Dell latitude d630 haitaki kupokea mzigo

Dell latitude d630 haitaki kupokea mzigo

kama HDD ingekuwa imekufa window xp pro sp3 isinge ingia ila ili tatizo nimekumbana nalo kwa mara ya tano kwa pc tofauti na nimegundua kuwa baada ya kuformat sana pc HDD inaanza kubagua window na window ya kwanza kubaguliwa huwa ni 7 home pre alafu pro then 8 alafu ultimate ndio zinakuja hizi ndogo ndogo za vista na pro sp1 na 2 lakini 3 huwa inaingia na tatizo kubwa huanzia kwenye DVD rom kwasababu ni external naomba nikuulize swali huwa unatumia dvd yako kuangalizia movie za dvd esp alibaba na blu rays?

asante bwana Srebrina ! mkuu sidhani kama hii DVD rom (RW) ina shida! manake hapo mwanzo nilikuwa naweza kuinstall hata kwa setup ya Windows 7 niliyoisave ndani ya local disc, lakini sasa inagoma! DVD huwa situmii, mara chache huwa nacopy na kuangalia baadae kama softcopy!
 
Last edited by a moderator:
hilo tatizo ni hard disk fail, period.
lilishawahi kutokea kwangu kitambo mwisho hard disk ikafa kabisa, ipo tu makumbusho yangu.
 
Hapana CD zake zinawezekana hazina shida. Kwa maana hiyo upande wa software nikiwa na maana OS CDs zake zinawezekana ni nzima kabisa. Hatua ya pili anatakiwa kubadili HDD na kutumia nyingine ambayo ana uhakika ni nzima. Endapo tatatizo litaendelea basi atoe RAM/DDR zote kwenye slots zake then apachike moja kisha aanze tena kupandisha Operating system au abadili kabisa aweke amabazo ana uhakika kwamba ni nzima ama amezitoa katika mashine ambayo ni nzima. Hilo nalo nilikataa option ya mwisho aangalie je Processor yake inafanya kazi vizuri, akitaka kujua kama inafanya kazi viziri awashe mashine then aguse heat sink na kuangalia kama inapata joto la kutosha. Kama joto lake sio la kutosha basi na efficiency yake itakuwa sio nzuri sana. pia anaweza akachukua jukumu la kubadili Processor alafu aendelee ku-install Operating System. Hope hapo atapata ufumbuzi.
Nimependa ufafanuzi wako ila tatizo ni hili je watu wangapi wana RAM/HDD za akiba au kuwa na access ya kuazima hata kwa rafiki? Unapoongelea joto la kutosha ni kiasi gani kwenye CPU na unatumia nini kujua kama hilo joto linatosha, pungufu au Limezidi? Nafikiri ikifikia wakati wa kujua km processor ni nzuri, bora kuipeleka kwa fundi. Ila kwa ushauri wangu processor na shida aliyonayo havina uhusiano wa karibu sana. Bei ya processor ni karibu sawa na bei ya used laptop kwa maana hiyo sioni km ni idea nzuri kununua cpu nyingine kuinstall kwenye used laptop. Km kazi yako ni kutengeneza computer karibu 99.99% ya matatizo yatakuwa nje ya cpu yenyewe.
 
Back
Top Bottom