wanajf,
Naomba tafadhari leo ni mjulisheni mh. Filikunjombe dhambi yake huko jimboni kwake kama atakuwa amesahau basi namwomba aje na majibu haya kwa wananchi wa tarafa ya mwambao wa ziwa Nyasa, yaani vijji vya Makonde,Lifuma,Nsisi na Lupinga.
Dhambi yako kubwa pamoja na kukubalika kwako ni umewasahau kabisa wakisi kule
ziwa Nyasa yaani kimawasiliano wako nyuma wakisi hawawezi hata kidogo kuwasiliana kwa njia ya simu tangu mawasiliano haya yaanze hapa Tz. Sasa mh. hivi una furahi sana unapoona Wakisi toka Makonde na Lifuma wapande milima ya Mambuhesa kilomita takriban 75 kwenda kijiji cha Mawengi kupiga simu?
Nilitegemea umuhimize aikumbushe serikali kuweka sawa miundombinu ya barabara kwanza simu baadaye...kuna samaki na dagaa nyasa huko mnavua je mnajua bei tunayonunulia DSM...? Ni masikitiko na sidhani kama ndugu zangu wanapata faida kama wanavyopata wafanya biashara wachache huko..!!
Hivi wewe unaona ni vizuri hvo,kumbuka wewe una heshima kubwa sana hapa tz kutokana na umahiri wako pale bungeni sasa kwanini usiwajengee mnara wa mawasiliano pale Makonde? wakisi nao wakawa na mawasiliano.
Tafadhari naomba majibu yako juu ya hili kwani mwaka 2015 sio mbali kabisa utakuwa na wakati mgumu sana kule kwani Wakisi sio watu wa kuwapuuza hivi hawakawii kubadilika wale nami nitaungana nao katika kuijenga CHADEMA kule kuanzia sasa.
Mh. naomba majibu kuna mkakati wa kujenga mnara wa simu za mkononi ktk eneo hilo la mwambao?
nsangupaul@gmail.com
naomba kuwasilisha wakuu