Democrats na unafiki huu......

Mkuu lini mtaacha kuitegemea serikali tena ya nchi nyingine?????

Aliesema tuitegemee nani?
mimi nasema wao kujitangaza kuwa
watu wa kuisaidia Africa huku wanafanya kinyume ni unafiki

bora wanyamaze

halafu nimezungumzia watu kuwa na pesa ya kusoma Marekani
na kunyimwa visa while wanajitangaza dunia nzima kuwa na best colleges
na wanaruhusu watu wa nchi zingine bila vikwazo
mfani Israel
 

Bakuli?
 

Kwa haraka haraka ni analysis nzuri ila kwa undani mkuu bado hujafanya utafiti hakuna kitu cha bure hao republican wanatoa sana na ndo wanaongoza kwa kutunyonya africa. Obama na democratic wenzake hawatoa sana ila ndo salama yetu ya kupunguzwa kunyonywa. Politics ni win- win situation hakuna wazungu wanaowapenda waafrika chini ya jua hili. Wapo kwa maslahi yao na wao wanasema wazi "God bless America and America only"

Obama alipokuwa Misri awamu yake ya kwanza tu alituambia ukweli ni wakati wa Afrika kujisimamia wenyewe na kutumia raslimali zetu wenyewe kujiendeleza na kondokana na tabia ya ombaomba ambayo anajua kila wanapotupa wao wanatafuta namna ya kuchukua kikubwa zaidi. Huu ndo ukweli hata kama ni mchungu

Xi Jinping kaja hapa kasaini mikataba kama ni ya heri kwa nini wasiiweke wazi sie tunabaki kuambiwa ni mikataba ya kutusaidia ili nasie tuendelee wapi na wapi kwani sie ndugu zao mpaka watupe msaada mbona kwao kuna ombaomba kibao hawawasaidii waondokane na ombaomba hiyo kama kweli wanautu.

Nampongeza sana Obama na naomba aendelee kukata misaada ili tujifunze sema baada ya mchina tu kuja naye kaamua kuja hapa kinachofuata utasikia tumepewa mabilioni ya pesa halafu mikataba itasainiwa watu wajenge military base kigamboni fasta na mingine ya uranium na mafuta na gesi na madini ambayo kama Bush hakuwa ameyasaini.

Bush katupa vyandarua ndo wakumsifia wakati wanamikataba kibao ya kuchukua madini yetu..... basi mkuu ngoja niishie hapa naanza kupata hasira nisije kuharibu keyboard ya PC yangu na nikajikuta nimekula ban bure. "Think big" The Boss
 
Last edited by a moderator:
Reactions: EMT
The Boss siyo Marekani tuu, nchi nyingi zimeacha kutoa aid kwa South Africa.

Uingereza nayo imetangaza rasmi kuacha kuipa South Afrika aid kuanzia mwaka 2015: BBC News - South Africa criticises UK decision to end direct aid

Ifike mahali tujitegemee. Kutegemea misaada won't get us anywhere.

We have the means, we have the resources so badala ya kuzivuja, lets utilise them effectively.

Our relations with developed countries should be based on trade na siyo misaada.

Jana nimesoma mabilioni ya dola yatamwaga Congo jiulize kwa nini wakati nchi ina resources nyingi hivyo.
 

Democraps ndiyo salama yetu? You are seriously laboring under a major misapprehension!

Politics ni win- win situation hakuna wazungu wanaowapenda waafrika chini ya jua hili.

Je, wapo Waafrika wanaowapenda Wazungu chini ya jua hili?
 
Waafrika tuacheni kutegemea misaada.

Kitu kikishakuwa msaada huwezi kukipangia masharti.

Bora hata Jadakiss - raia wa Marekani- anaposema "Why they ain't give us the cure for AIDS?" (Jadakiss -Why?) anaweza kulalamika kwamba serikali ya Marekani itumie kodi yake kuweka mazingira mazuri ya AIDS research.

Sie waafrika kwa nini tusifanye mambo yetu mpaka kutegemea wengine? Wakitaka kututawala kwa kuwa tu wategemezi tutasemaje?

Waswahili wanasema "Cha mtu mavi"

Mbona mnakikodolea?
 

Very well said. Tuache sera za mabakuli
 


Sikusema tusijitegemee
kujitegemea nayo ni process
halafu Marekani ina watu ndani ambao ni political base ya Democrats
ambao wanataka Obama asaidie Africa
kama ambavyo kuisaidia Israel ni political pia kwa siasa za Marekani

Usisahau waathirika wote wa HIV Tz wanapata dawa bure sababu ya PEPFAR aliyoanzisha Bush
kui cancel now eti ili ujitegemee ni kuhukumu watu vifo
 

Yaani mkuu The Boss serikali yako ina pesa za kumsafirisha rais na masafara wake kila kukicha
Lakini haina hela hata ya kuwasaidia waathirika?
Miaka 50 plus imepita most of African states zipate uhuru sasa hiyo process ya kujitegemea unataka miaka mingapi? 1000???
 

Now this is politics
ungekuwa HIV Positive usingesema
 

OBAMA anatufaa zaidi kuliko Bush, tumezoea vya kupewa, ifikie mahali tutafute vya kwetu na kujitegemea,
hv bara la Afrika na nchi tajiri kama ya kwetu hatuoni aibu kutembeza bakuli kama matonya kila siku, kwann tusitumie akili kidogo tuzalishe na kuwakopesha wamarekani kama china inavyofanya sasa hivi? ningepata nafasi ya kuongea na obama ningemwambia asilete hata shilingi moja ya tz kwa bara la Afrika ili tujifunze kujitegemea. cha kusikitisha zaidi, hata hela wanazotupa nyingi zinaliwa na wajanja wa mjini
 

Mkuu msaada wa Arv kutoka USA ni moja ya gesture kubwa wanaaonyesha wamarekani kuwa bado wanathamini uwepo wa muafrika . Tatizo letu kitu tukipewa bure basi tuna assume kuwa kitu hicho ni rahisi. Gharama za dawa za Arv na Tb kwa mwezi ni karibu dola 600 kwa mtu mmoja, na hiyo ni generic version! Nchi kama RSA ambayo ina uchumi imara inategemea msaada huo , Sidhani kama kuna nchi nyingine Africa inaweza kumudu gharama hizi kwa wananchi wake. Bill clinton na wenzake ndo walifanya lobying na wenye viwanda vya madawa vilivyokuwa vina formula ya Arv, ndo ikapatikana hiyo generic Arv. Kama msaada huo wa Arv utaondolewa hali itakuwa mbaya kuliko unayodhani!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…