenga barabara na kuweka mawasiliano ya simu. Sasa sijui mleta mada ulikuwa unafuatilia???
 
Back
Top Bottom