Deni la taifa lazidi kupaa

Jul 24, 2012
81
6
mgimwa.jpg
Dk. William Mgimwa

WAZIRI wa Fedha, Dk. William Mgimwa, amesema deni la taifa limezidi kukua. Amesema deni hilo limeongezeka hadi Sh bilioni 20,865 Juni, mwaka huu kutoka Sh bilioni 18,617 Juni mwaka jana.
Dk. Mgimwa, alitoa taarifa hiyo bungeni jana alipokuwa akisoma hotuba ya bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha wa 2012/2013.

“Wizara ya Fedha imeendelea kusimamia deni la taifa kwa kuzingatia mkakati wa kusimamia deni la taifa la mwaka 2002 pamoja na sheria ya mikopo, dhamana na misaada namba 30 ya mwaka 1974 pamoja na marekebisho yake ya mwaka 2004.

“Hadi mwishoni mwa Juni mwaka 2012, deni la taifa lilikuwa Sh bilioni 20,865 ikilinganishwa na deni la Sh bilioni 18,617 Juni, mwaka jana ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 10.7.

“Kati ya fedha hizo, Sh bilioni 15,927.1 ni deni la nje na Sh bilioni 4,937.9 ni deni la ndani. Kati ya kiasi hicho cha deni la nje, Sh 12,644.6 ni deni la umma na kiasi kilichobaki cha Sh 3,282.5 ni deni la sekta binafsi.

“Pia hadi kufikia Juni mwaka huu, deni la ndani la Serikali lilifikia Sh bilioni 4,937.9 ikilinganishwa na Sh bilioni 4,729 Juni, mwaka jana ambalo ni sawa na ongezeko la asilimia 4.2.

Wakati deni la taifa likikua, Dk. Mgimwa alisema mfumko wa bei nao umezidi kupaa kutoka asilimia 13 Julai mwaka jana hadi kufikia asilimia asilimia 17.4 Juni mwaka huu.

Msemaji wa Kambi ya Upinzani katika wizara hiyo, ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), alitaka ufanyike ukaguzi maalum kubaini uhalali wa deni hilo.

Kwa mujibu wa Zitto, ukaguzi ukifanyika utawezesha kujulikana kama miradi iliyotekelezwa kupitia miradi hiyo inatekelezwa kama inavyotakiwa au kuna mazingira yenye utata.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi, Dunstan Kitandula (CCM), alisema kuna haja Serikali ikadhibiti deni hilo la taifa kabla halijaongezeka zaidi.

Kitandula ambaye ni Mbunge wa Mkinga, alisema kuna haja pia Serikali ikaendelea kuwa na sera nzuri za bajeti na fedha kuepukana na madeni yasiyokuwa na maana.
 
Nchi inaendeshwa kisanii kwelikweli...hivi ni kwamba tumekosa wana-uchumi mahiri wa kutusaidia katika ili? Maana kila siku deni la taifa linakuwa, na pesa inayopatikana haigusi watanzania wakawaida. Mfumuko wa bei ndio imekuwa kama kiitikio kwetu, na hakuna anayechukua hatua za dhati kusahihisha hili.
 
Ndo uchumi unakuwa kwa kasi! na si lazima ukuaji uende kwa wananchi hata ukienda kwa waliochaguliwa na wakatajirika pia uchumi ndo unaimarika zaidi! Kila siku kiguu na njia utalima lini kama wewe ni mkulima na kama uko hivyo njia rahisi ni kukuza uchumi wa mifuko yako kwa mikopo ya wanaofanya kazi na wale ambao hawatembei bila malengo kuwa wakwanza kusalimia!
 
Unajua tatizo lililopo ni wananchi kutokuwa na elimu/uelewa wa kutosha kuhusu jinsi gani deni la taifa linaathiri maisha yao ya kila siku, lakini pia madhara yake kwa maisha yao ya uzeeni na yale ya wajukuu zao; kuna umuhimu wa wananchi kuanza kuelimishwa juu ya hili hasa uhusiano wa moja kwa moja baina ya deni la taifa na maisha yao ya kila siku na ya baadae;
 
Ndo uchumi unakuwa kwa kasi! na si lazima ukuaji uende kwa wananchi hata ukienda kwa waliochaguliwa na wakatajirika pia uchumi ndo unaimarika zaidi! Kila siku kiguu na njia utalima lini kama wewe ni mkulima na kama uko hivyo njia rahisi ni kukuza uchumi wa mifuko yako kwa mikopo ya wanaofanya kazi na wale ambao hawatembei bila malengo kuwa wakwanza kusalimia!

Deni la taifa halilipwi na kasi ya kukua kwa uchumi bali kasi ya kukusanya mapato ya nchi, ingawa kuna uhusiano wa mbali baina ya kasi ya kukua kwa uchumi na deni la taifa;.
 
Tanzania faces new debt crisis ...AS NATIONAL DEBT SOARS TO MORE THAN $10 BILLION

By ThisDay Reporter

25th October 2010
TANZANIA is facing a new debt crisis as budget crunches in rich countries are bringing cuts in aid spending, forcing the government to seek loans to meet budget deficits.

During the year ending July 2010, the national debt stock soared by more than $1.185 billion to a staggering $10.1 billion, according to Bank of Tanzania figures.


At the end of December 2006, the country's national debt stood at around $7 billion.


My Take:
Waliosema kuchagua CCM ni janga walisema kweli.
 
Yani by december 2006 deni lilikuwa $7b and now barely five years later it has more than doubled! Kweli kazi tunayo
 
Hili ni janga la kitaifa ndugu zangu mimi nafikiri wananchi wote wa hitikadi zote, wazalendo na wenye mapenzi mema tukae tuangalie tufanye nini kuepusha janga hili. Ukiliangalia deni accumulated in hardly 7 years kesho maisha ni magumu. Wajukuu zetu pamoja vitukuu watallipa deni hili lakini wakati huo watauliza hivi hii debt was accumulated kwa kufanya nini? Hakuna watakachokiona cha maana barabara za mzee wa kukariri njia zitakuwa zimebaki mashimo tu. Wataona shule za kata lakini wahitimu wasijua kitu, reli ya mjerumani iliyokufa maana deni hili halikuiboresha, mashimo yaliyokana na machimbo ya madini lakini faid ya madini haionekani maana kusingekuwa na deni kubwa na hali tunachimba madini. Kwa kweli they will find everything pathetic, in a shumbles and total obsicurity. Ole watu tulioshiriki ufisadi huu wataponda makaburi yetu kwa mayai viza
 
Deni lipo kwenye currency za nje USD,Euro, Pound nk

Hata kama hakuna ongezeko la kukopa shillingi ikishuka kwa senti 5 dhidi ya dollar tayari deni linaongezeka kwenye hesabu zetu za madafu.
 
tungekuwa tunaongeza wahitimu wa vyuo wenye uwezo mkubwa (competent) basi tungekuwa na imani kuwa nchi ina future maana hawa wangeweza kufanya kazi kwa bidii na maarifa kulipunguza. Lakini ndio kabisa wanaofaulu kwenda sekondari hawajui hata kusoma na kuandika dalili iliyo wazi kuwa watoto wa vigogo pekee hawawezi kulilipa hili deni, wako most likely kuaiga tabia za wazazi wao - ufisadi, kutowajibika na wizi!

Tunaomba asimame Mtanzania hapa na kutangaza kuwa akipewa nchi kuiongoza atapunguza DENI LA TAIFA!!!!
 
Deni lipo kwenye currency za nje USD,Euro, Pound nk

Hata kama hakuna ongezeko la kukopa shillingi ikishuka kwa senti 5 dhidi ya dollar tayari deni linaongezeka kwenye hesabu zetu za madafu.


Masikini Tanzania,watu wako wameishiwa upendo mtu anajiangalia yeye. Haiingia akilini mtu anayejiita great thinker anatetea uozo wa namna hii, hata kama exchange rate inabadilika kwa kasi deni lisingekua kwa kasi namna hii. Too bad kwa sababu wakiambiwa waoneshe hizo pesa zimefanya kitu gani hawawezi. Lets be realistic, tusitetee ushenzi wa namna hii kwa sababu ya itikadi za vyama vyetu, lets term black black..... Kama wewe kwenye jamii forum unafikia hatua ya kutetea uozo huu namna hii, sipati picha kwa mtu ambaye yuko sigimbi atafanya nn.... Its shame.
 
Back
Top Bottom