DC Simanjiro arejeshwa JWTZ

DC Simanjiro arejeshwa JWTZ

Adharusi

JF-Expert Member
Joined
Jan 22, 2012
Posts
14,493
Reaction score
7,417
Mkuu wa wilaya Simanjiro Brigedia Jenerali Cosmas Kayombo amerudishwa makao makuu ya Jeshi la Wananchi kuendelea na kazi yake na kuiacha nafasi hiyo ya mkuu wa Wawilaya.

Maswali najiuliza..
Alipokuwa mkuu wa wilaya alikua anaingia katika vikao vya CCM kwa nafasi yake,sijui na kadi alishapewa,wanajeshi na maaskari awaruhisiwi kuwa wanachama, sasa itakuaje kwa huyu bwana katika utendaji wake?

Chanzo: gazeti la mwananchi la agosti 2

CC Ritz,H-D na wote CCM wenzangu.

Mimi ni mwanachama wa CCM ila Tanzania kwanza vyama baadae.

"Vox populi,Vox dei"
 
Mbona unajishutukia kama una oga bafu la nje,hatuna haja ya kujua uana chama wako
 
Nchi hii taab kweli! Yaani Brigadier General mzima kuwa Mkuu wa Wilaya? Au alishastaafu?
 
hivi hii nchi maccm yanaifananisha na shamba la bibi,ndo maana watu wanaposema vyombo vya usalama navyo ni ccm hawakosei.
 
weka chanzo cha habari.ila kama ni kweli haitakuwa mara ya kwanza kwani hata mnadhimu mkuu wa majeshi SAMWEL NDOMBA naye alishakuwa mkuu wa mkoa na kurudishwa jeshini na kupandishwa vyeo haraka haraka.KUNA NAFASI INAACHWA WAZI ANAENDA KUZIBA
 
Ni tatizo la kikatiba hili.Vyama vingi vilianzishwa kama geresha tu baada ya Mwl Nyerere kuwageuka na kuwaambia wakubali tu.
 
Hivi si walifutaga huu utaratibu na ikawa lazima kuchagua kimoja either siasa au kubakia jeshini?
 
weka chanzo cha habari.ila kama ni kweli haitakuwa mara ya kwanza kwani hata mnadhimu mkuu wa majeshi SAMWEL NDOMBA naye alishakuwa mkuu wa mkoa na kurudishwa jeshini na kupandishwa vyeo haraka haraka.KUNA NAFASI INAACHWA WAZI ANAENDA KUZIBA

Kwa maana hiyo, Askari wetu wanatumiwa vibaya na chama kilichoko madarakani. Kwa sababu wakiwa wakuu wa mikoa ama wilaya watatekeleza "ILANI" ya chama kilichoko madarakani na watakuwa ni sehemu ya chama hicho. Sasa wanaporudishwa Jeshini, si wanakuwa bado na viji-elements vya hicho chama? Je wataweza kweli kuilinda katiba endapo chama kilichopo madarakani kitapumzishwa kwa kutumia sanduku la kura? Nadhani kuna tatizo kidogo hapo! Na tuwaache askari wetu wafanye kazi zao za kulinda usalama wa taifa letu na watu wake, wasizifanye kazi za kisiasa!

Just thinking ......
 
Jibu analo Jaji Warioba, subirini atakavyowafanya hawa CCM, hata wafanyeje, ishakula kwao kwa huyu mzee.
 
Jeshi wasikubali kudhalilishwa zaidi.Brigedia Generali kuwa Mkuu wa Wilaya ni sawa na Profesa kuwa mwalimu wa Chekechea.Hizi nafasi wawaachie akina Juliana Shonza,Mwampamba na Mwingulu.
 
kwanza ndomba halafu huyu ! Au nchi inatawaliwa kijeshi ?
 
weka chanzo cha habari.ila kama ni kweli haitakuwa mara ya kwanza kwani hata mnadhimu mkuu wa majeshi SAMWEL NDOMBA naye alishakuwa mkuu wa mkoa na kurudishwa jeshini na kupandishwa vyeo haraka haraka.KUNA NAFASI INAACHWA WAZI ANAENDA KUZIBA

Chanzo gazeti la mwananchi la leo tr 2 agost,ukurasa wa saba juu kushoto
"Vox populi,Vox dei"
 
Kwa maana hiyo, Askari wetu wanatumiwa vibaya na chama kilichoko madarakani. Wanatumiwa kivipi? Kwa sababu wakiwa wakuu wa mikoa ama wilaya watatekeleza "ILANI" ya chama kilichoko madarakani na watakuwa ni sehemu ya chama hicho.. Sasa wanaporudishwa Jeshini, si wanakuwa bado na viji-elements vya hicho chama? Je wataweza kweli kuilinda katiba endapo chama kilichopo madarakani kitapumzishwa kwa kutumia sanduku la kura?. Nadhani kuna tatizo kidogo hapo! Na tuwaache askari wetu wafanye kazi zao za kulinda usalama wa taifa letu na watu wake, wasizifanye kazi za kisiasa!
Just thinking ......
Watumishi wote wa umma wa serkali kuu na serikali za mitaa wanatekeleza ilani ya chama kilichopo madarakani duniani kote, hivyo kwasasa kwa Tanzania wanatekeeza ilani ya CCM.Ni kwele kwa asilimia kubwa viongozi haswa wa kijeshi wa miaka hiyo ya zamani kwa namna moja au nyingine ni watumishi wa CCM, TANU Youth League ndio ilikuwa inaamua ajira yako. Ndio maana tunahitaji katiba mpya. Baada ya 2015 huenda unayoyataka yakatimie, tufanye kazi.
 
Back
Top Bottom