Dear waziri wa nishati

abunerimgaya

Member
Nov 13, 2012
78
15
Dear Waziri wa Nishati, Nna uhakika kwamba wizara yako inajua kuhusu teknolojia ya uzalishaji wa gesi kwa kutumia takataka,kwani najua kuna viwanda vichache vinatumia teknolojia hii kujizalishia umeme unaoendeshwa na gesi itokanayo na takataka baada ya uzalishaji wa bidhaa zao. Jambo ambalo silijui ni kwamba je, wizara yako ina mpango gani kuhusu hili? Nina uhakika kwamba endapo hili litasimamiwa na kufanyiwa kazi vizuri, mambo mawili mazuri yatajitokeza:

1. Umeme utapatikana, tena kwa
gharama nafuu kabisa.
2. Mazingira yetu yatakuwa safi

Wakati wote kilio cha wananchi kukerwa na madampo kitaisha. Nina uhakika pia kuwa unapotembelea nchi za wenzetu unaliona hili. Tafadhali mzee, LIFANYIE KAZI!
Ni mimi Mwananchi ...
 
Back
Top Bottom