ntabhaligwa
Senior Member
- Jan 2, 2017
- 141
- 104
Kwa miaka mingi njia ya majadiliano ya hoja zinazokinzana maarufu kama 'debate' imekuwa ni kivutio kikubwa kwa wasikilizaji, sio tu kwa mada zinazojadiliwa bali hata kwa namna na mtindo wa uwasilishaji. Sasa hivi debate zimebaki mashulen na vyuon zaidi. Gwiji wa debate (pengine ndie mtu aliyefanya debate nyingi sana kuliko mtu yeyote duniani) Shk Ahmed Deedat atakumbukwa kwa uwezo wake mkubwa wa kujenga hoja na kujibu maswali baada ya debate, Aliwahi kuomba debate na Papa wa R.C kwa miongo kadhaa na kuahid kugharamia gharama zote zitakazotokana na debate lakin Papa alikataa! Pengine hapo ndio linakuja suala la katika majadiliano upo upande gani? una ujuz wa kutosha wa unachokitetea?Yote ikiwa unayo linabaki moja Je unatetea haki na ukweli? Ahmed deedat alishinda deebate nyingi kwa sababu licha ya kuwa na uwezo mkubwa wa kujenga hoja alitetea haki na ukweli. Shk Deedat aliacha wanafunz kadhaa lakin aliyejitokeza kuwa na kipaji kikubwa ni Dr. Zakir Naik. Hebu tujikumbushe debate maarufu iliyofanyika Marekan ikimhusisha Dr. William Campbel na Dr. zakir Naik katika mada 'The Quran & the Bible in the light of science.