Demokrasia Bungeni Inapokuwa Demoghasia

Demokrasia Bungeni Inapokuwa Demoghasia

Hata hivyo kilichofanywa na Ukawa bungeni jana ni jambo la kawaida sana kwenye mabunge mengi duniani.
Hiyo ndiyo njia pekee ya kufikisha ujumbe kwa watawala ambao huwa wanajifanya 'viziwi' kutotaka kusikiliza hoja za msingi zinazotolewa na kambi za upinzani kwa maslahi ya Umma wa wananchi waliowapa ridhaa ya kuingia bungeni.
Hata hivyo mbona walichofanya Ukawa jana bungeni ni 'cha mtoto' ukilinganisha na kashikashi zinazotokea kwenye baadhi ya mabunge mengine duniani?
Yapo baadhi ya mabunge mengine huwa inafikia waheshimiwa wabunge wanazichapa kavu kavu kutokana na 'kiburi' cha watawala na hata wakati mwingine kurushiana hadi viti vilivyoko mabungeni.
Ujumbe pekee tunaoweza kumpa huyo Spika Ndugai na msaidizi wake Dr Tulia Ackson, kama hawatataka bunge letu lisifikie huko kulikofikiwa kwenye mabunge mengine duniani, watalazimika kujivua 'ukada' na wawe fair kwa wabunge wote bila kujali itikadi zao za kisiasa.
Lakini kama wataamua kupuuzia ushauri huu na wakaamua kuendelea kutumia 'mbeleko'yao ya Uspika kuibeba serikali basi watarajie ngumi zikichapwa humo bungeni siku si nyingi sana kutoka hivi sasa.
 
Huku unguja tuko powa viongozi wote wanaendelea na kazi, nimeshuhudia ving'ora gari zao zikipita,hivyo tuna uongozi kamili hadi uchaguzi mwengine
 
Uzuri wenyewe Mungu alimpa hekima mh rais ya kuwaona hawa ukawa kama watoto wanao stahili kuvumiliwa na kupewa malezi.

Na mimi na msisitiza rais aendelee kuwachukulia kama watoto. Na asisahau maandiko matakatifu yanasema usimnyime mtoto kiboko. Kiboko cha kutomnyia huyu mtoto ni kanuni za kuliendesha bunge. Kanuni hizi zirekebishwe iliziweze kuwapa hawa wajinga stahili yao.

Sasa si mrudishe mfumo wa chama kimoja tu, unafiki wa nini?
 
Walichofanya wabunge wa Ukawa ni sahihi kwa asilimia 100.
Huyo mama Naibu Spika Dr Tulia Ackson aliombwa mwongozo na nguli wa sheria hapa nchini Tundu Lissu kuhusu uhalali wa Dr Shein kuhudhuria bunge hilo akiwa na wadhifa wa Urais wakati Urais wake ulishakoma tokea tarehe 2/11/2015.
Lakini cha kushangaza Mwanasheria huyo alijibu mwongozo huo kwa lengo la kuibeba serikali 'iliyomzawadia' nafasi hiyo.
Alidai kuwa Katiba ya Zanzibar ya Zanzibar inaeleza kuwa Rais wa Zanzibar ataendelea kuwa Rais hadi Rais mwingine atakapoapishwa.
Hivi nimuulize swali moja tu dogo huyo Mwanasheria hivi iwapo hao wahafidhina wa CCM wataamua kutofanya uchaguzi wowote hata kwa kipindi cha miaka 10 ijayo, hivi bado huyo Dr Shein Urais wake utaendelea kuwa halali?
Hivi inawezekanaje huyo mwanasheria aliyebobea hadi kufikia kuwa na PhD ya sheria akaamua kujitoa ufahamu kwa lengo tu la kutumia ule msemo unaosema mtumikie ------ ili upate mradi wako?!

acha kutoa mapovu wewe, hujui kuwa uchaguzi wa marudio umesha tangazwa kuwa utafanyika? mipango yenu ya kuihujumu serikali ya awamu ya tano ya JMT haitafanikiwa. kaa ukijua hilo.
 
natumia neno zuri mpumbavu ni wewe usiejua kuwa watu wanaendesha political consipiracy zao kwa mgongo wa znz.


Unastaili kuwa mpumbafu kwasababu mbumbafu ujilidhisha nafsi yake kwa upumbaf sasa kama wewe unaona yanayotokea zanzibar ni thawa endelea kwa upumbaf wako...akili zako na viongzi wako ndiyo wanaotia aibu uafrika...
 
Hata hivyo huyo Ndugai aache mikwara yake ya kitoto...........
Eti anadai siku zijazo hataweza kuvumilia wale wanaoleta vurugu bungeni.
Hivi anataka kutwambia kuwa anataka kuwachapa bakora wabunge wenzake kama ambavyo alivyomchapa yule mgombea mwenzie wa ubunge kwenye kura za maoni za CCM kule jimboni kwake Kongwa?
Huo mkwara wake hautafua dafu, badala yake huyo Ndugai kama atatekeleza huo mkwara wake itakuwa tu kama anataka kuugeuza ukumbi wa bunge kuwa boxing ring kwa kuwa hakuna mbunge yeyote wa upinzani atakayekubali kuchapwa bakora kirahisi kama alivyokubali yule mgombea mwenzie wa ubunge kule Kongwa.
 
"Zomea zomea" ni njia moja ya kufikisha ujumbe.

Mimi sikusikia zomea zomea, nilisikia wakisema "Maalim Seif, Maalim Seif".

CCM na Rais aliyetangazwa na NEC amepata ujumbe...waheshimu maamuzi ya wapiga kura wa Zanzibar. Unaweza kujibu ni kwa nini ZEC haikumtangaza Dr. Shein kuwa mshindi wa Urais?



Uhuni na dhuluma itaharibu kisiwa cha amani na utulivu.
Unaikumbuka KANU? KANU ya Kenya.


Unazungumzia KANU ya kenya hapa? ambayo mlikuwa mnadangwanya na kingunge wakati wa kampeni kuwa CCM imeishiwa na pumzi na itakuwa kama KANU na the likes. Na kwa vile ni wajinga mkawa mkimshangilia, huku mkisahau kuwa walio kuwa wana ikaba CCM ikose pumzi ni haohao waliondoka CCM na kuja kuwakaba UKIWA/CDM.
 
Last edited by a moderator:
Hiv niulize tu ikiwa Shen akiachia madaraka nani atakuwa MKUU mpaka Uchaguz wakati mwingine UKAWA tumien akili Au ndo yule FORM 6 DJ kashawachanganya na viti maalumu vyake?

Kwaani Znz hawakufanya uchaguzi? na mshindi anajulikana huyo ndy anatakiwa kuwa rais
 
Ni pale Wabunge walio aminiwa na kupewa dhamana na wananchi kuwa wakilisha bungeni wanapotumia uhuru na haki hii ya kidemokrasia kufanya ghasia za zomeazomea.

ni maoni yangu tufike mahali sasa tusi ivumilie hii tabia ya baadhi ya wabunge wetu.

Mh rais wa JMT JPM amezunguzia vizuri sana kuhusu majipu yanayo lisumbua taifa letu, ambayo yeye binafsi kajitolea kuyakamua ili taifa hili lipone.

bila kumungunya maneno hii tabia tuliyoiona bungeni ni moja ya hayo majipu. tena hili jipu lina kiini chake ambacho ni hatarishi sana. lisiposhughulikiwa kwa muda muuafaka jipu hili litageuka kuwa kansa. hebu tujiulize hivi hawa wabunge wangekaidi amri ya spika Ndungai ya kutoka nje kwa hiari yao ni nini kingetoke, kumbuka pale alikuwapo amiri jeshi mkuu wa majeshi yetu


sasa mheshimiwa rais tunakuomba hebu kamua jipu hili linaloendelea kukua hapo bungeni. tafahali jamani tusiendelee kupuuzua hii hali. Na andika hivi ni kijua rais ni sehemu ya bunge kwa mujibu wa katiba yetu.
mwambie seini aachie madaraka wazizabari hawamtakiiiiiiiiiiiiiiii
 
Unastaili kuwa mpumbafu kwasababu mbumbafu ujilidhisha nafsi yake kwa upumbaf sasa kama wewe unaona yanayotokea zanzibar ni thawa endelea kwa upumbaf wako...akili zako na viongzi wako ndiyo wanaotia aibu uafrika...

wewe na mwezako mnazani matusi yanasomewa chuoni sio? natumia tena neno zuri, wapumbavu.
 
Sasa si mrudishe mfumo wa chama kimoja tu, unafiki wa nini?

wanafiki ni wale walioenda bungeni Dodoma huku wakijua kuna mambo hawakubaliani nayo, ndio maana hata hao mabwana zao huko ulaya wanaoenda kuwalilia kila wakati safari hii wamewapuuza baada ya kujua ujinga wao.
 
natumia neno zuri mpumbavu ni wewe usiejua kuwa watu wanaendesha political consipiracy zao kwa mgongo wa znz.

Na cha ajabu ni kwamba hapo walipofanya fujo ni znz? Ama aliyekuwa anahutubia bunge ni Shein? Tunapokwenda sipo
 
Tanzania democracy bado sana hata baadhi ya wananchi hayaelewiki maana ya democracy na pia watanganyika majority hawajui haki zao mtu yuko tayari kununua haki yake.Ushauri:rudisheni utawala wa chama kimoja au usultani kwani wengi hawaelewi
 
Ndo maana waafrica tunadharauliwa yaani sio viongozi wala wananchi wa kawaida wananchi wakawaida wapo tayarri tetea upumbavu kwa sababu ya mapenzi yao kwa chama flani kwa ambacho ccm inakifanya haitakiwi watu kuchekea hata kidogo suala la znz limejaaa figisu matokeo yanafutwa wakati huo huo matokeo ya upande mwingine yabakubaliwa hivi nyinyi mnaotetea huu upuzi mmekuwa wehu kiasi gani mbona mnatia aibu yaani mmeshindwa ng'amua upuuzi ambao unaonekana kwa macho this is shame hatutokaa tupige hatua hata siku moja kwa mitazamo hii,

Na kwa kinachoendelea bungeni sasa hivi ni jambo la kupongeza sana maana hakuna namna nyingine yakuweza fikisha ujumbe, eti kuna ma mtu humu wanasema si muende mahakamani wamejitoa fahamu kiasi cha kushindwa elewa kuwa hata muhimili wa mahakama unaegemea upande wa serikal ni aibu sanaa
 
acha kutoa mapovu wewe, hujui kuwa uchaguzi wa marudio umesha tangazwa kuwa utafanyika? mipango yenu ya kuihujumu serikali ya awamu ya tano ya JMT haitafanikiwa. kaa ukijua hilo.
Kurudia uchaguzi ni swala moja, lakini jiulize swali lingine la ziada ambalo ni la muhimu sana, hivi ikitokea na uchaguzi mwingine ukafanywa na ikatokea Maalim Seif akashinda tena na ukafutwa kwa mara nyingine na ukarudiwa tena na hao maccm wahafidhina wakaufuta tena, ndipo hapo ninapomuuliza huyo mwanasheria aliyebobea Dr Tulia Ackson kuwa bado hoja yake aliyoitoa bungeni jana kuwa Rais wa Zanzibar ataendelea kuwa Rais halali hadi pale Rais mwingine atakapoapishwa itaendelea kufanya kazi?
Vile vile tusiwe wepesi wa kusahau, ni mwaka jana tu kule kwenye Bunge la Katiba, mwanamama mmoja wa Zanzibar anayeitwa Asha Bakari alieleza waziwazi msimamo wa serikali ya CCM kule Zanzibar kuwa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kamwe haitakuja kutolewa kwa 'vikaratasi' vya kura!
Cha kushangaza sana aliyekuwa Spika wa Bunge hilo Samuel Sitta alimuacha mama huyo ayaongee maneno hayo hatari sana bila kumkatisha huku akiwaacha wabunge wenzake wa CCM wakimshangilia kwa nguvu zao zote!
Kama kweli serikali yetu ingekuwa inaendeshwa kwa utawala wa sheria huyo mama kwa wakati huu angekuwa anaozea jela!
Lakini badala yake yupo mitaani akipeta kwa kuwa alichoongea kwenye BMK ndicho hicho tulichokiona kwa huyo mtu anayeitwa Jecha kumpora waziwazi Maalim Seif ushindi wake wa dhahiri alioupata kwenye uchaguzi uliofanyika tarehe 25/10/2015.
 
Unazungumzia KANU ya kenya hapa? ambayo mlikuwa mnadangwanya na kingunge wakati wa kampeni kuwa CCM imeishiwa na pumzi na itakuwa kama KANU na the likes. Na kwa vile ni wajinga mkawa mkimshangilia, huku mkisahau kuwa walio kuwa wana ikaba CCM ikose pumzi ni haohao waliondoka CCM na kuja kuwakaba UKIWA/CDM.
CCM ilikwisha zamani ndugu. Sasa imebakia magari 777 ya maji washawasha na "bring back our General". Nje ya hilo ni DOMOkrasi tu.

Piga mahesabu ya mlalahoi waliopatiwa "maisha bora" na CCM. CCM ina wanachama ngapi?

Upinzani wote wana wanachama ngapi?

Ukijua haya mahesabu utajua Uchaguzi hapa Tz ni maigizo na ukamilisho tu wa utaratibu wa kupata kibali cha kwenda kutembeza bakuli.
 
Kurudia uchaguzi ni swala moja, lakini jiulize swali lingine la ziada ambalo ni la muhimu sana, hivi ikitokea na uchaguzi mwingine ukafanywa na ikatokea Maalim Seif akashinda tena na ukafutwa kwa mara nyingine na ukarudiwa tena na hao maccm wahafidhina wakaufuta tena, ndipo hapo ninapomuuliza huyo mwanasheria aliyebobea Dr Tulia Ackson kuwa bado hoja yake aliyoitoa bungeni jana kuwa Rais wa Zanzibar ataendelea kuwa Rais halali hadi pale Rais mwingine atakapoapishwa itaendelea kufanya kazi?
Vile vile tusiwe wepesi wa kusahau, ni mwaka jana tu kule kwenye Bunge la Katiba, mwanamama mmoja wa Zanzibar anayeitwa Asha Bakari alieleza waziwazi msimamo wa serikali ya CCM kule Zanzibar kuwa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kamwe haitakuja kutolewa kwa 'vikaratasi' vya kura!
Cha kushangaza sana aliyekuwa Spika wa Bunge hilo Samuel Sitta alimuacha mama huyo ayaongee maneno hayo hatari sana bila kumkatisha huku akiwaacha wabunge wenzake wa CCM wakimshangilia kwa nguvu zao zote!
Kama kweli serikali yetu ingekuwa inaendeshwa kwa utawala wa sheria huyo mama kwa wakati huu angekuwa anaozea jela!
Lakini badala yake yupo mitaani akipeta kwa kuwa alichoongea kwenye BMK ndicho hicho tulichokiona kwa huyo mtu anayeitwa Jecha kumpora waziwazi Maalim Seif ushindi wake wa dhahiri alioupata kwenye uchaguzi uliofanyika tarehe 25/10/2015.

mimi na amini kama maalimu Seif hatachukua jukumu la zec kujitangazia matokeo hakuna kitakacho haribika huko zenji kwenye uchaguzi wa marudio.
 
Back
Top Bottom