Dereva mzuri husikiliza abiria wake

Dereva mzuri husikiliza abiria wake

Me namshaur huyu dereva aongeze magia zaidi maana wawakilishi wetu sis kama abiria wanatetea siti zao na masirah yao pamoja na vyama...dereva piga magia hii gari haina abiria wa njian wote ni kituo kikuu
 
Dereva anajua jukumu lake, ukitaka kusikiliza abiria watakuyumbisha, maana kila abiria anaongea yake, mwingine mara Dereva ongeza mwendokasi, mwingine Dereva punguza mwendokasi, atafuata lipi hapo, mwishoni unaweza kususa hata kuendesha gari.

Mimi nilimwelewa vizuri, kwa tuliosoma fasihi haikuwa vigumu kumwelewa alichomaanisha.
 
Nijuavyo mimi Lori ni gari la mizigo na siyo abiria. kwa hiyo kwa sisi tuliosoma falsafa huyu anayesema yaye ni dereva mzuri wa Lori anatufanya kwamba sisi watanzania ni mizigo kama mizigo mingine tu ya magunia ya mkaa, viazi, nyanya, n.k. Hii ni dharau iliyopitiliza. Ni kweli dereva wa Lori hawezi kusikiliza kelele za mizigo kujibamiza bamiza ndani ya Lori.

Tungekuwa tumo kwenye gari la abiria tungekuwa na haki ya kusikilizwa. Maana hata polisi wa barabarani (Traffic) huwa wanaingia hadi ndani ya basi na kutuuliza kuhusu safari ilivyo, na hutuuliza kama dereva anaendesha kwa weledi. Mojawapo ya maswali hutuuliza hivi "Jamani kuna tatizo lolote katika safari yenu?". Hii maana yake ni kwamba abiria husikilizwa tofauti na mizigo ya kwenye Lori. Kutuita sisi ni mizigo ndani ya Lori ni kutudharau kabisa. Tunapaswa kuombwa radhi.
 
Godman: Unasema ulisoma fasihi? Fasihi hii hii tuliyosoma na sisi wenzako? Kama kweli ulisoma fasihi basi ilikupita 'kushoto'. Nikuulize swali, je, Lori ni gari la nini? Kwa mimi niliyesoma fasihi ni kwamba yeye anayesema ni dereva wa Lori, maana yake ni mbeba mizigo, maana Lori ni gari la mizigo na siyo gari la abiria. Kwa fasihi hiyo hiyo maana yake sisi tuliobebwa kwenye hilo Lori ni mizigo. Tunafananishwa na magunia ya mkaa, vitunguu, mbao, nyanya, n.k. Hii ni dharau kubwa sana. na kwa kweli abiria wa Lori hapaswi kusikiliza kelele za mizigo. Maana yake sisi watanzania ni mizigo. Tusingekuwa mizigo tungepakiwa kwenye gari la abiria kama vile Coaster, bus, ndege, n.k. Na tungekuwa humo tungesikilizwa tu. Mbona polisi wameweka hadi namba za simu ili tuseme nini kinaendelea safarini? Mbona hata traffic police huwa wanaingia hadi kwenye gari na kutuuliza habari ya safari yetu kama kuna chochote kibaya kinaendelea. Kuna hata kampeni ya "Abiria paza sauti"? Eti huyu Godman naye ni msomi wa fasihi. Ndo wasomi wa chama tawala kutuongoza kwenye Tanzania ya Viwanda! Vituko Tanzania haviishi.
 
izzo: Umefika darasa la ngapi ndugu yangu? Nikujuze kuwa ukimwambia jambo au shida yako Konda au Utingo na yeye akafikisha kwa dereva na kukusaidia shida yako au jambo lako maana yake ni kwamba dereva kakusikiliza shada yako. Kwa mfano, unamwambia konda kwamba umeshafika unaomba ushuke, naye akamwambia dereva akasimamisha gari ukashuka, je, dereva hajakusikiliza? Halafu nyie akina izzo mjue kwamba si magari yote yana konda au utingo. Ina maana wewe ukipanda gari isiyo na utingo huwezi kumwambia dereva shida yako? Akili hizi za kushoto mnazipata wapi?
 
Yaani tumefanywa mang'ombe tunapakiwa kwenye lori kweli watanzanian m50 tunaburuzwa na wasukuma wawili du nyerere baba uko wapi ununiio isinihusu bure maana siku hizi ni tz ya na kushangalia movie
 
Back
Top Bottom