George Bush, Snr
George Bush, Jr
Jamani, sio Tanzania tu. Ukweli utabaki kuwa wanasiasa huwaandaa watoto wao kushika uongozi tangia wakiwa wadogo. Watoto nao huanza kuona raha ya uongozi wakiwa wadogo, na hivyo hupania kuwa viongozi ili kuendeleza "utajiri" wa wazazi wao.
Samahani nikisema kuwa, hata vyama vingine vya siasa havitaepa kawaida hii. Mjadala hapa ni je wamepatikana "by merits" na kwa njia zilizo wazi na bila upendeleo? Mfano, CHADEMA tunao wabunge wawili Nyerere na wawili Lisu, je hilo ni kosa? Binafsi sioni kama ni kosa, ili mradi wamepatikana kwa "merits" zao na kwa vigezo vilivyo sahihi.
Hata hivyo, haipendezi kuona msululu wa viongozi katika chama au katika serikali wanatoka katika familia moja, na hasa kama hawana uwezo zaidi ya wengine. Ninaona huu ni mtihani mkubwa kwa CHADEMA katika chaguzi tunazozitegemea ndani ya chama. Nitasikitika sana kama CHADEMA kitaingia katika mtego wa "undugu".