Ms Judith
JF-Expert Member
- Dec 24, 2010
- 2,563
- 918
1.
Kila niwapo salani, naomba mola nichunge,
Nipatetinga ndoani, upendo wako nipunge,
Niishi kama peponi, dunia isinizonge,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
2.
Butege aliuliza, kwa vipi ningali misi,
Hoja yake kakuza, wangu huu si halisi,
Hata bila kuuliza, yeye kajipa makisi,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge.
3.
Kweli wengi nimeepa, wachumba pia washenga,
Walokuwa na za epa, wote walipigwa chenga,
Walonukia vikwapa, kwa wao huo mpunga,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
4.
Walianza praimari, nikiwa bado kichanga,
Enzi zile sekondari, wengi walijiunga,
Chuo hakika hatari, kama vya hari vimbunga,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
5.
Kutunza bikira kazi, katika hii dunia,
Wengi waruka wazazi, kwa zao mbaya tabia,
Ya siri sasa ya wazi, wapi bikira tunzia,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
6.
Namshukuru Manani, himeni yangu salama,
Hadi huko mwakani, haitotiwa alama,
Wala siweki sokoni, yake wangu kujinoma,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
7.
Maisha yetu mabinti, kweli yataka hesabu,
Ili kupata pointi, liwe sahihi jawabu,
Ukihaha nazo senti, tachacha kama ulabu,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
8.
Miaka inapopaa, nawe wapaswa jipanga,
Ni nani wa kukufaa, lazima kichwa kugonga,
Japo awe msambaa, tabibu au mchunga,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
9.
Mimi yangu tayari, ndoa ni hapo mwakani,
mlio nayo mahari, sasa leteni ukweni,
hima leteni habari, ya ndoa ilo makini,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
10.
Nawaaga mabachala, nao wenye masitazi,
wapweke na makapela, usingo hakika kazi,
hata ukiwa na hela, hazikwishi jinamizi
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
Kila niwapo salani, naomba mola nichunge,
Nipatetinga ndoani, upendo wako nipunge,
Niishi kama peponi, dunia isinizonge,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
2.
Butege aliuliza, kwa vipi ningali misi,
Hoja yake kakuza, wangu huu si halisi,
Hata bila kuuliza, yeye kajipa makisi,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge.
3.
Kweli wengi nimeepa, wachumba pia washenga,
Walokuwa na za epa, wote walipigwa chenga,
Walonukia vikwapa, kwa wao huo mpunga,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
4.
Walianza praimari, nikiwa bado kichanga,
Enzi zile sekondari, wengi walijiunga,
Chuo hakika hatari, kama vya hari vimbunga,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
5.
Kutunza bikira kazi, katika hii dunia,
Wengi waruka wazazi, kwa zao mbaya tabia,
Ya siri sasa ya wazi, wapi bikira tunzia,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
6.
Namshukuru Manani, himeni yangu salama,
Hadi huko mwakani, haitotiwa alama,
Wala siweki sokoni, yake wangu kujinoma,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
7.
Maisha yetu mabinti, kweli yataka hesabu,
Ili kupata pointi, liwe sahihi jawabu,
Ukihaha nazo senti, tachacha kama ulabu,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
8.
Miaka inapopaa, nawe wapaswa jipanga,
Ni nani wa kukufaa, lazima kichwa kugonga,
Japo awe msambaa, tabibu au mchunga,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
9.
Mimi yangu tayari, ndoa ni hapo mwakani,
mlio nayo mahari, sasa leteni ukweni,
hima leteni habari, ya ndoa ilo makini,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
10.
Nawaaga mabachala, nao wenye masitazi,
wapweke na makapela, usingo hakika kazi,
hata ukiwa na hela, hazikwishi jinamizi
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge