Deni la Taifa sasa lafikia 39 trillioni

Deni la Taifa sasa lafikia 39 trillioni

- Deni la taifa

- kuporomoka kwa shilingi

- siasa chafu

Am worried tunakoelekea Tanzania..really worried!!!

Tunaelekea Ugiriki.

Sadly hatuna common currency na mataifa mengine.

We are on our own. Nchi atauziwa mchina.
 
Elimu yenyewe wanafunzi hawana madawat, chakula hakuna mishahara mbuzi. Madarasa, maabara hakuna.

Kaka mbaya zaidi WAKULIMA wadogo wadogo hawajalipwa mazaoyao na huu ni msimu wa pili..Kwa maana toka mwaka jana wakulima hawajalipwa mazao yao waliyoiuzia serikali,na wengi kati yao wameshindwa kumudu kulima sababu ya kushindwa kununua pembejeo,leo unasimama jukwaani kuwadanganya watanzania eti CCM inawaletea maendeleo..sijui maendeleo haya ni yapi,ya kudhulumu wakulima wadogo wadogo......
 
  • Thanks
Reactions: BAK
BAK mbaya zaidi pamoja na deni kupanda kuna WAKULIMA wadogo ambao walilazimishwa kuiuzia serikali mazao yao hawajalipwa toka mwaka jana msimu wa kuvuna.

Hebu fikiria wakulima hawa wameshindwa kulimamsimu huu sababu ya kukosa pembejeo na zana nyingine za kuwawezesha kulima.

Halafu leo unasubiria UCHUMI kukua utakuwaje ikiwa serikali ndiyo inayofadhili umaskini kwa kushindwa kuwalipa wakulima hawa haki yao makusudi kabisa.

Sioni umuhimu wa kuweka pesa nyingi za kuipigia Katiba ya Chenge ilhali kuna wakulima wengi hawajalipwa mazao yao kwa kipindi cha mwaka jana.

Halafu eti tunawaziri wa chakula sijui kilimo......yaani ni shida tu huko vijijini........wakulima wanatia huruma ndugu acha kabisa.............
 
Kaka mbaya zaidi WAKULIMA wadogo wadogo hawajalipwa mazaoyao na huu ni msimu wa pili..Kwa maana toka mwaka jana wakulima hawajalipwa mazao yao waliyoiuzia serikali,na wengi kati yao wameshindwa kumudu kulima sababu ya kushindwa kununua pembejeo,leo unasimama jukwaani kuwadanganya watanzania eti CCM inawaletea maendeleo..sijui maendeleo haya ni yapi,ya kudhulumu wakulima wadogo wadogo......

Hicho chakula walichowauzia nacho wameuza kupata pesa za kampein,shule za serikali eti wamefunga kabla ya muula hawana chakula....jamani jaman tanganyika yangu.
 
Hicho chakula walichowauzia nacho wameuza kupata pesa za kampein,shule za serikali eti wamefunga kabla ya muula hawana chakula....jamani jaman tanganyika yangu.

Uchaguzi mwaka huu wasidhani watu watazipokea hizo T-shirt,sijui itakuwaje huko ni taabi ndugu...wabunge nao wamelala usingizi hawajui kinachoenelea huko vijijini...............
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hizi ndio athari za kuwa na viongozi wasio kuwa na weledi na maono juu ya nchi kudaiwa kiasi hicho cha fedha. Huyu waziri wa fedha amepewa cheo hicho kama zawadi na sio uwezo wa kuongoza wizara hiyo nyeti; ifahamike tu kuwa kukua kwa deni la Taifa kunathiri uimara wa sarafu yetu kwani tunapokuwa tunalipa madeni kwa nchi za nje hatulipi kwa fedha yetu ya madafu bali kwa hard currency hivyo kupungua kwa reserves zetu kunakoletwa na ulipaji wa madeni kwa nchi za nje kunapunguza uwezo wa BOT kuweza kufanya intervention na kustabilize sarafu yetu!! Kikwete has done this country a terrible disservice during his ten year tenure by believing in mediocracy instead of meritocracy!!!
 
Ukiwa kiongozi CCM lazima ujifumie akili jumla. Huyu Saad.a atakuwa anaongea akiwa kashajitwika viroba vya kutosha
 
attachment.php
 
Waungwana,

Utawasikia hawa wahuni na vilaza na wimbo wao maarufu "Tanzania inakopesheka" na hivyo kuendelea kukopa toka ndani ya mabenki ya biashara nchini ambayo riba yake ni kubwa mno. Miaka miwili iliyopita deni la Taifa lilikuwa ni 20 Trillioni lakini hawa vilaza na wahuni waliojivisha ngozi ya uongozi wakaendelea na wimbo wao maarufu ambao haujali maslahi ya Tanzania na Watanzania wimbo wa "Tanzania inakopesheka" na hivyo kuendelea kuchukua mikopo mikubwa toka mabenki ya biashara. Hatima yake katika miaka miwili deni la Taifa limeongezeka karibu mara mbili toka trillion 20 mpaka Trilioni 39 na yule mkwer pale Ikulu yuko kimyaaaaa wala hati neon. Kama alivyosema kishajichokea anangoja miezi yake ikatike akatafune mabilioni yake aliyopewa na marafiki zake akina Ruge na wenzie.

Cha kustaajabisha waungwana pamoja na deni kuongezeka kwa kasi ya kutisha hakuna hatua zozote zinazochukuliwa ili kupambana na kasi ya ukuaji wa deni la Taifa. Bado kila mwaka Serikali inaruhusu misamaha ya kodi ya shilingi trilioni 1.5, bado kila mwaka matumizi yaliyojaa matanuzi makubwa ununuzi wa mashangingi chungu nzima, safari za nje za mkwere ambazo hazina tija kwa Taifa akiwa na kundi kubwa la maofisa wake badi zinaendelea karibu kila mwezi bila kujali kwamba hali ya nchi kifedha ni mbaya sana. Na wakati huo huo pamoja na hali ya kifedha nchini kuwa mbaya Wabunge, Mawaziri, Waziri Mkuu na Rais ambao wana mishahara mikubwa sana bado mishahara yao haitozwi kodi. Serikali ilikuja na utaratibu wa wenye nyadhifa za juu wauziwe magari ya Serikali ili kuipunguzia Serikali mzigo mkubwa wa kuyagharamia magari hayo kwa petroli, matengenezo na mishahara ya madreva, lakini baada ya kuuziana magari hayo wakaendelea na ununuzi wa magari ya kifahari yenye consumption kubwa sana ya petroli bila kujali mzigo kwa walipa kodi na yale waliyonunua kuyaweka majumbani mwao.

Pamoja na nchi yetu kujaliwa utajiri mkubwa sana wa rasilimali chungu nzima ikiwemo dhahabu, uranium, almasi, Tanzanet, gesi na nyingi nyinginezo hawa wahuni na vilaza wamesaini mikataba ambayo haina maslahi kwa nchi yetu na watu wake. Kama mtakumbuka Muhongo alivyogoma kata kata kuipeleka mikataba mbali mbali ya madini nchini ikajadiliwe na Wabunge lakini hakufanya hivyo. Huyu Waziri mpya wa Madini na Nishati naye sijaona dalili zozote kama ana mpango wa kuipeleka mikataba hii Bungeni ili Watanzania tuwezi kufahamu kulikoni pamoja na utajiri mkubwa wa rasilimali nchini na kuwakaribisha wageni wavune rasilimali hizo lakini karibu mwaka wa 20 sasa bado Watanzania hatujaona maslahi yoyote yaliyoletwa na utjiri wetu mkubwa. Mashule, Mahospitali yetu bado yana hali ya kusikitisha. Shule hazina madawati wala walimu, barabara zetu ziko chini ya viwango, ATC iko hohehahe, usafiri wetu wa majini bado ni wa hatari na wa kusikitisha sana, mahospitali hayana madawa wala vifaa muhimu hawa wenye nchi wakiugua hao kiguu na njia kwenda kutibiwa nje ya nchi kwa pesa za walipa kodi na huku mahospitali yakizidi kuwa katika hali mbaya. Upatikanaji wa maji na umeme bado ni wa kusuasua miaka nenda miaka rudi lakini hakuna anayejali hata kidogo.

Wanachojali hawa wahuni na vilaza ni wao kubaki madarakani kwa nguvu zao zote hata kama kwa kutumia mtutu wa bunduki na huku nchi ikizidi kuangamia. Waliimba wimbo wao maarufu "Tanzania tunakopesheka" wakati deni la Taifa liko trilioni 10, wakaendelea na wimbo huo miaka miwili iliyopita wakati deni lilikuwa limeongezeka mara mbili na kufikia Trilioni 20 hatima yake ni kwamba sasa deni liko karibu kufikia trilioni 40 bado tu wanaendelea na nyimbo yao "Tanzania tunakopesheka" sijui tunalipa principal kiasi gani kwa mwezi/mwaka na riba tunalipa kiasi gani hawa wahuni na vilaza wanalificha hili makusudi ili waweze kuendelea kuimba wimbo wao "Tanzania tunakopesheka"

Haya Waungwana tuendelee nasi kuimba huu wimbo wa hawa wahuni na vilaza "Tanzania tunapokesheka" na labda miaka miwili mingine hili deni la Taifa litakuwa limefikia trilioni 80 labda hapo tutastuka na kubadili wimbo na kuanza kuimba "Tanzania hatukopesheki" wimbo ambao tulitakiwa tuuimbe miaka 20 iliyopita.

Muwe na weekend njema.


 
They just don't care because they know that they are losing the battle, mambo si shwari kabisa ndani ya ccm, so why should they care? Kila mtu anajiandalia'safe exit'
 
Waungwana,

Utawasikia hawa wahuni na vilaza na wimbo wao maarufu "Tanzania inakopesheka" na hivyo kuendelea kukopa toka ndani ya mabenki ya biashara nchini ambayo riba yake ni kubwa mno. Miaka miwili iliyopita deni la Taifa lilikuwa ni 20 Trillioni lakini hawa vilaza na wahuni waliojivisha ngozi ya uongozi wakaendelea na wimbo wao maarufu ambao haujali maslahi ya Tanzania na Watanzania wimbo wa "Tanzania inakopesheka" na hivyo kuendelea kuchukua mikopo mikubwa toka mabenki ya biashara. Hatima yake katika miaka miwili deni la Taifa limeongezeka karibu mara mbili toka trillion 20 mpaka Trilioni 39 na yule mkwer pale Ikulu yuko kimyaaaaa wala hati neon. Kama alivyosema kishajichokea anangoja miezi yake ikatike akatafune mabilioni yake aliyopewa na marafiki zake akina Ruge na wenzie.

Cha kustaajabisha waungwana pamoja na deni kuongezeka kwa kasi ya kutisha hakuna hatua zozote zinazochukuliwa ili kupambana na kasi ya ukuaji wa deni la Taifa. Bado kila mwaka Serikali inaruhusu misamaha ya kodi ya shilingi trilioni 1.5, bado kila mwaka matumizi yaliyojaa matanuzi makubwa ununuzi wa mashangingi chungu nzima, safari za nje za mkwere ambazo hazina tija kwa Taifa akiwa na kundi kubwa la maofisa wake badi zinaendelea karibu kila mwezi bila kujali kwamba hali ya nchi kifedha ni mbaya sana. Na wakati huo huo pamoja na hali ya kifedha nchini kuwa mbaya Wabunge, Mawaziri, Waziri Mkuu na Rais ambao wana mishahara mikubwa sana bado mishahara yao haitozwi kodi. Serikali ilikuja na utaratibu wa wenye nyadhifa za juu wauziwe magari ya Serikali ili kuipunguzia Serikali mzigo mkubwa wa kuyagharamia magari hayo kwa petroli, matengenezo na mishahara ya madreva, lakini baada ya kuuziana magari hayo wakaendelea na ununuzi wa magari ya kifahari yenye consumption kubwa sana ya petroli bila kujali mzigo kwa walipa kodi na yale waliyonunua kuyaweka majumbani mwao.

Pamoja na nchi yetu kujaliwa utajiri mkubwa sana wa rasilimali chungu nzima ikiwemo dhahabu, uranium, almasi, Tanzanet, gesi na nyingi nyinginezo hawa wahuni na vilaza wamesaini mikataba ambayo haina maslahi kwa nchi yetu na watu wake. Kama mtakumbuka Muhongo alivyogoma kata kata kuipeleka mikataba mbali mbali ya madini nchini ikajadiliwe na Wabunge lakini hakufanya hivyo. Huyu Waziri mpya wa Madini na Nishati naye sijaona dalili zozote kama ana mpango wa kuipeleka mikataba hii Bungeni ili Watanzania tuwezi kufahamu kulikoni pamoja na utajiri mkubwa wa rasilimali nchini na kuwakaribisha wageni wavune rasilimali hizo lakini karibu mwaka wa 20 sasa bado Watanzania hatujaona maslahi yoyote yaliyoletwa na utjiri wetu mkubwa. Mashule, Mahospitali yetu bado yana hali ya kusikitisha. Shule hazina madawati wala walimu, barabara zetu ziko chini ya viwango, ATC iko hohehahe, usafiri wetu wa majini bado ni wa hatari na wa kusikitisha sana, mahospitali hayana madawa wala vifaa muhimu hawa wenye nchi wakiugua hao kiguu na njia kwenda kutibiwa nje ya nchi kwa pesa za walipa kodi na huku mahospitali yakizidi kuwa katika hali mbaya. Upatikanaji wa maji na umeme bado ni wa kusuasua miaka nenda miaka rudi lakini hakuna anayejali hata kidogo.

Wanachojali hawa wahuni na vilaza ni wao kubaki madarakani kwa nguvu zao zote hata kama kwa kutumia mtutu wa bunduki na huku nchi ikizidi kuangamia. Waliimba wimbo wao maarufu "Tanzania tunakopesheka" wakati deni la Taifa liko trilioni 10, wakaendelea na wimbo huo miaka miwili iliyopita wakati deni lilikuwa limeongezeka mara mbili na kufikia Trilioni 20 hatima yake ni kwamba sasa deni liko karibu kufikia trilioni 40 bado tu wanaendelea na nyimbo yao "Tanzania tunakopesheka" sijui tunalipa principal kiasi gani kwa mwezi/mwaka na riba tunalipa kiasi gani hawa wahuni na vilaza wanalificha hili makusudi ili waweze kuendelea kuimba wimbo wao "Tanzania tunakopesheka"

Haya Waungwana tuendelee nasi kuimba huu wimbo wa hawa wahuni na vilaza "Tanzania tunapokesheka" na labda miaka miwili mingine hili deni la Taifa litakuwa limefikia trilioni 80 labda hapo tutastuka na kubadili wimbo na kuanza kuimba "Tanzania hatukopesheki" wimbo ambao tulitakiwa tuuimbe miaka 20 iliyopita.

Muwe na weekend njema.


BAK naomba ukiweza hii post fanya uiweke Kule MAWIO kama makala, ni mojawapo ya post zilizo na na ukweli mtupu, ukweli mchungu ambao unapaswa kusomwa na wengi kadiri iwezekanavyo
Inapaswa kusoma hasa na wale wenye macho ya upofu walioko ccm na wanaoona mambo yako OK,
Kwangu haitakuwa weekend njema BAK Bali WEEKEND YA TAFAKURI
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom