Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 17,018
- 20,489
Kifalsafa zaidi Afrika haiwezi kuishi maisha yaliyoishi Ulaya na Amerika, Nchi zote zilizoendelea zilipita kwenye mikono ya kiimla na kidikteta japokuwa nyakati ziliruhusu kuwa hivyo,
Njia hizo haziwezi na hazitotokea kuisaidia Afrika, Afrika lazima ichague utaratibu wake wa kufikia malengo iyatakayo na siyo njia hii tuiendeayo ambayo ni njia waliyopita Ulaya na Amerika karne ya 18-19, Nyakati za leo zinakataa. Wapo wanaoitazama dunia kuwa inaongwa kidkteta hasa Uchina, Korea Kaskazini, Korea Kusini, Urusi nk... Lakini hawafahamu kuwa ule sio udikta ni utawala wa sheria na katiba uliojengwa katika misingi ya karne ya 18-19 ambpo dunia ilikuwa chini ya mkono wa chuma. Leo ule SIO UDIKTETA.
Udikteta upo wa aina moja tu, ni utawala usiofuata katiba na sheria, utawala wa mtu mmoja tu, utawala wa matamko (decree), na madikteta wapo wa aina mbili, ambao ni Dikteta msomi, na dikteta mpuumbavu... Hawa hutofautiana katika staili zao za kutawala, Dikteta msomi hutawala huku watu wake wakilia machozi moyoni na usoni wakicheka, huku dikteta mpuumbavu, hutawala huku watu wake wakilia machozi machoni huku moyoni wakikenua meno... Uchaguzi ni wako.
Udikteta wowote hata ule unaopambwa na wajasiliasiasa kuwa ni udikteta mamboleo kamwe haujawahi kuiendesha dunia ya leo, labla kwenye nchi ya Nodi. Hakuna udikteta mamboleo duniani, hilo ni ingizo jipya katika uhalifu wa kisiasa wa wanasiasa wanaotumia vibaya kiuongo chao kiitwacho tumbo.. Tumbo ukiliruhusu likutawale litakufanya hata uwe Prof utafanya mambo kama Prof Lipumba au hata uwe Dr utafanya mambo kama Dr Rutengwe.
Demokrasia ya ulaya katika nchi masikini ni umasikini.
Njia hizo haziwezi na hazitotokea kuisaidia Afrika, Afrika lazima ichague utaratibu wake wa kufikia malengo iyatakayo na siyo njia hii tuiendeayo ambayo ni njia waliyopita Ulaya na Amerika karne ya 18-19, Nyakati za leo zinakataa. Wapo wanaoitazama dunia kuwa inaongwa kidkteta hasa Uchina, Korea Kaskazini, Korea Kusini, Urusi nk... Lakini hawafahamu kuwa ule sio udikta ni utawala wa sheria na katiba uliojengwa katika misingi ya karne ya 18-19 ambpo dunia ilikuwa chini ya mkono wa chuma. Leo ule SIO UDIKTETA.
Udikteta upo wa aina moja tu, ni utawala usiofuata katiba na sheria, utawala wa mtu mmoja tu, utawala wa matamko (decree), na madikteta wapo wa aina mbili, ambao ni Dikteta msomi, na dikteta mpuumbavu... Hawa hutofautiana katika staili zao za kutawala, Dikteta msomi hutawala huku watu wake wakilia machozi moyoni na usoni wakicheka, huku dikteta mpuumbavu, hutawala huku watu wake wakilia machozi machoni huku moyoni wakikenua meno... Uchaguzi ni wako.
Udikteta wowote hata ule unaopambwa na wajasiliasiasa kuwa ni udikteta mamboleo kamwe haujawahi kuiendesha dunia ya leo, labla kwenye nchi ya Nodi. Hakuna udikteta mamboleo duniani, hilo ni ingizo jipya katika uhalifu wa kisiasa wa wanasiasa wanaotumia vibaya kiuongo chao kiitwacho tumbo.. Tumbo ukiliruhusu likutawale litakufanya hata uwe Prof utafanya mambo kama Prof Lipumba au hata uwe Dr utafanya mambo kama Dr Rutengwe.
Demokrasia ya ulaya katika nchi masikini ni umasikini.