Dean Ambrose awa Bingwa mpya wa WWE

escrow one

JF-Expert Member
Nov 29, 2014
1,472
2,867
Mwanamieleka nguli Dean Ambrose hapo Jana katika Money in the bank ppv aliibuka Bingwa mpya wa WWE WORLD HEAVYWEIGHT baada ya kumshinda Seth Rollins.

Awali Seth Rollins aliibuka mshindi dhidi ya mpinzani wake na bingwa wa zamani Roman Reigns. Ubingwa wa Seth haukudumu sana kwani muda kidogo baadae Dean Ambrose aliibuka na briefcase ya Money in the bank contract na hivyo mechi kuanza upya na kushuhudia Dean akiibuka mshindi.

Dean Ambrose, Seth Rollins na Roman Reigns kwa pamoja walishawahi kuunda kundi linalojulikana kama The Shield kabla ya kusambaratika.

Matokeo mengine ya Money in the bank ppv

Dean Ambrose anyakua briefcase ya Money in the bank contract na kuwashinda Chris Jericho, Sami Zayn, Kevin Owens, Alberto De Rio na Cesaro. Hii ndiyo ilimsaidia kuwa bingwa mpya.

Aj Styles ameeibuka mshindi dhidi ya John Cena.

New day wametetea ubingwa wao wa Tag Team.

Rusev ametetea ubingwa wake wa US title.
 
Back
Top Bottom