Dereva bodaboda mtatuua

Dereva bodaboda mtatuua

Marco shija

Member
Joined
Sep 20, 2015
Posts
64
Reaction score
36
Yaliyonikuta mie jaman sina ya kusemea, napenda niwajulishe na rafk zangu mtambue hasa nyie mtakaokuja kufanya kazi iringa mjini.
Ni miezi takribani 7 hivi tangu nimepata kazi kwenye taasisi moja binafsi hapa mjini iringa, tangu nianze kazi nimekuwa nipo busy Sana na kazi zangu ili kuiwezesha taasisi hii niliyonayo iweze kupata faida kutokana na Mimi.
Mara nyingi nimekuwa siyo mtu wa kukaa Sana nyumban, nakaa sana ikiwa na weekend na siku za sikukuu, nimekuwa nikitumia ndugu zetu hawa wa pkpk kunisaidia kuniletea mahitaji yangu madogo madogo hasa mahitaji ya ndan kama nyama, Nyanya, chipsi na vingine ambavyo havihitaji gharama Sana.
Nimekuwa nikimtumia dereva bodaboda mmoja ajulikanae kwa jina la Rasi kuniletea nyama, hivi majuzi nilimtuma nyama kilo 1 aniletee na kweli aliniletea baada ya kama Dak 30 hivi, lakn kukawa na mahitaji mengne ya nyanya nikampigia simu hakupokea Kama Mara 3, ikanbd nimpigie dereva bodaboda mwingine akasema yupo karibu na mabucha ila Rasi hilo eneo hayupo, nikamuuliza ina maana nyama amenunulia wapi? Mwenzake akanijb ngoja afike home kwangu atanieleza, kweli huyu mwingine akaleta Nyanya zangu, Limao na viungo vingne, alipofika nikamuuliza kuna nn kwani. Akaniambia kaka uwe mtulivu Sana, akaniambia RASI HUYU ANAAMIKA KWA KUPELEKEA WATU NYAMA ZA MBWA Kwa kweli nilianguka nikijifikiria takribani miezi 6-7 namtuma yeye aniletee nyama kwa hiyo miezi yote hiyo nakula MBWA? Nimeumia na niliumia Sana, haikupita Dak 5 Rasi akaleta nyama zangu kiukweli sikuzipokea nikamwambia nyama nyingne imeletwa baada ya kutokupokea cm yake, nikamwambia Basi ila pesa nikampatia. Mbaya Zaid Kuna nyumba jiran ya police mmoja nae vile vile wanamtumia maana wao ndiyo walinielekeza, najiuliza na huyu kamanda nae anakula nyama ya MBWA, je kesi nikipeleka hapo kituoni watanisikiliza? Kiafya nipo salama sina tatzo japo sijapima. Nawashauri ndugu zangu hawa dereva pkpk siyo wa kuamin sana. Mie nimeumia Sana.
Jaman nisaidieni nifanyeje?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binamu yangu alikwenda masomoni Sweden, kufika kule alipokelewa na familia ya ki-Tanzania, walikaa nae weekend nzima. J3 imefika watoto wote walikwenda shule na wenyeji kazini, binadmu alikuwa na njaa, hakutaka kuingilia jiko la watu kwani weekend nzima mother house ndiye aliyekuwa anakorofisha. Aliamua kwenda dukani na pesa alizokuwa nazo kununua chakula. Kufika kule aliona kopo la nyama, lakini kwakua lugha haielewi alikwenda kwenye till aliambiwa kiasi cha pesa cha kulipa alilipa na kwenda nyumbani. Alifungua kopo lile na kula na mkate. Wenyeji waliporudi walikuta kopo la chakula cha mbwa kwenye bin, walimuuliza hiki chakula cha mbwa ni vipi aliwaambia alijiwahi njaa ilivyomtinga sana. Wenyeji walidhoofika kuwa kwanini hawakumuonyesha mazingira ya nyumba vizuri.
 
Mkuu una elimu gani na umri gani?
Maana sion jambo la maana uliloandika hapa..
Huyo aliyekuambia ni muongo na mnafiki .. Hyo ni mchoyo anamuharibia mwenzake biashara..
Kuna bodaboda waaminifu na ndio hutumiwa na watu wengi ila wale wasio waaminifu huona gere
 
Ungeipokea ile nyama aliyokuletea ungeenda kureport una wasi wasi ni nyama ya mbwa, ingefanyiwa uchunguzi na kama ingebainika ni kweli angechukuliwa hatua za kisheria.

Kumshtaki mtu huku huna uthibitisho wowote mimi naona ni ngumu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binamu yangu alikwenda masomoni Sweden, kufika kule alipokelewa na familia ya ki-Tanzania, walikaa nae weekend nzima. J3 imefika watoto wote walikwenda shule na wenyeji kazini, binadmu alikuwa na njaa, hakutaka kuingilia jiko la watu kwani weekend nzima mother house ndiye aliyekuwa anakorofisha. Aliamua kwenda dukani na pesa alizokuwa nazo kununua chakula. Kufika kule aliona kopo la nyama, lakini kwakua lugha haielewi alikwenda kwenye till aliambiwa kiasi cha pesa cha kulipa alilipa na kwenda nyumbani. Alifungua kopo lile na kula na mkate. Wenyeji waliporudi walikuta kopo la chakula cha mbwa kwenye bin, walimuuliza hiki chakula cha mbwa ni vipi aliwaambia alijiwahi njaa ilivyomtinga sana. Wenyeji walidhoofika kuwa kwanini hawakumuonyesha mazingira ya nyumba vizuri.
Mkuu hapo umechangia alichokiandika jamaa au naww umeandika story?
 
Binamu yangu alikwenda masomoni Sweden, kufika kule alipokelewa na familia ya ki-Tanzania, walikaa nae weekend nzima. J3 imefika watoto wote walikwenda shule na wenyeji kazini, binadmu alikuwa na njaa, hakutaka kuingilia jiko la watu kwani weekend nzima mother house ndiye aliyekuwa anakorofisha. Aliamua kwenda dukani na pesa alizokuwa nazo kununua chakula. Kufika kule aliona kopo la nyama, lakini kwakua lugha haielewi alikwenda kwenye till aliambiwa kiasi cha pesa cha kulipa alilipa na kwenda nyumbani. Alifungua kopo lile na kula na mkate. Wenyeji waliporudi walikuta kopo la chakula cha mbwa kwenye bin, walimuuliza hiki chakula cha mbwa ni vipi aliwaambia alijiwahi njaa ilivyomtinga sana. Wenyeji walidhoofika kuwa kwanini hawakumuonyesha mazingira ya nyumba vizuri.
Duuuh
 
Mkuu hujioni tofauti tofauti tangu uanze kula hizo nyama? Yaani una nguvu nguvu hivi na upeo wa kupambanua mambo umekua?? mambo ya mbwa hayo... Hahahahaha dunia ina vituko

Nishakula sana nyama za ajabu miaka ileee nafata pindi la hesabu mchikichini kwa Hiden

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hujioni tofauti tofauti tangu uanze kula hizo nyama? Yaani una nguvu nguvu hivi na upeo wa kupambanua mambo umekua?? mambo ya mbwa hayo... Hahahahaha dunia ina vituko

Nishakula sana nyama za ajabu miaka ileee nafata pindi la hesabu mchikichini kwa Hiden

Sent using Jamii Forums mobile app
Wachina wanadai inaleta nguvu sana mwilini hasa katika kipindi cha baridi
 
kitokacho ndicho haramu,
umekula hakijakudhuru nakushauri pambana na hali yako, ukisikia sana utachizi
 
Uko fit mkuu muda wote huo umetumia lakini hujadhurika.
 
Sasa huyo ni dereva boda au rasi?

sent from my iPhone 7s using JamiiForum mobile app.
 
Sasa wewe ni kitu gani kinakufanya uamini kuwa Ras anakuletea nyama ya mbwa?? Hata polisi watakushangaa....ushahindi kwanza ndo useme
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom