Wewe ndio hujui uhamiaji ni idara iliyoko katika wizara ya mambo ya ndani na haina chuo cha kufundishia vyuo vyake vinapatikana katika vyuo vifuatavyo
1.chuo cha ccp
hapa wanapiga wote kozi ya ujumla isipokuwa vipindi vya darasani vinatofautiana tu ila vipindi vyote vya mazoezi ni vile vile mud wa mafunzo ni miezi sita na itategemea maamuzi ya mkuu wa chuo anaweza kuwaongezea miezi ya mafunzo kutegemeana na mnavyoelewa
2.chuo cha magereza
hapa nako ni mpangilio uleule tu mazoezi mwanzo mwisho ila masomo ndio yanatofautiana
wizara ndio yenye uwezo wa kupanga kuwa ni wapi mafunzo yanafanyikia na pindi mafunzo yanaisha kwa vyuo vyote askari wa uhamiaji huwa wanabaki kwa ajili ya kumalizia topic kama hamjamaliza kwa hiyo mwenye kujua kuwa yanafanyikia wapi ni wizara kama wewe ndio waziri thibitisha ili watu wajiandae na siyo kuja na maneno ya vijiweni