Dah! Mwanangu ummetumia busara kweli.
Kibuti cha kimya kimya huwa kinawauma sana hasa vicheche.
Mimi kuna mmoja alikuwa ana mipango hiyo hiyo, mara tukiwa naye mtu anampigia simu naye bila aibu eti anapokea na anaongea na njemba mbele yangu,,, nilichofanya hata sikumuuliza huyo ni nani uliyekuwa unaongea naye. Tulimaliza mambo yetu na tukaagana kwa amani tu. Ikatokea kila akipiga simu tukutane nampa visingizio kibaao mradi tusikutane.. Alivyokuja kugundua kuwa mwenzake sina habari naye tena eti anakuja kunambia nikimhitaji wakati wowote nisisite kumtafuta eti bado ananipenda! Siku hizi huwa tunawasiliana kama marafiki tu. Mpaka leo ananiomba nimwambie sababu ya kutokutaka mahusiano naye, eti moyo unamuuma...
Jamani ukimtenda mpenzi wako na ukaona amekaa kimya usifikiri kuwa umepata boya la kuchezea..