Papaa Mobimba
JF-Expert Member
- Jan 27, 2018
- 980
- 3,646
Akiongea na wanahabari mkoani Morogoro ambapo yeye na wanachama wengine wamejivua uanachama wa CHADEMA, Devotha Minja amesema kuwa Makamu Mwenyekiti ameshindwa kuitisha kikao cha kamati kuu ili kwa pamoja wakae na kujadili madhila ambayo chama kinapitia kwa sasa ikiwa ni pamoja na kesi inayomkabili Tundu Lissu, lakini pia wanachadema kukamatwa
"Siyo jambo la kawaida tangu uchaguzi umeisha tukapata viongozi wapya, Kamati Kuu pekee iliyoitishwa ni ile iliyofanya usajihili wa wagombea wa uchaguzi wa kanda mbili ambazo ni kanda za Zanzibar, ambazo zilikuwa zimebakia kabla ya Mkutano Mkuu ili kupata viongozi wapya."
"Lakini chama kimepata madhila makubwa sana kwa mwenyekiti wetu (Tundu Lissu) kukamatwa na kusafirishwa usiku kucha na hatimaye kupewa kesi kubwa na mbaya, kesi ngumu ya uhaini lakini Makamu Mwenyekiti (John Heche) ambaye anajinasibu kuzuia uchaguzi ameshindwa kuitisha Kamati Kuu ili tujadili kwa pamoja ikiwa ni namna gani ya kupata ushauri wa wanasheria juu ya upi mwelekeo kwenye kukabiliana huko mahakamani ingawa Makamu Mwenyekiti anaonekana huko Dar es Salaam, anaonekana akiendelea na mikutano lakini ameshindwa kuitisha Kamati Kuu tujadili kwa pamoja namna ya kuhakikisha Mwenyekiti wetu anatoka gerezani." Devotha Minja
"Siyo jambo la kawaida tangu uchaguzi umeisha tukapata viongozi wapya, Kamati Kuu pekee iliyoitishwa ni ile iliyofanya usajihili wa wagombea wa uchaguzi wa kanda mbili ambazo ni kanda za Zanzibar, ambazo zilikuwa zimebakia kabla ya Mkutano Mkuu ili kupata viongozi wapya."
"Lakini chama kimepata madhila makubwa sana kwa mwenyekiti wetu (Tundu Lissu) kukamatwa na kusafirishwa usiku kucha na hatimaye kupewa kesi kubwa na mbaya, kesi ngumu ya uhaini lakini Makamu Mwenyekiti (John Heche) ambaye anajinasibu kuzuia uchaguzi ameshindwa kuitisha Kamati Kuu ili tujadili kwa pamoja ikiwa ni namna gani ya kupata ushauri wa wanasheria juu ya upi mwelekeo kwenye kukabiliana huko mahakamani ingawa Makamu Mwenyekiti anaonekana huko Dar es Salaam, anaonekana akiendelea na mikutano lakini ameshindwa kuitisha Kamati Kuu tujadili kwa pamoja namna ya kuhakikisha Mwenyekiti wetu anatoka gerezani." Devotha Minja