Deadline yangu mwakani, ndoa lazima nifunge

Ms Judith

JF-Expert Member
Dec 24, 2010
2,563
918
1.
Kila niwapo salani, naomba mola nichunge,
Nipatetinga ndoani, upendo wako nipunge,
Niishi kama peponi, dunia isinizonge,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

2.
Butege aliuliza, kwa vipi ningali misi,
Hoja yake kakuza, wangu huu si halisi,
Hata bila kuuliza, yeye kajipa makisi,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge.

3.
Kweli wengi nimeepa, wachumba pia washenga,
Walokuwa na za epa, wote walipigwa chenga,
Walonukia vikwapa, kwa wao huo mpunga,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

4.
Walianza praimari, nikiwa bado kichanga,
Enzi zile sekondari, wengi walijiunga,
Chuo hakika hatari, kama vya hari vimbunga,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

5.
Kutunza bikira kazi, katika hii dunia,
Wengi waruka wazazi, kwa zao mbaya tabia,
Ya siri sasa ya wazi, wapi bikira tunzia,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

6.
Namshukuru Manani, himeni yangu salama,
Hadi huko mwakani, haitotiwa alama,
Wala siweki sokoni, yake wangu kujinoma,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

7.
Maisha yetu mabinti, kweli yataka hesabu,
Ili kupata pointi, liwe sahihi jawabu,
Ukihaha nazo senti, tachacha kama ulabu,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

8.
Miaka inapopaa, nawe wapaswa jipanga,
Ni nani wa kukufaa, lazima kichwa kugonga,
Japo awe msambaa, tabibu au mchunga,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

9.
Mimi yangu tayari, ndoa ni hapo mwakani,
mlio nayo mahari, sasa leteni ukweni,
hima leteni habari, ya ndoa ilo makini,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

10.
Nawaaga mabachala, nao wenye masitazi,
wapweke na makapela, usingo hakika kazi,
hata ukiwa na hela, hazikwishi jinamizi
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
 
mmh, sijakuelewa hapo. weka kamstari japo kamoja nawe ujaribu vina na mizani basi. hahah.

mzima lakini, ulipotea sana na nilikumiss

Mimi mzima ndugu, hapo kwenye kuweka vina na mizani usiwe na wasi wasi,, ndo namalizia ubeti wa mwisho halafu nitamtuma mshenga aje kughani kwenu,,, ila natumaini na yeye hutamkwepa kama ulivyotanabaisha kwenye ubeti wa tatu.....

Tulimisiana kwa kweli:tea:
 
Mungu Akubariki malengo yatimie nikapata Muda nirtaweka mashairi kukusaidia
 
hodi hodi naingia, naomba nipokeeni
miss nakusalimia, bibie u hali gani?
waanza kufurahia, ndoa ya hapo mwakani
mchumba hatujamjua,usitufiche jamani

mbona umejiamini , kwenye lako shairi
ni lazima mwakani, hakuna hili na hili
muowaji ni nani ?, umeificha kauli
hapa kuna siri gani?, taja ubavu wa pili

yupo hapa jeiefu?, suala najiuliza
ni upi wake wasifu?, shule ameshamaliza?
macho yake ni kipofu? au ana makengeza?
utatujuza halafu? , maelezo yako giza

kama haujampata, mbona umejiamini?
kwa makeke mejikita,lazima iwe mwakani
kama unamtafuta , usiweke dedilaini
yasije yakakukuta, ukakimbia jamvini

naomba ufafanuzi, nipate kukuelewa
nisije nikakuuzi , mke wa mtarajiwa
pengine ni mwanafunzi, shairi sijaelewa
kipenzi wangu laazizi , naomba fafanuliwa

na kama ni siri yako, usihofu endelea
harusi sio maziko , dua tunakuombea
ufurahi na mwenzako, kama ushajipatia
au kesho aje kwako, kama wajitafutia
 
Kama hilo shairi umejiimbia wewe basi mimi na mke wangu tunakutakia ndoa njema. Lakini ubeti wa kwanza kwamba uishi hapa duniani kama peponi sidhani, kumbuka hapa duniani hata Yesu alijaribiwa.

Kila la kheri twakutakia, mchango wetu elfu thelathini (isiwe ndoa ya kifahari please)
 
1.
Kila niwapo salani, naomba mola nichunge,
Nipatetinga ndoani, upendo wako nipunge,
Niishi kama peponi, dunia isinizonge,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

2.
Butege aliuliza, kwa vipi ningali misi,
Hoja yake kakuza, wangu huu si halisi,
Hata bila kuuliza, yeye kajipa makisi,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge.

3.
Kweli wengi nimeepa, wachumba pia washenga,
Walokuwa na za epa, wote walipigwa chenga,
Walonukia vikwapa, kwa wao huo mpunga,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

4.
Walianza praimari, nikiwa bado kichanga,
Enzi zile sekondari, wengi walijiunga,
Chuo hakika hatari, kama vya hari vimbunga,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

5.
Kutunza bikira kazi, katika hii dunia,
Wengi waruka wazazi, kwa zao mbaya tabia,
Ya siri sasa ya wazi, wapi bikira tunzia,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

6.
Namshukuru Manani, himeni yangu salama,
Hadi huko mwakani, haitotiwa alama,
Wala siweki sokoni, yake wangu kujinoma,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

7.
Maisha yetu mabinti, kweli yataka hesabu,
Ili kupata pointi, liwe sahihi jawabu,
Ukihaha nazo senti, tachacha kama ulabu,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

8.
Miaka inapopaa, nawe wapaswa jipanga,
Ni nani wa kukufaa, lazima kichwa kugonga,
Japo awe msambaa, tabibu au mchunga,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

9.
Mimi yangu tayari, ndoa ni hapo mwakani,
mlio nayo mahari, sasa leteni ukweni,
hima leteni habari, ya ndoa ilo makini,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

10.
Nawaaga mabachala, nao wenye masitazi,
wapweke na makapela, usingo hakika kazi,
hata ukiwa na hela, hazikwishi jinamizi
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

Kila la heri Judy. Kwa michango yako hapa jamvini miye nakuona ni mtu makini sana hivyo huyo atakayebahatika kukuoa atapata mke mwema na ndoa yenu itadumu kwa miaka mingi.






 
1.
Kila niwapo salani, naomba mola nichunge,
Nipatetinga ndoani, upendo wako nipunge,
Niishi kama peponi, dunia isinizonge,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

2.
Butege aliuliza, kwa vipi ningali misi,
Hoja yake kakuza, wangu huu si halisi,
Hata bila kuuliza, yeye kajipa makisi,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge.

3.
Kweli wengi nimeepa, wachumba pia washenga,
Walokuwa na za epa, wote walipigwa chenga,
Walonukia vikwapa, kwa wao huo mpunga,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

4.
Walianza praimari, nikiwa bado kichanga,
Enzi zile sekondari, wengi walijiunga,
Chuo hakika hatari, kama vya hari vimbunga,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

5.
Kutunza bikira kazi, katika hii dunia,
Wengi waruka wazazi, kwa zao mbaya tabia,
Ya siri sasa ya wazi, wapi bikira tunzia,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

6.
Namshukuru Manani, himeni yangu salama,
Hadi huko mwakani, haitotiwa alama,
Wala siweki sokoni, yake wangu kujinoma,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

7.
Maisha yetu mabinti, kweli yataka hesabu,
Ili kupata pointi, liwe sahihi jawabu,
Ukihaha nazo senti, tachacha kama ulabu,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

8.
Miaka inapopaa, nawe wapaswa jipanga,
Ni nani wa kukufaa, lazima kichwa kugonga,
Japo awe msambaa, tabibu au mchunga,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

9.
Mimi yangu tayari, ndoa ni hapo mwakani,
mlio nayo mahari, sasa leteni ukweni,
hima leteni habari, ya ndoa ilo makini,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

10.
Nawaaga mabachala, nao wenye masitazi,
wapweke na makapela, usingo hakika kazi,
hata ukiwa na hela, hazikwishi jinamizi
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge

Hivi hii si ingeenda kule kwenye forum ya burudani? Au ungetoa single. Halafu wewe ni Miss Judith na yule mwimbaji wa ubongo wa flavour (JeyD) ni Judith Wambura, ndio huyo huyo au tofauti?
 
muweke Muumba Mbele, kwa unayojipangia
Akupe baraka tele, mwenza kukupatia
sali na omba milele, utakacho kitamea
Nakutakia lakheri, Katika yako mipango

Miss uwe misezi, dada uitwe mama
upate watoto shazi, maisha yawe mema
Upate mme mlezi, shida zenu kuzizima
Nakutakia lakheri, Katika yako mipango

funzadume mwana wa washawasha
 
hodi hodi naingia, naomba nipokeeni
miss nakusalimia, bibie u hali gani?
waanza kufurahia, ndoa ya hapo mwakani
mchumba hatujamjua,usitufiche jamani

mbona umejiamini , kwenye lako shairi
ni lazima mwakani, hakuna hili na hili
muowaji ni nani ?, umeificha kauli
hapa kuna siri gani?, taja ubavu wa pili

yupo hapa jeiefu?, suala najiuliza
ni upi wake wasifu?, shule ameshamaliza?
macho yake ni kipofu? au ana makengeza?
utatujuza halafu? , maelezo yako giza

kama haujampata, mbona umejiamini?
kwa makeke mejikita,lazima iwe mwakani
kama unamtafuta , usiweke dedilaini
yasije yakakukuta, ukakimbia jamvini

naomba ufafanuzi, nipate kukuelewa
nisije nikakuuzi , mke wa mtarajiwa
pengine ni mwanafunzi, shairi sijaelewa
kipenzi wangu laazizi , naomba fafanuliwa

na kama ni siri yako, usihofu endelea
harusi sio maziko , dua tunakuombea
ufurahi na mwenzako, kama ushajipatia
au kesho aje kwako, kama wajitafutia

Asante klorokwini, mistari yako makini,
Karibu sana ukweni, sote tutakuthamini,
Kama hujawa ndoani, nawe wafaa kundini,
Beti ya tisa makini, bado ni mchakatoni,

Beti ya tisa I wazi, mchumba bado kupata,
japo kumpata kazi, kwalo siwezi kudata,
Mwakani hilo ni wazi, lazima nitakamata
Beti ya tisa makini, bado ni mchakatoni,

Walojitokeza kenda, watatu walizimia,
Vitendo wakavitenda, subira kuazimia,
Mie nikubali tenda, mlango wafungulia
Beti ya tisa makini, bado ni mchakatoni,

Kauli sikuitoa, nani wa kumkubali,
Masomo yalizingia, ratiba ikawa kali,
Muda kusubiria, hadi ifaapo hali,
Beti ya tisa makini, bado ni mchakatoni,

Jiamini sina budi, japo bado kumpata,
Sina walau ahadi, nachanga vyema karata,
Taweka hata miadi, moja lazima tanata
Beti ya tisa makini, bado ni mchakatoni,
 
muweke Muumba Mbele, kwa unayojipangia
Akupe baraka tele, mwenza kukupatia
sali na omba milele, utakacho kitamea
Nakutakia lakheri, Katika yako mipango

Miss uwe misezi, dada uitwe mama
upate watoto shazi, maisha yawe mema
Upate mme mlezi, shida zenu kuzizima
Nakutakia lakheri, Katika yako mipango

funzadume mwana wa washawasha

asante funzadume, kwa hizo zako Baraka,
mwema mwana wa kiume, najua hilo hakila,
wanena kama mtume, kwa yote uloandika,
Mola anipapo mume, duazo tazikumbuka,

Misi kuwa misezi, hilo jema hakika,
dada geuka mzazi, hizo za mola Baraka,
yakiwa mema malezi, shukuru kwazo fanaka,
Mola anipapo mume, duazo tazikumbuka,
 
Mimi mzima ndugu, hapo kwenye kuweka vina na mizani usiwe na wasi wasi,, ndo namalizia ubeti wa mwisho halafu nitamtuma mshenga aje kughani kwenu,,, ila natumaini na yeye hutamkwepa kama ulivyotanabaisha kwenye ubeti wa tatu.....

Tulimisiana kwa kweli:tea:

haha....

wako siwezimkwepa, hilo liko hadharani,
nafasi hiyo takupa, kama ukija makini,
mkono sitakutupa, takutia maanani,
kama waweza kulipa, jongea sasa ukweni
 
haha....

wako siwezimkwepa, hilo liko hadharani,
nafasi hiyo takupa, kama ukija makini,
mkono sitakutupa, takutia maanani,
kama waweza kulipa, jongea sasa ukweni

Miss Judith, all the best my dear!!!,
lakini italeta raha zaidi,
ukimpata mume anaejua kughani vilevile!!!!!
 
Mungu Akubariki malengo yatimie nikapata Muda nirtaweka mashairi kukusaidia

karibu mbona wasita, na muda waulilia,
hata pasipo vitita, vya muda utawezea,
shairi nalo lapita, wengi wanalimendea,
beti zipake mafuta, zing'are kusaidia
 
Back
Top Bottom