Dhamana ya Lema: Tume iundwe suala zito la unajisi wa sheria na kuchafua mahakama nchini

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Maneno yaliyotamkwa na Jaji Bernard Luanda, mwenyekiti wa jopo la majaji lililoshughulika na rufaa ya serikali dhidi ya dhamana ya Lema ni mazito sana na suala hili halipaswi kuachwa likapita kirahisi. Kimsingi, yaliyosemwaa na jaji, kulingana na IPP Media, ni kwamba;

  • Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka inachafua mahakama nchini
  • Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka inawafanya wanasheria wote nchini hawana akili
  • Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka imetia najisi taaluma ya sheria nchini
  • Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) alitenda hila ili Lema anyimwe dhamana
  • Lema alinyimwa dhamana bila sababu za msingi kwa lengo la Mkurugenzi wa Mashitaka kumnyima haki
  • Inatia shaka kama ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka ina watu wanaojua sheria
Majaji hawa wameonyesha wazi kwamba mfumo mzima wa utawala wa sheria nchini uko hatarini kwa sababu tu taifa limeingiliwa na watu wachache wenye kiburi cha madaraka na ambao wanadhani wako juu ya sheria, wakitumia taasisi nyeti ya serikali kwa manufaa binafsi ya kisiasa.

Maneno ya jaji Luanda kwa niaba ya majaji wenzake, Jaji Stella Mugasha na Jaji Kipenka Mussa ni mazito sana. Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka kushutumiwa kwa maneno mazito kama hayo inabidi Waziri wa Sheria, Mwanasheria Mkuu na Mkurugenzi wa Mashitaka wote wajiuzuru mara moja ili kupisha tume huru kuchunguza nani alikuwa nyuma ya unajisi huu wa taaluma ya sheria na matumizi mabaya ya ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka nchini.

Mtu yeyote atakaepatikana kuhusika na unajisi huu wa sheria na matumizi mabaya ya ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka kunyima haki anapaswa kuchukuliwa hatua bila kujali ana madaraka gani nchini. Hata kama itadhihirika Raisi alihusika basi itabidi utaratibu wa "impeachment" au hatua yeyote inayofanana na hiyo zichukuliwe.
 
Looks familiar? Unajisi wa taaluma ya sheria
upload_2017-2-28_23-42-53.png
 
Kama jambo hili lingetokea ndani ya taifa lililostaarabika, hao wote uliowataja hawangesubiri kutumbuliwa tukianzia na Waziri mwenyewe. Bahati mbaya Tanzania haiko kwenye orodha ya nchi kama hizo...wenzetu wako karne ya ishirini na moja lakini sisi bado tunapiga mark-time kwenye karne ya kumi na tisa zama za viongozi madikteta uchwara.

Fikiria nchi ambayo wananchi wake wanapiga vigelegele na kushangilia kiongozi wao anapovunja Katiba, nchi ambayo vichaa kama Makonda huteuliwa na kupewa madaraka ya kuweza kumweka ndani kiongozi aliyechaguliwa na wananchi kuwawakilisha, nchi ambayo kazi ya polisi si kulinda bali kuhatarisha usalama wa wananchi and the list goes on...
 
Daaaa tuhuma nzito sanaa hizo nchi ya demokrasia kweli ilitakiwa DPP ajiuzulu au JPM amtoe haraka sana lakini sabbabu ya home boy amekubali hata ugomvi wake na AG ameufumbia macho sababu hizo hizo
 
Maneno yaliyotamkwa na Jaji Bernard Luanda, mwenyekiti wa jopo la majaji lililoshughulika na rufaa ya serikali dhidi ya dhamana ya Lema ni mazito sana na suala hili halipaswi kuachwa likapita kirahisi. Kimsingi, yaliyosemwaa na jaji, kulingana na IPP Media, ni kwamba;

  • Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka inachafua mahakama nchini
  • Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka inawafanya wanasheria wote nchini hawana akili
  • Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka imetia najisi taaluma ya sheria nchini
  • Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) alitenda hila ili Lema anyimwe dhamana
  • Lema alinyimwa dhamana bila sababu za msingi kwa lengo la Mkurugenzi wa Mashitaka kumnyima haki
  • Inatia shaka kama ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka ina watu wanaojua sheria
Majaji hawa wameonyesha wazi kwamba mfumo mzima wa utawala wa sheria nchini uko hatarini kwa sababu tu taifa limeingiliwa na watu wachache wenye kiburi cha madaraka na mbao wanadhani wako juu ya sheria, wakitumia taasisi nyeti ya serikali kwa manufaa binafsi ya kisiasa.

Maneno ya jaji Luanda kwa niaba ya majaji wenzake, Jaji Stella Mugasha na Jaji Kipenka Mussa ni mazito sana. Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka kushutumiwa kwa maneno mazito kama hayo inabidi Waziri wa Sheria, Mwanasheria Mkuu na Mkurugenzi wa Mashitaka wote wajiuzuru mara moja ili kupisha tume huru kuchunguza nani alikuwa nyuma ya unajisi huu wa taaluma ya sheria na matumizi mabaya ya ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka nchini.

Mtu yeyote atakaepatikana kuhusika na unajisi huu wa sheria na matumizi mabaya ya ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka kunyima haki anapaswa kuchukuliwa hatua bila kujali ana madaraka gani nchini. Hata kama itadhihirika Raisi alihusika basi itabidi utaratibu wa "impeachment" au hatua yeyote inayofanana na hiyo zichukuliwe.

Mahakama ni tambara bovu. Juzi ulimsikia Tundu Lissu analazimisha polisi akiri kuwa Judge Jecha alikosoa? Unamsikia kila siku anamtukana Rais kuwa ni uchwara? Sheria ndivyo ilivyo. Lakini aliyotenda Lema hakuonewa: alipewa dhamana alatumia muda huo kumtukana tena rais. Tuambie Lema hasa alikuwa na ujumbe gani aliouona no mchungu hati alamshawishi mkewe naye amtukane RC? Nchi hii tulikuwa tumefika mbali ngoja watu wanyoke kidogo
 
Mahakama ni tambara bovu. Juzi ulimsikia Tundu Lissu analazimisha polisi akiri kuwa Judge Jecha alikosoa? Unamsikia kila siku anamtukana Rais kuwa ni uchwara? Sheria ndivyo ilivyo. Lakini aliyotenda Lema hakuonewa: alipewa dhamana alatumia muda huo kumtukana tena rais. Tuambie Lema hasa alikuwa na ujumbe gani aliouona no mchungu hati alamshawishi mkewe naye amtukane RC? Nchi hii tulikuwa tumefika mbali ngoja watu wanyoke kidogo
Kwani wamepinda?Ukimuweka lema ndani ndio nchi ya viwanda imepatikana
 
Mahakama ni tambara bovu. Juzi ulimsikia Tundu Lissu analazimisha polisi akiri kuwa Judge Jecha alikosoa? Unamsikia kila siku anamtukana Rais kuwa ni uchwara? Sheria ndivyo ilivyo. Lakini aliyotenda Lema hakuonewa: alipewa dhamana alatumia muda huo kumtukana tena rais. Tuambie Lema hasa alikuwa na ujumbe gani aliouona no mchungu hati alamshawishi mkewe naye amtukane RC? Nchi hii tulikuwa tumefika mbali ngoja watu wanyoke kidogo

Muulize Gambo kilichomsibu akamwandikia ujumbe mke wa mwenzake??Hivi hujui kwa mwanaume Rijali yeyote,cheza na kila kitu chake lakini si mkewe.Karibu siku moja uone.

Kama Gambo hakufunzwa jandoni asicheze na wake za watu basi asubirie siku atakayoijutia.
 
Godbless Lema hakustahili kulala rumande hata kwa wiki moja, lakini kutokana na chuki za kutisha za mtu mmoja amelala rumande kwa miezi minne. Huu ukiukwaji wa sheria za nchi unaosababishwa na chuki za kutisha ni lazima ukemewe kwa nguvu zote.

Na huyu DPP ni lazima awajibishwe kwa kukubali kutumika na dikteta ili kuminya haki ya Kamanda Lema.
 
Inashangaza kwa nchi inayojiita ina utawala wa sheria, halafu inatokea mtu mmoja 'anaagiza' kuwa mtuhumiwa aendelee kusota Rumande kwa miezi 4, huku akijua wazi kuwa tuhuma anayokabiliwa nayo huyo mtu inadhaminika..........

Naunga mkono hoja hiyo kwa asilimia 100 kuwa kwa kuwa tayari majaji wameeleza kwa masikitiko makubwa namna suala la dhamana ya Mheshimiwa Lema ilivyofanyiwa 'figisu figisu' na wanasheria wa serikali chini ya DPP, ni lazima iundwe Tume huru ili ichunguze ni nani hasa alikuwa behind this ukiukwaji mkubwa kabisa wa sheria za nchi kwa lengo tu la kumkomoa mtu fulani.............
 
Maneno yaliyotamkwa na Jaji Bernard Luanda, mwenyekiti wa jopo la majaji lililoshughulika na rufaa ya serikali dhidi ya dhamana ya Lema ni mazito sana na suala hili halipaswi kuachwa likapita kirahisi. Kimsingi, yaliyosemwaa na jaji, kulingana na IPP Media, ni kwamba;

  • Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka inachafua mahakama nchini
  • Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka inawafanya wanasheria wote nchini hawana akili
  • Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka imetia najisi taaluma ya sheria nchini
  • Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) alitenda hila ili Lema anyimwe dhamana
  • Lema alinyimwa dhamana bila sababu za msingi kwa lengo la Mkurugenzi wa Mashitaka kumnyima haki
  • Inatia shaka kama ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka ina watu wanaojua sheria
Majaji hawa wameonyesha wazi kwamba mfumo mzima wa utawala wa sheria nchini uko hatarini kwa sababu tu taifa limeingiliwa na watu wachache wenye kiburi cha madaraka na mbao wanadhani wako juu ya sheria, wakitumia taasisi nyeti ya serikali kwa manufaa binafsi ya kisiasa.

Maneno ya jaji Luanda kwa niaba ya majaji wenzake, Jaji Stella Mugasha na Jaji Kipenka Mussa ni mazito sana. Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka kushutumiwa kwa maneno mazito kama hayo inabidi Waziri wa Sheria, Mwanasheria Mkuu na Mkurugenzi wa Mashitaka wote wajiuzuru mara moja ili kupisha tume huru kuchunguza nani alikuwa nyuma ya unajisi huu wa taaluma ya sheria na matumizi mabaya ya ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka nchini.

Mtu yeyote atakaepatikana kuhusika na unajisi huu wa sheria na matumizi mabaya ya ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka kunyima haki anapaswa kuchukuliwa hatua bila kujali ana madaraka gani nchini. Hata kama itadhihirika Raisi alihusika basi itabidi utaratibu wa "impeachment" au hatua yeyote inayofanana na hiyo zichukuliwe.
TLS should take lead
 
Kumbe ndiyo maana Bwana yule hapendi kabisa kusikia Tundu Lissu anakuwa Rais wa Tanganyika Law Society, kumbe ni kutokana na hizi 'figisu figisu' anazozifanya kuingilia mhimili wa Mahakama?

Anajua wazi kuwa Tundu Lissu atakapokuwa Presidaa wa TLS, hatakubali kuona mhimili mmoja ukijigamba kuwa wenyewe ndiyo uko juu ya mingine eti kwa sababu ndiyo uliojichimbia zaidi chini........
 
Mahakama ni tambara bovu. Juzi ulimsikia Tundu Lissu analazimisha polisi akiri kuwa Judge Jecha alikosoa? Unamsikia kila siku anamtukana Rais kuwa ni uchwara? Sheria ndivyo ilivyo. Lakini aliyotenda Lema hakuonewa: alipewa dhamana alatumia muda huo kumtukana tena rais. Tuambie Lema hasa alikuwa na ujumbe gani aliouona no mchungu hati alamshawishi mkewe naye amtukane RC? Nchi hii tulikuwa tumefika mbali ngoja watu wanyoke kidogo
tuambie hilo tusi ni tusi gani hilo?kusema ukiendelea na kiburi mungu atachukua uhai wako kabla ya 2020 ni tusi?
 
Maneno yaliyotamkwa na Jaji Bernard Luanda, mwenyekiti wa jopo la majaji lililoshughulika na rufaa ya serikali dhidi ya dhamana ya Lema ni mazito sana na suala hili halipaswi kuachwa likapita kirahisi. Kimsingi, yaliyosemwaa na jaji, kulingana na IPP Media, ni kwamba;

  • Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka inachafua mahakama nchini
  • Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka inawafanya wanasheria wote nchini hawana akili
  • Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka imetia najisi taaluma ya sheria nchini
  • Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) alitenda hila ili Lema anyimwe dhamana
  • Lema alinyimwa dhamana bila sababu za msingi kwa lengo la Mkurugenzi wa Mashitaka kumnyima haki
  • Inatia shaka kama ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka ina watu wanaojua sheria
Majaji hawa wameonyesha wazi kwamba mfumo mzima wa utawala wa sheria nchini uko hatarini kwa sababu tu taifa limeingiliwa na watu wachache wenye kiburi cha madaraka na mbao wanadhani wako juu ya sheria, wakitumia taasisi nyeti ya serikali kwa manufaa binafsi ya kisiasa.

Maneno ya jaji Luanda kwa niaba ya majaji wenzake, Jaji Stella Mugasha na Jaji Kipenka Mussa ni mazito sana. Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka kushutumiwa kwa maneno mazito kama hayo inabidi Waziri wa Sheria, Mwanasheria Mkuu na Mkurugenzi wa Mashitaka wote wajiuzuru mara moja ili kupisha tume huru kuchunguza nani alikuwa nyuma ya unajisi huu wa taaluma ya sheria na matumizi mabaya ya ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka nchini.

Mtu yeyote atakaepatikana kuhusika na unajisi huu wa sheria na matumizi mabaya ya ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka kunyima haki anapaswa kuchukuliwa hatua bila kujali ana madaraka gani nchini. Hata kama itadhihirika Raisi alihusika basi itabidi utaratibu wa "impeachment" au hatua yeyote inayofanana na hiyo zichukuliwe.
Labda likifikishwa bungeni lakini hili halitawezekana mpaka pale mheshimiwa T.A.LISU atakapopewa u Presidwaa wa TLS otherwise itakuwa makidamakida tu. Maneno hayo ya majaji yatumike kama kichocheo cha kuwafanya Wanachama wa tls waone umuhimu wa T.A.LISU kuwa raisi wao
 
MWENYEKITI wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amesema, uamuzi serikali kundoa pingamizi la rufaa ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema umewafariji sana.

Amewaeleza waandishi wa habari kuwa, rufaa ya serikali imeondolewa baada ya kuomba wenyewe kufanya hivyo, lakini imejidhihirisha kuwa mahakama ni mhimili unaojitegemea kwani inafanya kazi pasipo kusikiliza amri za wengine nje.

"Leo Mahakama imetufariji sana na kuturudishia imani yetu kwao kuwa ni chombo kilichosimama kwa miguu yake kama mhimili wake na haipokei maagizo ya serikali.

Awali Kesi ya Lema ilikwama kutolewa uamuzi na Jaji Salma Magimbi, Januari 4 mwaka huu, baada ya Wakili wa Serikali Innocent Njau, kuomba Mahakama hiyo kutoendelea na kesi hiyo kwa sababu wao wamekata Rufaa Mahakama ya Rufaa, kupinga Jaji Dk Modesta Opiyo kumwongezea muda wa siku 10 Lema ili akate rufaa ya hatma yake ya dhamana, nje ya muda.

Pia mawakili wa serikali walikata rufaa ya pili kupinga Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kukubali kumpa dhamana Lema. Hata hivyo, Jaji Salma Magimbi alisema kwa kuwa upande wa Jamhuri umekata rufaa hataweza kuendelea kutoa uamuzi wa kesi hiyo aliyosikiliza ya kulalamikia kunyimwa dhamana wakati mahakama ilimkubalia kumpa na kutoendelea kutoa masharti ya dhamana, sababu ya upande wa Jamuhuri kukata rufaa mahakama Kuu kupinga kupewa dhamana.

Jaji Dk Modesta Opiyo alitoa uamuzi Desemba 20 mwaka jana wa kumwongezea muda wa siku kumi Lema, ili akate rufaa yake ya kupinga kupewa dhamana bila masharti ya dhamana na kutupa pingamizi mbili za wanasheria wa serikali, waliokupinga kusikilizwa kwa rufaa hiyo kwa sababu iko nje ya muda kisheria lakini jaji huyo alisema kuwa hoja hizo hazikuwa na mashiko.

Lema alianza kukaa ndani Novemba 2 mwaka jana, baada ya kukamatwa viwanja vya Bunge Dodoma na kufikishwa Arusha, kisha Novemba 8 kufikishwa mbele ya Hakimu Mkazi Arusha na Hakimu Desderi Kamugisha na kumsomea mashitaka ya kesi namba 440 na 441 za uchochezi dhidi ya Rais Dk John Magufuli.

Hakimu Desderi Kamugisha alikubali kutoa dhamana kwa madai kuwa sheria haizuii kumpa dhamana mtu, kwa kesi ya uchochezi, ila kabla ya kutoa masharti ya dhamana licha ya kutamka dhamana ipo wazi lakini kabla ya kutoa masharti ya dhamana Mawakili wa serikali, Paul Kadushi na Wakili Mfawidhi wa serikali Mkoani Arusha, Materius Marandu walipinga kumpatia dhamana Lema kwa madai wameonesha nia ya kukata rufaa.

Kutokana na Mawakili hao kusema hivyo, Hakimu aliamua kesi hiyo ibaki kama ilivyo, mtuhumiwa asubiri maamuzi ya mahakama kuu na Lema alilazimika kwenda mahabusu hadi sasa yuko gereza Kuu la Kisongo.

Rufaa ya Lema sasa itasikilizwa mahakama Kuu Kada ya Arusha muda wowote kuazia sasa kwa mujibu wa wakili wa Lema Peter Kibatala. Kibatala alisema walikuwa wakihangaikia uamuzi mdogo wa majaji hao kisha kufungua kesi mahakama kuu ili ipangwe kwa jaji husika na ombi la rufaa liweze kusikilizwa na kupata hatma ya mbunge Lema kama atapewa dhamana au la.
 
Back
Top Bottom