Bahati mbaya miradi yenyewe tukoteketeza fedha zetu mingi hailipi hata 25% ya makusudio yake, sababu ya kwanza kubwa ni kucheleweshwa mno. Mfano, mradi wa DART umetumia mabilioni mengi sana lengo ikiwa ni kupunguza foleni jijini Dar es Salaam. Hata hivyo, foleni inazidi na haielekei kuwa DART itapunguza foleni badala yake itaiongeza. Ina maaana kuwa fedha yoote tuliyokopa ni kama tumeichoma moto, haina faida yoyote kwenye uchumi wa nchi kwani mzigo wa kiuchumi unaosababishwa na foleni unaongezeka. Pili DART imechelewa mno toka ilipopangwa kuwa ianze. Ikumbukwe kuwa mkopeshaji huanza kuhesabu siku fedha inapochukuliwa na si siku unapomaliza mradi. Maanake ni kuwa kuendelea kuchelewa kwa DART ni kuendeleza mzigo wa kiuchumi Jumlisha sasa tuna deni linaloanza kuzaa faida, hata kama ni kwa asilimia ndogo.